-
Matayo 12:38-42Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
38 Kisha ili kumujibu, waandishi fulani na Wafarisayo wakasema: “Mwalimu, tunataka kuona alama kutoka kwako.”+ 39 Akawajibu na kuwaambia: “Kizazi kiovu na chenye kufanya uzinifu* kinaendelea kutafuta alama, lakini hakitapewa alama yoyote isipokuwa alama ya nabii Yona.+ 40 Kwa maana kama vile Yona alikuwa ndani ya tumbo la ule samaki mukubwa siku tatu (3) muchana na usiku,+ ni vile Mwana wa binadamu atakuwa katika kaburi* siku tatu muchana na usiku.+ 41 Watu wa Ninawi watasimama katika hukumu pamoja na kizazi hiki na watakihukumu, kwa sababu walitubu wakati walisikia mambo yenye Yona alihubiri.+ Lakini muangalie! hapa kuko kitu kikubwa kuliko Yona.+ 42 Malkia wa kusini atasimamishwa katika hukumu pamoja na kizazi hiki, na atakihukumu, kwa maana alikuja kutoka kwenye miisho ya dunia ili kusikia hekima ya Sulemani.+ Lakini muangalie! hapa kuko kitu kikubwa kuliko Sulemani.+
-