-
Ezekieli 1:5-10Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
-
-
5 Katikati yake kulikuwa kitu chenye kilifanana na viumbe ine (4) vyenye uzima,+ na kila kimoja kilionekana kama mwanadamu. 6 Kila kimoja cha viumbe hivyo kilikuwa na nyuso ine (4) na mabawa ine.+ 7 Miguu ya viumbe hivyo ilikuwa imenyooka, na vikanyangio vya miguu ya viumbe hivyo vilikuwa kama vikanyangio vya kitoto-dume cha ngombe, na vilikuwa vinangaa kama vile kungaa kwa shaba yenye kungarishwa.+ 8 Vilikuwa na mikono ya mwanadamu chini ya mabawa yavyo pande zote ine (4), na vyote ine vilikuwa na nyuso na mabawa. 9 Mabawa ya viumbe hivyo yalikuwa yanagusana. Havikukuwa vinageuka wakati vilikuwa vinaenda; kila kimoja cha viumbe hivyo kilikuwa kinaenda mbele moja kwa moja.+
10 Nyuso za viumbe hivyo zilionekana hivi: Kila kimoja cha viumbe hivyo ine (4) kilikuwa na uso wa mwanadamu na uso wa simba+ upande wa kuume, uso wa ngombe-dume+ upande wa kushoto, na kila kimoja cha viumbe hivyo ine kilikuwa na uso wa tai.+
-