Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 2 Wakorinto 7
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 2 Wakorinto

      • Tujisafishe uchafu (1)

      • Furaha ya Paulo juu ya Wakorinto (2-4)

      • Tito analeta habari ya muzuri (5-7)

      • Huzuni yenye kupatana na mapenzi ya Mungu, na toba  (8-16)

2 Wakorinto 7:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Kor. 6:16
  • +Rom. 12:1; 1 Tim. 1:5; 3:9; 1 Yo. 3:3

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    “Upendo wa Mungu,” uku. 93

    Munara wa Mulinzi,

    1/11/2006, uku. 26

    Furaha ya Familia,

    uku. 45-48

2 Wakorinto 7:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Rom. 12:10; 2 Kor. 6:12, 13
  • +Mdo 20:33, 34; 2 Kor. 12:17

2 Wakorinto 7:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Flp 2:17; Flm 7

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/5/2006, uku. 15

2 Wakorinto 7:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 20:1

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/6/2014, uku. 23

2 Wakorinto 7:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Kor. 1:3, 4

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 166

2 Wakorinto 7:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “bidii yenu.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 166

2 Wakorinto 7:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Kor. 2:4

2 Wakorinto 7:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 32:5; 1 Yo. 1:9

2 Wakorinto 7:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kuwa na mwenendo safi; bila kosa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mt 3:8

2 Wakorinto 7:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Kor. 5:5

2 Wakorinto 7:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “upendo wake mwororo.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Kor. 2:9; Ebr 13:17

2 Wakorinto 7:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao pengine, “ninaweza kuwa na ujasiri kwa sababu yenu.”

Maandiko ingine

2 Wakorintho 7:12 Kor. 6:16
2 Wakorintho 7:1Rom. 12:1; 1 Tim. 1:5; 3:9; 1 Yo. 3:3
2 Wakorintho 7:2Rom. 12:10; 2 Kor. 6:12, 13
2 Wakorintho 7:2Mdo 20:33, 34; 2 Kor. 12:17
2 Wakorintho 7:4Flp 2:17; Flm 7
2 Wakorintho 7:5Mdo 20:1
2 Wakorintho 7:62 Kor. 1:3, 4
2 Wakorintho 7:82 Kor. 2:4
2 Wakorintho 7:10Zab 32:5; 1 Yo. 1:9
2 Wakorintho 7:11Mt 3:8
2 Wakorintho 7:121 Kor. 5:5
2 Wakorintho 7:152 Kor. 2:9; Ebr 13:17
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
2 Wakorinto 7:1-16

Ya Pili kwa Wakorinto

7 Kwa hiyo, wapendwa, kwa kuwa tuko na ahadi hizi,+ tujisafishe kila uchafu wa mwili na roho,+ tukikamilisha utakatifu katika kumuogopa Mungu.

2 Mutupatie nafasi katika mioyo yenu.+ Hatukumukosea mutu yeyote, hatukumuharibu mutu yeyote, hatukumudanganya mutu yeyote ili tupate faida.+ 3 Siseme jambo hili ili kuwahukumu ninyi. Kwa maana nimekwisha kusema kwamba ninyi muko ndani ya mioyo yetu ili kufa pamoja na kuishi pamoja. 4 Niko na uhuru mwingi wa kusema kuwaelekea ninyi. Ninajisifu kwa njia kubwa kuhusiana na ninyi. Nimejaa faraja; ninajaa sana furaha katika taabu yetu yote.+

5 Kwa kweli, wakati tulifika Makedonia,+ miili yetu haikupata kitulizo, lakini tuliendelea kuteswa katika kila njia⁠—⁠kulikuwa mapigano inje, woga ndani. 6 Lakini Mungu, mwenye kufariji wale wenye wameshuka moyo,+ alitufariji kupitia kuwapo kwa Tito; 7 na haiko kupitia kuwapo kwake tu lakini pia kupitia faraja yenye alipokea kwa sababu yenu, kwa kuwa wakati alirudia, alitujulisha juu ya tamaa yenu ya kuniona, huzuni yenu nyingi, na namna mulihangaika sana* juu yangu; basi nikafurahi hata zaidi.

8 Kwa maana hata kama niliwahuzunisha ninyi kwa barua yangu,+ sisikitike juu ya jambo hilo. Hata kama pale mwanzo nilisikitika (wakati niliona kwamba barua hiyo iliwahuzunisha ninyi, hata kama ni kwa wakati kidogo tu), 9 sasa ninafurahi, haiko kwa sababu mulihuzunishwa tu, lakini kwa sababu mulihuzunishwa mupaka mukatubu. Kwa maana mulihuzunishwa kwa namna yenye kupatana na mapenzi ya Mungu, na hivyo hamukupatwa na jambo lolote la mubaya kwa sababu yetu. 10 Kwa maana kuwa na huzuni kwa njia yenye kupatana na mapenzi ya Mungu kunatokeza toba yenye kuongoza kwenye wokovu, bila kufanya mutu asikitike;+ lakini huzuni ya ulimwengu inatokeza kifo. 11 Kwa maana, muone namna huzuni yenu yenye kupatana na mapenzi ya Mungu ilitokeza bidii nyingi ndani yenu, ndiyo, kujisafisha wenyewe, ndiyo, kasirani kali, ndiyo, woga, ndiyo, kutamani sana, ndiyo, bidii, ndiyo, kutengeneza kosa!+ Katika kila njia mulijionyesha kuwa safi* juu ya jambo hili. 12 Hata kama niliwaandikia ninyi, sikufanya vile kwa ajili ya ule mutu mwenye alifanya kosa,+ ao kwa ajili ya ule mutu mwenye alikosewa, lakini ili bidii yenu kwa ajili yetu ionekane wazi katikati yenu mbele ya macho ya Mungu. 13 Ndiyo sababu tumefarijiwa.

Lakini kwa kuongezea faraja yetu, tulifurahi hata zaidi juu ya furaha ya Tito, kwa sababu ninyi wote muliburudisha roho yake. 14 Kwa maana kama nimejisifu mbele yake juu yenu, sikupata haya; lakini kama vile mambo yenye tuliwaambia ninyi yalikuwa ya kweli, ni vile pia kujisifu kwetu mbele ya Tito kumekuwa kweli. 15 Pia, upendo wake wenye upole* kuwaelekea ninyi ni mukubwa wakati anakumbuka utii wenu ninyi wote,+ namna mulimupokea kwa kuogopa na kutetemeka. 16 Ninafurahi kwamba katika kila njia ninaweza kuwatumainia ninyi.*

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine