Kumbukumbu la Torati
26 “Wakati mwishowe utaingia katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia kuwa uriti na wakati utakuwa umeiriti na kuishi ndani yake, 2 utakamata sehemu fulani ya matunda ya kwanza ya mazao* yote ya udongo, yenye utakusanya katika inchi yako yenye Yehova Mungu wako anakupatia, na utayatia katika kitunga na kuenda mahali kwenye Yehova Mungu wako atachagua jina lake likae.+ 3 Utaenda kwa kuhani mwenye atakuwa anatumikia wakati huo na kumuambia, ‘Leo ninamujulisha Yehova Mungu wako kwamba nimeingia katika inchi yenye Yehova aliapia mababu zetu kwamba atatupatia sisi.’+
4 “Kisha kuhani atakamata kitunga hicho katika mukono wako na kukiweka mbele ya mazabahu ya Yehova Mungu wako. 5 Kisha utatangaza hivi mbele ya Yehova Mungu wako: ‘Baba yangu alikuwa Mwaramu mwenye alikuwa anatanga-tanga,*+ na akashuka kuenda Misri+ na kukaa kule akiwa mugeni, pamoja na watu kidogo katika nyumba yake.+ Lakini kule akakuwa taifa kubwa, lenye nguvu na lenye watu wengi.+ 6 Na Wamisri wakatutendea mubaya na kutukandamiza na kuweka utumwa mukali juu yetu.+ 7 Kwa hiyo tukaanza kumulilia Yehova, Mungu wa mababu zetu, na Yehova akasikia sauti yetu na kuangalia mateso yetu na taabu yetu na kukandamizwa kwetu.+ 8 Mwishowe Yehova akatutosha Misri kwa mukono wenye nguvu na mukono wenye kunyooshwa+ na kwa matendo yenye kuogopesha sana na kwa alama na miujiza.+ 9 Kisha akatuleta mahali hapa na kutupatia inchi hii, inchi yenye kutiririka maziwa na asali.+ 10 Sasa nimeleta matunda ya kwanza ya mazao ya udongo wenye Yehova amenipatia.’+
“Unapaswa kutia kitunga hicho chini mbele ya Yehova Mungu wako na kuinama mbele ya Yehova Mungu wako. 11 Kisha utashangilia kwa sababu ya mambo yote ya muzuri yenye Yehova Mungu wako amekupatia wewe na nyumba yako, wewe na Mulawi na mukaaji mugeni mwenye kuwa kati yako.+
12 “Wakati utamaliza kutoa+ sehemu moja yote ya kumi (1/10) ya mazao yako katika mwaka wa tatu (3), mwaka wa sehemu moja ya kumi, utapatia sehemu hiyo Mulawi, mukaaji mugeni, mutoto mwenye hana baba,* na mujane, nao watakula na kushiba katika miji yako.*+ 13 Kisha utasema mbele ya Yehova Mungu wako, ‘Nimeondoa sehemu takatifu katika nyumba yangu na kuipatia Mulawi, mukaaji mugeni, mutoto mwenye hana baba, na mujane,+ kama vile umeniamuru. Sijavunja wala kuzarau amri zako. 14 Sikuikula wakati nilikuwa ninaomboleza wala kuondoa sehemu yake yoyote wakati nilikuwa muchafu ao kutoa sehemu yake yoyote kwa ajili ya wafu. Nimetii sauti ya Yehova Mungu wangu na kufanya mambo yote yenye uliniamuru. 15 Sasa angalia chini ukiwa katika makao yako matakatifu, mbinguni, na ubariki watu wako Israeli na inchi yenye umetupatia,+ kama vile uliapia mababu zetu,+ inchi yenye kutiririka maziwa na asali.’+
16 “Leo Yehova Mungu wako anakuamuru utende masharti haya na maamuzi haya ya hukumu. Unapaswa kuyashika na kuyatenda kwa moyo wako wote+ na nafsi* yako yote. 17 Leo Yehova amekutangazia kwamba atakuwa Mungu wako wakati unatembea katika njia zake na kushika masharti yake,+ amri zake,+ na maamuzi yake ya hukumu,+ na wakati unasikiliza sauti yake. 18 Na leo umemutangazia Yehova kwamba utakuwa kikundi chake cha watu, mali yake ya pekee,*+ kama vile amekuahidi, na kwamba utashika amri zake zote 19 na kwamba atakuweka juu ya mataifa mengine yote yenye amefanya,+ na hivyo kukupatia sifa na kujulikana sana na utukufu wakati unajionyesha kuwa kikundi cha watu watakatifu kwa ajili ya Yehova Mungu wako,+ kama vile amekuahidi.”