-
Matayo 12:43-45Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
43 “Wakati roho muchafu anatoka ndani ya mutu, anapita mahali kwenye hakuna maji akitafuta mahali pa kupumuzikia, lakini hapate mahali popote.+ 44 Kisha roho huyo anasema, ‘Nitarudia kwenye nyumba yangu kwenye nilitoka,’ na wakati anafika, anakuta nyumba haijakaliwa lakini imefagiwa na iko safi, na imepambwa. 45 Kisha anaenda na kuleta roho wengine saba (7) waovu zaidi kuliko yeye, na kisha kuingia ndani, wanakaa mule; na hali ya mwisho ya mutu huyo inakuwa mubaya zaidi kuliko ya kwanza.+ Ni vile pia itakuwa kwa kizazi hiki kiovu.”
-