Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 21:1-6
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 21 Kisha wakati fulani Daudi akafika Nobu+ kwa kuhani Ahimeleki. Ahimeleki akaanza kutetemeka wakati alikutana na Daudi, na akamuambia: “Sababu gani uko peke yako na hakuna mutu pamoja na wewe?”+ 2 Daudi akamujibu kuhani Ahimeleki: “Mufalme aliniagiza nifanye jambo fulani, lakini alisema, ‘Usimujulishe mutu yeyote kuhusu kazi yenye ninakutuma ufanye na kuhusu maagizo yenye nimekupatia.’ Nilisikilizana na vijana wangu tukutane mahali fulani. 3 Sasa kama uko na mikate tano (5), unipatie tu mikate hiyo, ao kitu chochote chenye kitapatikana.” 4 Lakini kuhani akamuambia Daudi: “Kwa sasa hakuna mikate ya kawaida, lakini kuko mikate mitakatifu+⁠—ikiwa tu vijana wako wamejiepusha* na wanamuke.”+ 5 Daudi akamujibu kuhani: “Hakika tumejiepusha na wanamuke kama vile tulifanya mbele wakati nilienda katika mapambano ya kijeshi.+ Kama miili ya vijana hawa ni mitakatifu hata wakati kazi yenye walitumwa wafanye ni ya kawaida, je, haiko mitakatifu zaidi leo?” 6 Kwa hiyo kuhani akamupatia mikate mitakatifu,+ kwa sababu hapakukuwa mikate ingine isipokuwa mikate ya wonyesho, yenye ilikuwa imeondolewa mbele ya Yehova ili mikate mipya iwekwe pa nafasi yake siku hiyo yenye iliondolewa.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine