Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 27
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Kumbukumbu la Torati

      • Sheria itaandikwa kwenye majiwe (1-10)

      • Kwenye Mulima Ebali na Mulima Gerizimu (11-14)

      • Laana zinatangazwa (15-26)

Kumbukumbu la Torati 27:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kuyapakaa chokaa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yosh. 8:30-32

Kumbukumbu la Torati 27:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 13:26, 27

Kumbukumbu la Torati 27:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “utayapakaa chokaa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 11:29

Kumbukumbu la Torati 27:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 20:25

Kumbukumbu la Torati 27:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 3:1
  • +Law. 7:15
  • +Kum 12:7

Kumbukumbu la Torati 27:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 24:12

Kumbukumbu la Torati 27:9

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 19:5; Kum 26:18

Kumbukumbu la Torati 27:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 2:3; Mt 19:17; 1 Yo. 5:3

Kumbukumbu la Torati 27:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 11:29

Kumbukumbu la Torati 27:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yosh. 8:33

Kumbukumbu la Torati 27:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 33:10

Kumbukumbu la Torati 27:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “sanamu ya kuyeyushwa.”

  • *

    Ao “fundi wa mbao na metali.”

  • *

    Ao “Ikuwe vile!”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 20:4; Kum 4:15, 16; Isa 44:9
  • +Kut 34:17; Law. 19:4
  • +Kum 7:25; 29:17

Kumbukumbu la Torati 27:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 20:12; Kum 21:18-21; Mez. 20:20; 30:17; Mt 15:4

Kumbukumbu la Torati 27:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 19:14; Mez. 23:10

Kumbukumbu la Torati 27:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 19:14

Kumbukumbu la Torati 27:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “yatima.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 16:20; Mez. 17:23; Mik 3:11
  • +Kut 22:21, 22; Kum 10:17, 18; Mal 3:5; Yak 1:27

Kumbukumbu la Torati 27:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “amefunua upindo wa nguo ya baba yake.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 18:8; 1 Kor. 5:1

Kumbukumbu la Torati 27:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 22:19; Law. 18:23; 20:15

Kumbukumbu la Torati 27:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 18:9; 20:17

Kumbukumbu la Torati 27:23

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 18:17; 20:14

Kumbukumbu la Torati 27:24

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 20:13; 21:12; Hes 35:31

Kumbukumbu la Torati 27:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kata-midomo.”

  • *

    Ao “amupige na kumuua.”

  • *

    Ao “nafsi ya damu yenye haina hatia.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mt 27:3, 4

Kumbukumbu la Torati 27:26

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 28:15; Gal 3:10

Maandiko ingine

Kum. 27:2Yosh. 8:30-32
Kum. 27:3Hes 13:26, 27
Kum. 27:4Kum 11:29
Kum. 27:5Kut 20:25
Kum. 27:7Law. 3:1
Kum. 27:7Law. 7:15
Kum. 27:7Kum 12:7
Kum. 27:8Kut 24:12
Kum. 27:9Kut 19:5; Kum 26:18
Kum. 27:101 Fal. 2:3; Mt 19:17; 1 Yo. 5:3
Kum. 27:12Kum 11:29
Kum. 27:13Yosh. 8:33
Kum. 27:14Kum 33:10
Kum. 27:15Kut 20:4; Kum 4:15, 16; Isa 44:9
Kum. 27:15Kut 34:17; Law. 19:4
Kum. 27:15Kum 7:25; 29:17
Kum. 27:16Kut 20:12; Kum 21:18-21; Mez. 20:20; 30:17; Mt 15:4
Kum. 27:17Kum 19:14; Mez. 23:10
Kum. 27:18Law. 19:14
Kum. 27:19Kum 16:20; Mez. 17:23; Mik 3:11
Kum. 27:19Kut 22:21, 22; Kum 10:17, 18; Mal 3:5; Yak 1:27
Kum. 27:20Law. 18:8; 1 Kor. 5:1
Kum. 27:21Kut 22:19; Law. 18:23; 20:15
Kum. 27:22Law. 18:9; 20:17
Kum. 27:23Law. 18:17; 20:14
Kum. 27:24Kut 20:13; 21:12; Hes 35:31
Kum. 27:25Mt 27:3, 4
Kum. 27:26Kum 28:15; Gal 3:10
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Kumbukumbu la Torati 27:1-26

