Hesabu
22 Kisha Waisraeli wakaondoka na kupiga kambi kwenye maeneo tambarare ya jangwa la Moabu ngambo ya Yordani kutoka Yeriko.+ 2 Sasa Balaki+ mwana wa Sipori aliona mambo yote yenye Israeli alikuwa ametendea Waamori, 3 na Moabu akaogopa sana watu hao, kwa sababu walikuwa wengi sana; kwa kweli, Moabu akaogopa na kuchukizwa sana kwa sababu ya Waisraeli.+ 4 Kwa hiyo Moabu akaambia wazee wa Midiani:+ “Sasa kutaniko hili litameza maeneo yetu yote yenye kutuzunguka, kama vile ngombe-dume anamezaka majani katika pori.”
Balaki mwana wa Sipori alikuwa mufalme wa Moabu wakati huo. 5 Alituma wajumbe kwa Balaamu mwana wa Beori kule Petori,+ karibu na ule Muto* katika inchi yenye alizaliwa ndani. Alimuita, na kumuambia: “Angalia! Watu fulani wametoka Misri. Angalia! Wamefunika uso wa* dunia,*+ na wanakaa hapa tu mbele yangu. 6 Basi, tafazali, kuja na ulaani watu hawa kwa ajili yangu,+ kwa maana wako na nguvu kuliko mimi. Pengine ninaweza kuwashinda na kuwafukuza katika inchi, kwa maana ninajua muzuri kama ule mwenye unabariki amebarikiwa na ule mwenye unalaani amelaaniwa.”
7 Kwa hiyo wazee wa Moabu na wazee wa Midiani wakasafiri na malipo ya uaguzi katika mikono yao na kuenda kwa Balaamu+ na wakamuambia maneno ya Balaki. 8 Halafu akawaambia: “Mulale hapa, na nitawaletea neno lolote lenye Yehova ataniambia.” Kwa hiyo wakubwa wa Moabu wakabakia kwa Balaamu.
9 Kisha Mungu akamutokea Balaamu na kusema:+ “Wanaume hawa wenye wako pamoja na wewe ni nani?” 10 Balaamu akamuambia Mungu wa kweli: “Balaki mwana wa Sipori, mufalme wa Moabu, amenitumia ujumbe, na kusema, 11 ‘Angalia! Watu wenye wanatoka Misri wanafunika uso wa* dunia.* Sasa kuja na uwalaani kwa ajili yangu.+ Pengine ninaweza kupigana nao na kuwafukuza.’” 12 Lakini Mungu akamuambia Balaamu: “Usiende pamoja nao. Usilaani watu hao, kwa maana wamebarikiwa.”+
13 Balaamu akaamuka asubui na kuambia wakubwa wa Balaki: “Muende katika inchi yenu, kwa maana Yehova amekataa kuniruhusu niende pamoja na ninyi.” 14 Kwa hiyo wakubwa wa Moabu wakaondoka na wakarudia kwa Balaki na kumuambia: “Balaamu amekataa kuja pamoja na sisi.”
15 Lakini, Balaki akatuma tena wakubwa, wengi zaidi na wenye kuheshimika zaidi kuliko wale wa kikundi cha kwanza. 16 Wakafika kwa Balaamu na kumuambia: “Balaki mwana wa Sipori amesema, ‘Tafazali, usiruhusu kitu chochote kikuzuie kuja kwangu, 17 kwa maana nitakuonyesha heshima kubwa na nitafanya kila kitu chenye utaniambia nifanye. Kwa hiyo, kuja, tafazali, na ulaani watu hawa kwa ajili yangu.’” 18 Lakini Balaamu akajibu watumishi wa Balaki: “Hata kama Balaki ananipatia nyumba yake mwenyewe yenye kujaa feza na zahabu, siwezi kufanya jambo lolote lenye linavunja agizo la Yehova Mungu wangu, ikuwe jambo la kidogo ao la mukubwa.+ 19 Lakini tafazali, mubakie hapa usiku wa leo pia, ili nijue Yehova ataniambia jambo gani lingine.”+
20 Kisha Mungu akamutokea Balaamu usiku na kumuambia: “Kama wanaume hao wamekuja kukuita, uende pamoja nao. Lakini utasema tu maneno yenye nitakuambia useme.”+ 21 Basi Balaamu akaamuka asubui na akamutandika punda* wake na kuenda pamoja na wakubwa wa Moabu.+
22 Lakini kasirani ya Mungu ikawaka sana kwa sababu Balaamu alikuwa anaenda, na malaika wa Yehova akasimama katika njia ili kumupinga. Sasa Balaamu alikuwa amepanda juu ya punda wake, na watumishi wake wawili walikuwa pamoja naye. 23 Na wakati punda huyo aliona malaika wa Yehova amesimama katika njia akiwa na upanga wenye kuchomolewa katika mukono wake, alijaribu kutoka katika njia ili aingie katika eneo la mashamba. Lakini Balaamu akaanza kumupiga punda huyo ili arudie katika njia. 24 Kisha malaika wa Yehova akasimama katika njia nyembamba katikati ya mashamba mbili ya mizabibu, na kulikuwa ukuta wa majiwe kwenye pande zote mbili. 25 Wakati punda aliona malaika wa Yehova, akaanza kujisukuma kwenye ukuta na kufinya muguu wa Balaamu kwenye ukuta, na Balaamu akaanza kumupiga tena.
26 Sasa malaika wa Yehova akapita tena na kusimama mahali pembamba kwenye hakukuwa nafasi ya kugeukia upande wa kuume ao kushoto. 27 Wakati punda aliona malaika wa Yehova, akalala chini, chini ya Balaamu, kwa hiyo Balaamu akakasirika sana na kuendelea kumupiga punda kwa fimbo yake. 28 Mwishowe Yehova akamufanya punda huyo aseme,*+ na akamuambia Balaamu: “Nimekutendea nini yenye inafanya unipige mara hizi tatu (3)?”+ 29 Balaamu akamujibu punda huyo: “Ni kwa sababu umenifanya nionekane kuwa mupumbavu. Kama tu ningekuwa na upanga katika mukono wangu, ningekuua!” 30 Kisha punda akamuambia Balaamu: “Je, mimi siko punda wako mwenye umepanda maisha yako yote mupaka leo? Je, kuko siku nimekutendea hivi zamani?” Akajibu: “Hapana!” 31 Kisha Yehova akafungua macho ya Balaamu,+ naye akaona malaika wa Yehova amesimama katika njia akiwa na upanga wenye kuchomolewa katika mukono wake. Mara moja Balaamu akainama na kushusha uso chini.
32 Kisha malaika wa Yehova akamuambia: “Sababu gani umemupiga punda wako mara hizi tatu (3)? Angalia! Mimi mwenyewe nimekuja ili kukupinga, kwa sababu njia yako haipatane na mapenzi yangu.+ 33 Punda aliniona na akajaribu kunikwepa mara hizi tatu (3).+ Kama hangenikwepa! Kufikia sasa ningekuwa nimekuua na kumuacha punda akiwa muzima.” 34 Balaamu akamuambia malaika wa Yehova: “Nimetenda zambi, kwa sababu sikujua kama ni wewe ulisimama katika njia ili kukutana na mimi. Na sasa kama jambo hilo ni la mubaya mbele ya macho yako, mimi nitarudia.” 35 Lakini malaika wa Yehova akamuambia Balaamu: “Uende pamoja na wanaume hao, lakini utasema tu maneno yenye nitakuambia.” Kwa hiyo Balaamu akaendelea kuenda pamoja na wakubwa wa Balaki.
36 Wakati Balaki alisikia kama Balaamu amefika, akaenda inje mara moja ili kumupokea katika muji wa Moabu, wenye kuwa pembeni ya Arnoni kwenye mupaka wa Moabu. 37 Balaki akamuambia Balaamu: “Je, sikutuma wakuite? Sababu gani haukukuja kwangu? Je, uliwaza siwezi kukuonyesha heshima kubwa?”+ 38 Balaamu akamujibu Balaki: “Sasa nimekuja kwako. Lakini, je, nitaruhusiwa kusema jambo fulani? Ninaweza kusema tu maneno yenye Mungu anatia katika kinywa changu.”+
39 Kwa hiyo Balaamu akaenda pamoja na Balaki, na wakafika Kiriat-husoti. 40 Balaki akatoa zabihu za ngombe na kondoo na akatuma sehemu kwa Balaamu na kwa wakubwa wenye walikuwa pamoja naye. 41 Asubui Balaki akamuchukua Balaamu na kumupandisha mupaka Bamot-baali; na kule aliweza kuona watu hao wote.+