Isaya
61 Roho ya Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova iko juu yangu,+
Kwa sababu Yehova alinitia mafuta ili nitangazie wapole habari njema.+
Alinituma ili nifunge vidonda vya wenye kuvunjika moyo,
Ili nitangaze uhuru kwa wale wenye walikamatwa mateka
Na kufunguliwa kabisa kwa macho ya wafungwa,+
2 Ili kutangaza mwaka wa nia njema ya* Yehova
Na siku ya kisasi ya Mungu wetu,+
Ili kufariji wote wenye kuomboleza,+
3 Ili kutimiza mahitaji ya wale wenye kuombolezea Sayuni,
Ili kuwapatia nguo ya kichwa pa nafasi ya majivu,
Mafuta ya furaha pa nafasi ya maombolezo,
Nguo ya sifa pa nafasi ya roho yenye kuvunjika.
4 Watajenga upya mabomoko ya zamani;
Watasimamisha nafasi za zamani zenye ziliachwa ukiwa,+
Na watajenga upya miji yenye iliharibiwa,+
Nafasi zenye ziliachwa ukiwa kizazi kwa kizazi.+
5 “Wageni watasimama na kuchunga makundi yenu,
Na watu wa inchi zingine+ watakuwa walimaji wenu na watunza-mizabibu wenu.+
7 Kuliko kupata haya mutakuwa na fungu mara mbili,
Na kuliko kufezeheka watapiga vigelegele vya shangwe kwa sababu ya fungu lao.
Ndiyo, watakuwa na fungu mara mbili katika inchi yao.+
Watakuwa na shangwe milele.+
Nitawapatia mushahara wao kwa uaminifu,
Na nitafanya agano la milele pamoja nao.+
10 Nitashangilia sana katika Yehova.
Nafsi yangu yote itashangilia katika Mungu wangu.+