Esta
8 Siku hiyo Mufalme Ahasuero akamupatia Malkia Esta nyumba ya Hamani,+ adui ya Wayahudi;+ na Mordekai akaingia mbele ya mufalme, kwa maana Esta alikuwa amemuambia kwamba Mordekai ni mutu wa jamaa yake.+ 2 Kisha mufalme akatosha pete yake ya kutia muhuri+ yenye alikuwa amemunyanganya Hamani na akaipatia Mordekai. Na Esta akamupatia Mordekai mamlaka juu ya nyumba ya Hamani.+
3 Zaidi ya hayo, Esta akazungumuza tena na mufalme. Akaanguka kwenye miguu yake, akalia na kumuomba mufalme aondoe ubaya wenye Hamani Mwagagi alifanya na mupango wake wa kuua Wayahudi.+ 4 Mufalme akamunyooshea Esta fimbo ya ufalme ya zahabu,+ basi Esta akainuka na kusimama mbele ya mufalme. 5 Akasema: “Kama inamupendeza mufalme na kama amenikubali, na kama mufalme anaona kuwa ni muzuri na kama niko mwenye kupendeza mbele ya macho yake, agizo liandikwe la kufuta yale maandishi ya huyo mufanya-mipango-mibaya Hamani+ mwana wa Hamedata Mwagagi,+ yenye aliandika ili kuwaharibu Wayahudi katika majimbo yote ya* mufalme. 6 Kwa maana namna gani ninaweza kuvumilia kuona watu wangu wakipatwa na musiba, na namna gani ninaweza kuvumilia kuangalia watu wa jamaa yangu wakiharibiwa?”
7 Kwa hiyo Mufalme Ahasuero akamuambia Malkia Esta na Mordekai ule Muyahudi: “Angalia! Nimemupatia Esta nyumba ya Hamani+ na nimeagiza atundikwe kwenye muti,+ kwa sababu ya mupango wake wa kushambulia* Wayahudi. 8 Munaweza sasa kuandika katika jina la mufalme jambo lolote lenye munaona linafaa kwa ajili ya Wayahudi, na mulitie muhuri kwa pete ya mufalme; kwa maana amri yenye kuandikwa katika jina la mufalme na yenye kutiwa muhuri kwa pete ya mufalme haiwezi kufutwa.”+
9 Kwa hiyo waandishi wa mufalme wakaitwa katika mwezi wa tatu (3), ni kusema, mwezi wa Sivani,* siku ya makumi mbili na tatu (23) ya mwezi huo, na wakaandika mambo yote yenye Mordekai aliamuru Wayahudi, maliwali,+ magavana, na wakubwa wa majimbo*+ kuanzia India mupaka Etiopia, majimbo* mia moja makumi mbili na saba (127), kila jimbo* kwa mwandiko wake mwenyewe* na kila kikundi cha watu kwa luga yao wenyewe na kwa Wayahudi katika mwandiko wao wenyewe* na luga yao.
10 Akaandika amri hiyo katika jina la Mufalme Ahasuero na kuitia muhuri kwa pete ya mufalme+ na akatuma maandishi hayo kupitia mukono wa wajumbe wenye kupanda farasi; walipanda farasi wa kusafirisha barua wenye kukimbia mbio sana, wenye walifugwa kwa ajili ya utumishi wa kifalme. 11 Katika maandishi hayo mufalme alipatia Wayahudi ruhusa katika miji yote mbalimbali ili wajikusanye pamoja na kupigania uzima wao* na kuangamiza, kuua, na kuharibu majeshi yoyote ya watu ao jimbo, yenye yangeweza* kuwashambulia, kutia ndani wanamuke na watoto, na wanyanganye mali zao.+ 12 Jambo hilo lilipaswa kufanywa siku ileile katika majimbo yote ya* Mufalme Ahasuero, siku ya kumi na tatu (13) ya mwezi wa kumi na mbili (12), ni kusema, mwezi wa Adari.*+ 13 Kopi ya maandishi hayo ilipaswa kutolewa kuwa sheria katika majimbo yote.* Ilipaswa kutangaziwa vikundi vyote vya watu, ili Wayahudi wakuwe tayari siku hiyo kulipiza kisasi juu ya maadui wao.+ 14 Wajumbe wenye kupanda farasi wa kusafirisha barua wenye kukimbia mbio sana ambao walitumiwa katika utumishi wa kifalme wakaondoka haraka kwa agizo la mufalme. Sheria hiyo ilitolewa pia katika ngome* ya Shushani.*+
15 Sasa Mordekai akatoka mbele ya mufalme akiwa mwenye kuvaa nguo ya kifalme ya rangi ya bluu na rangi nyeupe, taji kubwa la zahabu na nguo ya inje ya kitambaa kizuri cha manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau.+ Muji wa Shushani* ukajaa shangwe na vigelegele. 16 Kwa Wayahudi kulikuwa kitulizo* na shangwe na furaha na heshima. 17 Na katika majimbo yote* na miji yote, kwenye amri ya mufalme na sheria yake ilifika, Wayahudi walifurahi na kushangilia, walifanya karamu na sherehe. Wengi kati ya watu wa inchi walikuwa wanajitangaza kuwa Wayahudi,+ kwa maana woga wa Wayahudi ulikuwa umeanguka juu yao.