Kumbukumbu la Torati

27 Kisha Musa pamoja na wazee wa Israeli wakaamuru watu, na kusema: “Mushike kila amri yenye ninawapatia leo. 2 Na siku mutavuka Yordani kuingia katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia, utasimamisha majiwe makubwa na kuyapiga lipu.*+ 3 Kisha uandike juu yake maneno yote ya Sheria hii wakati utakuwa umevuka, ili uingie katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia, inchi yenye kutiririka maziwa na asali, kama vile Yehova, Mungu wa mababu zako, amekuahidi.+ 4 Wakati mutakuwa mumevuka Yordani, mutasimamisha majiwe hayo kwenye Mulima Ebali+ na utayapiga lipu,* kama vile ninawaamuru leo. 5 Pia utamujengea Yehova Mungu wako mazabahu kule, mazabahu ya majiwe. Usitumie vyombo vya chuma juu ya majiwe hayo.+ 6 Utajenga mazabahu ya Yehova Mungu wako kwa majiwe mazima na kumutolea Yehova Mungu wako matoleo ya kuteketezwa juu yake. 7 Utatoa zabihu za ushirika+ na kuzikula mahali pale,+ na utashangilia mbele ya Yehova Mungu wako.+ 8 Na utaandika waziwazi maneno yote ya Sheria hii juu ya majiwe hayo.”+

9 Kisha Musa na makuhani Walawi wakasema na Israeli wote, na kuwaambia: “Nyamaza na usikilize, Ee Israeli. Leo hii umekuwa kikundi cha watu wa Yehova Mungu wako.+ 10 Unapaswa kusikiliza sauti ya Yehova Mungu wako na kushika amri zake+ na masharti yake, yenye ninakuamuru leo.”

11 Siku hiyo Musa akaamuru watu, na kusema: 12 “Makabila haya yatasimama kwenye Mulima Gerizimu+ ili kubariki watu wakati mutakuwa mumevuka Yordani: Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Yosefu, na Benyamini. 13 Na makabila haya yatasimama kwenye Mulima Ebali+ ili kutangaza laana: Rubeni, Gadi, Asheri, Zabuloni, Dani, na Naftali. 14 Na Walawi watamujibu kila mutu wa Israeli kwa sauti kubwa:+

15 “‘Alaaniwe mutu mwenye anatengeneza sanamu ya kuchongwa+ ao sanamu ya metali,*+ kitu chenye kuwa chukizo kwa Yehova,+ chenye kilitengenezwa na mikono ya fundi,* na mwenye amekificha.’ (Na watu wote watajibu, na kusema, ‘Amina!’*)

16 “‘Alaaniwe mutu mwenye anamutendea baba yake ao mama yake kwa zarau.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)

17 “‘Alaaniwe mutu mwenye anahamisha alama ya mupaka wa jirani yake.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)

18 “‘Alaaniwe mutu mwenye anamufanya kipofu apotee njia.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)

19 “‘Alaaniwe mutu mwenye anapotosha hukumu+ ya mukaaji mugeni, ya mutoto mwenye hana baba,* ao ya mujane.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)

20 “‘Alaaniwe mutu mwenye analala na bibi ya baba yake, kwa sababu amemuletea baba yake haya.’*+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)

21 “‘Alaaniwe mutu mwenye analala na munyama yeyote.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)

22 “‘Alaaniwe mutu mwenye analala na dada yake, binti ya baba yake ao binti ya mama yake.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)

23 “‘Alaaniwe mutu mwenye analala na mama-mukwe wake.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)

24 “‘Alaaniwe mutu mwenye anavizia na kuua jirani yake.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)

25 “‘Alaaniwe mutu mwenye anakubali rushwa* ili amuue* mutu mwenye hana kosa.’*+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)

26 “‘Alaaniwe mutu mwenye hataunga mukono maneno haya ya Sheria hii kwa kuyatenda.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine