Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Matayo 12:38-42
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 38 Kisha ili kumujibu, waandishi fulani na Wafarisayo wakasema: “Mwalimu, tunataka kuona alama kutoka kwako.”+ 39 Akawajibu na kuwaambia: “Kizazi kiovu na chenye kufanya uzinifu* kinaendelea kutafuta alama, lakini hakitapewa alama yoyote isipokuwa alama ya nabii Yona.+ 40 Kwa maana kama vile Yona alikuwa ndani ya tumbo la ule samaki mukubwa siku tatu (3) muchana na usiku,+ ni vile Mwana wa binadamu atakuwa katika kaburi* siku tatu muchana na usiku.+ 41 Watu wa Ninawi watasimama katika hukumu pamoja na kizazi hiki na watakihukumu, kwa sababu walitubu wakati walisikia mambo yenye Yona alihubiri.+ Lakini muangalie! hapa kuko kitu kikubwa kuliko Yona.+ 42 Malkia wa kusini atasimamishwa katika hukumu pamoja na kizazi hiki, na atakihukumu, kwa maana alikuja kutoka kwenye miisho ya dunia ili kusikia hekima ya Sulemani.+ Lakini muangalie! hapa kuko kitu kikubwa kuliko Sulemani.+

  • Matayo 16:4
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 4 Kizazi kiovu na chenye kufanya uzinifu* kinaendelea kutafuta alama, lakini hakitapewa alama yoyote+ isipokuwa alama ya Yona.”+ Basi akaenda na akawaacha.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine