Zaburi
Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki. Wimbo.
68 Mungu asimame, maadui wake wasambazwe,
Na wale wenye kumuchukia wakimbie kutoka mbele yake.+
2 Uwapeperushe mbali kama vile moshi unapeperushwa mbali;
Kama vile nta* inayeyuka mbele ya moto,
Waovu waangamie kwa njia hiyo kutoka mbele ya Mungu.+
4 Mumuimbie Mungu; muimbie jina lake sifa.*+
Mumuimbie Ule mwenye kupanda kupitia maeneo tambarare ya jangwa.*
Jina lake ni Yah!*+ Mushangilie mbele yake!
Lakini watu wenye wako kichwa-nguvu* lazima waishi katika inchi yenye kukauka.+
8 Dunia ilitetemeka;+
Mbingu ilimwanga* mvua kwa sababu ya Mungu;
Huu Mulima Sinai ulitetemeka kwa sababu ya Mungu, Mungu wa Israeli.+
9 Ulifanya mvua inyeshe kwa wingi, Ee Mungu;
Ulitia nguvu tena watu* wako wenye kuchoka.
10 Walikaa katika kambi yako yenye mahema;+
Kwa wema wako, uliandalia maskini, Ee Mungu.
12 Wafalme wa majeshi wanakimbia,+ wanakimbia!
Mwanamuke mwenye anabakia kwenye nyumba anapewa sehemu yake ya vitu vyenye vilichukuliwa katika vita.+
13 Hata kama ninyi wanaume mulikuwa munalala kati ya mioto ya kambi,*
Kutakuwa mabawa ya njiwa yenye kufunikwa kwa feza,
Yenye manyoya ya zahabu safi.*
16 Sababu gani munaangalia kwa wivu, ninyi milima yenye vichwa,
Kwa kweli, Yehova atakaa kule milele.+
17 Magari ya Mungu ya vita ni makumi ya maelfu, maelfu kwa maelfu.+
Yehova ametoka Sinai na kuingia mahali patakatifu.+
Ulichukua watu wenye walikamatwa mateka;
Ulikamata zawadi katika umbo ya wanadamu,+
Ndiyo, hata wenye wako kichwa-nguvu,+ ili ukae kati yao, Ee Yah Mungu.
19 Yehova asifiwe, yeye mwenye anatubebea muzigo wetu kila siku,+
Mungu wa kweli wa wokovu wetu. (Sela)
20 Kwetu, Mungu wa kweli ni Mungu mwenye kuokoa;+
Na Yehova Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi anaokoa katika kifo.+
21 Ndiyo, Mungu ataponda-ponda vichwa vya maadui wake,
Ataponda-ponda sehemu ya juu ya katikati ya kichwa yenye nywele ya mutu yeyote mwenye anaendelea* katika hatia yake.+
22 Yehova amesema: “Nitawarudisha kutoka Bashani;+
Nitawarudisha kutoka sehemu za chini kabisa za bahari,
23 Ili muguu wako ufunikwe na damu+
Na ulimi wa imbwa zako upate fungu lake kutoka kwa maadui.”
24 Wanaona misururu yako, Ee Mungu,
Misururu ya Mungu wangu, Mufalme wangu, ikiingia mahali patakatifu.+
25 Waimbaji wanatangulia mbele, wapiga-muziki wenye kupiga vyombo vya kamba wanawafuata;+
Katikati yao kuko vijana wanamuke wenye kupiga ngoma za kidogo.*+
26 Katika vikundi vya watu wenye kukutanika,* mumusifu Mungu;
Mumusifu Yehova, ninyi wenye kutoka katika Chemchemi ya Israeli.+
27 Kule Benyamini,+ ule mudogo zaidi, anawatiisha,
Pia wakubwa wa Yuda pamoja na kikundi chao cha watu wenye fujo,
Wakubwa wa Zabuloni, wakubwa wa Naftali.
28 Mungu wako ameamuru kwamba utakuwa na nguvu.
Onyesha nguvu zako, Ee Mungu, wewe mwenye umetenda kwa ajili yetu.+
30 Kemea wanyama wa pori wenye kuwa katika matete,
Mukusanyiko wa ngombe-dume+ na vitoto-dume vyao,
Mupaka wakati vikundi vya watu vitainama vikileta* vipande vya feza.
Lakini anasambaza vikundi vya watu wenye kupenda vita.
31 Vitu vya shaba nyekundu vitaletwa kutoka* Misri;+
Kushi itafanya haraka ili kumupatia Mungu zawadi.
33 Ule mwenye anapanda mbingu ya zamani ya zile mbingu.+
Angalia! Ananguruma kwa sauti yake, sauti yake yenye nguvu.
34 Mutambue nguvu za Mungu.+
Ukubwa wake uko juu ya Israeli,
Na nguvu zake ziko katika anga.*
35 Mungu ni mwenye kuogopesha sana kutoka katika patakatifu pake* pakubwa.+
Yeye ni Mungu wa Israeli,
Mwenye kupatia watu uwezo na nguvu.+
Mungu asifiwe.