26 Haipaswe kuwa vile katikati yenu;+ lakini kila mutu mwenye anataka kuwa mukubwa katikati yenu anapaswa kuwa mutumishi wenu,+27 na kila mutu mwenye anataka kuwa wa kwanza katikati yenu anapaswa kuwa mutumwa wenu.+
48 na akawaambia: “Kila mutu mwenye anamupokea mutoto huyu mudogo kwa sababu ya jina langu ananipokea mimi pia; na kila mutu mwenye ananipokea, anamupokea pia Ule mwenye alinituma.+ Kwa maana mwenye anajiendesha kama mudogo zaidi katikati yenu ninyi wote ndiye mukubwa.”+
26 Hata hivyo, ninyi hamupaswe kuwa vile.+ Lakini ule mwenye iko* mukubwa zaidi kati yenu akuwe kama mudogo zaidi,+ na ule mwenye anaongoza akuwe kama mutu wa kuwatumikia.
5 Katika njia ileile, ninyi vijana, mujitiishe kwa wanaume wazee.*+ Lakini ninyi wote muvae* unyenyekevu* wamoja kuelekea wengine, kwa sababu Mungu anawapinga wenye majivuno, lakini anawapatia wanyenyekevu fazili zenye hazistahiliwe.+