-
Matayo 13:3-9Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
3 Kisha akawaambia mambo mengi kwa kutumia mifano,+ kwa kusema: “Muangalie! Mupandaji alienda kupanda mbegu.+ 4 Wakati alikuwa anapanda, mbegu fulani zilianguka pembeni ya barabara, na ndege wakakuja na kuzikula.+ 5 Zingine zilianguka mahali kwenye miamba kwenye hapakukuwa udongo mwingi, na zikaota mara moja kwa sababu udongo haukukuwa mwingi.+ 6 Lakini wakati jua lilitokea, ziliungua na kukauka kwa sababu hazikukuwa na mizizi. 7 Zingine zilianguka katikati ya miiba, na miiba ikakomaa na kuzifinya.+ 8 Mbegu zingine pia zilianguka kwenye udongo muzuri, na zikaanza kuzaa matunda, hii mara mia moja (100) zaidi, ile mara makumi sita (60), na ile ingine mara makumi tatu (30).+ 9 Ule mwenye kuwa na masikio, asikilize.”+
-
-
Luka 8:5-8Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
5 “Mupandaji alienda kupanda mbegu zake. Wakati alikuwa anapanda, mbegu fulani zilianguka pembeni ya barabara na zikakanyangwa-kanyangwa, na ndege wa mbinguni wakazikula.+ 6 Zingine zilianguka kwenye mwamba, na kisha kuota, zikakauka kwa sababu hazikupata maji.+ 7 Zingine zilianguka katikati ya miiba, na miiba yenye ilikomaa pamoja nazo ikazifinya.+ 8 Lakini zingine zilianguka kwenye udongo muzuri, na kisha kuota, zikazaa matunda mara mia moja (100) zaidi.”+ Kisha kusema mambo hayo, akasema kwa sauti kubwa: “Ule mwenye kuwa na masikio ya kusikiliza, asikilize.”+
-