Mwanzo
25 Kisha Abrahamu akachukua tena bibi, na jina lake lilikuwa Ketura. 2 Kisha wakati fulani Ketura akamuzalia Zimrani, Yokshani, Medani, Midiani,+ Ishbaki, na Shua.+
3 Yokshani akazaa Sheba na Dedani.
Wana wa Dedani walikuwa Ashurimu, Letushimu, na Leumimu.
4 Wana wa Midiani walikuwa Efa, Eferi, Hanoki, Abida, na Eldaa.
Hao wote walikuwa wana wa Ketura.
5 Kisha wakati fulani Abrahamu akamupatia Isaka kila kitu chenye alikuwa nacho,+ 6 lakini Abrahamu akapatia wana wa masuria* wake zawadi. Kisha, wakati alikuwa angali muzima, aliwaambia waende upande wa mashariki, mbali na Isaka mwana wake,+ katika inchi ya Mashariki. 7 Miaka ya maisha ya Abrahamu ilikuwa miaka mia moja makumi saba na tano (175). 8 Kisha Abrahamu akavuta pumuzi yake ya mwisho na akakufa katika uzee muzuri; alikuwa muzee na mwenye kutosheka, naye akakusanywa kwa watu wake.* 9 Wana wake Isaka na Ishmaeli wakamuzika katika pango la Makpela katika shamba la Efroni mwana wa Zohari Muhiti lenye kuwa mbele ya Mamre,+ 10 shamba lenye Abrahamu alinunua kwa wana wa Heti. Ni kule Abrahamu na Sara bibi yake walizikwa.+ 11 Kisha Abrahamu kufa, Mungu aliendelea kumubariki Isaka mwana wake;+ na Isaka alikuwa anaishi karibu na Beer-lahai-roi.+
12 Hii ndiyo historia ya Ishmaeli+ mwana wa Abrahamu mwenye Hagari+ Mumisri, mutumishi wa Sara, alimuzalia Abrahamu.
13 Sasa haya ndiyo majina ya wana wa Ishmaeli, kufuatana na majina yao kulingana na asili za familia zao: Muzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli alikuwa Nebayoti,+ kisha Kedari,+ Adbeeli, Mibsamu,+ 14 Mishma, Duma, Masa, 15 Hadadi, Tema, Yeturi, Nafishi, na Kedema. 16 Hao ndio wana wa Ishmaeli, na hayo ndiyo majina yao kulingana na makao yao na kambi zao,* wakubwa kumi na mbili (12) kulingana na ukoo wao mbalimbali.+ 17 Na Ishmaeli akaishi miaka mia moja makumi tatu na saba (137). Kisha akavuta pumuzi yake ya mwisho na akakufa, naye akakusanywa kwa watu wake.* 18 Nao wakaanza kuishi kuanzia Havila+ karibu na Shuri,+ yenye iko karibu na Misri, mupaka kufikia Ashuru. Alikaa karibu na ndugu zake wote.*+
19 Hii ndiyo historia ya Isaka mwana wa Abrahamu.+
Abrahamu alimuzaa Isaka. 20 Isaka alikuwa na miaka makumi ine (40) wakati alimuoa Rebeka, binti ya Betueli+ Mwaramu wa Padan-aramu, dada ya Labani ule Mwaramu. 21 Na Isaka akaendelea kumulilia Yehova kwa ajili ya bibi yake, kwa sababu alikuwa tasa; kwa hiyo Yehova akasikia ombi lake, na Rebeka bibi yake akakuwa na mimba. 22 Na wana wenye walikuwa ndani ya tumbo lake wakaanza kupigana,+ kwa hiyo akasema: “Kama ni hivi, sababu gani niendelee kuishi?” Basi akamuuliza Yehova. 23 Na Yehova akamuambia: “Mataifa mbili yako katika tumbo lako la uzazi,+ na vikundi mbili vya watu vitatenganishwa kutoka ndani yako;+ na taifa moja litakuwa na nguvu kuliko taifa lingine,+ na mukubwa atamutumikia mudogo.”+
24 Wakati muda wa kuzaa ulifika, angalia! mapacha walikuwa katika tumbo lake la uzazi. 25 Kisha wakati wa kwanza alitoka, mwili wake wote ulikuwa mwekundu, na ulikuwa kama nguo ya manyoya,+ basi wakamupatia jina Esau.*+ 26 Kisha ndugu yake akatoka na mukono wake ulikuwa unashika kisigino cha Esau,+ kwa hiyo Isaka akamupatia jina Yakobo.*+ Isaka alikuwa na miaka makumi sita (60) wakati Rebeka aliwazaa.
27 Kadiri wale watoto wanaume waliendelea kukomaa, Esau akakuwa fundi wa kuwinda,+ mutu wa pori, lakini Yakobo akakuwa mutu mwenye hana lawama, mwenye kukaa katika mahema.+ 28 Na Isaka alimupenda Esau kwa sababu hiyo ilimaanisha nyama ya kuwinda katika kinywa chake, lakini Rebeka alimupenda Yakobo.+ 29 Siku moja Yakobo alikuwa anatokotesha muchuzi wakati Esau alirudia kutoka katika pori akiwa amechoka. 30 Kwa hiyo Esau akamuambia Yakobo: “Haraka, tafazali, unipatie sehemu fulani ya muchuzi mwekundu* wenye uko nao pale,* kwa maana nimechoka sana!”* Ndiyo sababu jina lake lilikuwa Edomu.*+ 31 Yakobo akamuambia: “Kwanza unipatie ninunue haki yako ya muzaliwa wa kwanza!”+ 32 Na Esau akasema: “Angalia, niko karibu kufa! Haki ya kuzaliwa itanifanyia nini?” 33 Yakobo akamuambia: “Uniapie kwanza!” Basi akamuapia na kumuuzisha Yakobo haki yake ya muzaliwa wa kwanza.+ 34 Kisha Yakobo akamupatia Esau mukate na muchuzi wa dengu, naye akakula na kunywa, kisha akasimama na kuenda. Hivyo Esau akazarau haki yake ya kuzaliwa.