Zaburi
2 Ndiyo sababu hatutaogopa, hata kama dunia inabadilika,
Hata kama milima inaanguka katika sehemu za chini kabisa za bahari,+
3 Hata kama maji yake yananguruma na kutosha pofu nyingi,+
Hata kama milima inatikiswa kwa sababu ya musukosuko wake. (Sela)
4 Kuko muto wenye mito yake midogo inafanya muji wa Mungu ushangilie,+
Tabenakulo takatifu na kubwa ya Mwenye Kuwa Juu Zaidi.
5 Mungu iko* katika muji huo;+ hauwezi kupinduliwa.
Mungu atausaidia wakati kunapambazuka.*+
6 Mataifa yalikuwa katika musukosuko, falme zilipinduliwa;
Alipandisha sauti yake, na dunia ikayeyuka.+
8 Mukuje na mujionee matendo ya Yehova,
Namna amefanya mambo yenye kushangaza katika dunia.
9 Anamaliza vita katika dunia yote.+
Anavunja upinde na kuvunja mukuki vipande-vipande;
Anateketeza kwa moto magari ya kukokotwa ya vita.*
10 “Muache na mujue kwamba mimi ni Mungu.