Ya Kwanza kwa Watesalonike
3 Basi wakati hatukuweza tena kuvumilia jambo hilo, tuliona ni muzuri zaidi tubakie Atene peke yetu;+ 2 na tukamutuma Timoteo,+ ndugu yetu na mutumishi* wa Mungu katika kutangaza habari njema juu ya Kristo, ili awafanye ninyi kuwa imara na kuwafariji kwa ajili ya imani yenu, 3 ili mutu yeyote asitikiswe* na taabu hizo. Kwa maana ninyi wenyewe munajua kama hatuwezi kuepuka mateso hayo.*+ 4 Kwa maana, wakati tulikuwa pamoja na ninyi, tulikuwa tunawaambia mbele ya wakati kwamba tutapata taabu, na ni vile mambo yametokea, kama vile munajua.+ 5 Hiyo ndiyo sababu, wakati sikuweza tena kuvumilia hilo, nilimutuma Timoteo kwenu ili nipate habari juu ya uaminifu wenu,+ kwa sababu, pengine kwa njia fulani Mujaribu+ alikuwa amewajaribu, na hivyo kazi yetu ya jasho ikuwe ya bure.
6 Lakini Timoteo amekuja sasa hivi kutoka kwenu+ na ametupatia habari njema juu ya uaminifu na upendo wenu, kwamba sikuzote munaendelea kufurahi wakati munatukumbuka, na kwamba munatamani kutuona kama vile sisi pia tunatamani kuwaona ninyi. 7 Hiyo ndiyo sababu, ndugu, katika mateso* na taabu zetu zote, tumefarijiwa kwa sababu yenu na uaminifu wenye munaonyesha.+ 8 Kwa sababu tunatiwa tena nguvu* kama munasimama imara katika Bwana. 9 Kwa maana, namna gani tunaweza kuonyesha shukrani yetu kwa Mungu kwa ajili yenu kwa sababu ya furaha kubwa yenye tuko nayo mbele ya Mungu wetu kwa sababu yenu? 10 Usiku na muchana tunatoa sala za kumulilia Mungu* kwa bidii yetu yote ili tuwaone ninyi uso kwa uso* na kuongeza jambo lenye munakosewa katika imani yenu.+
11 Sasa Mungu mwenyewe ambaye ni Baba yetu, pamoja na Bwana wetu Yesu watuwezeshe kuja kwenu. 12 Zaidi ya hayo, Bwana awafanye ninyi muongezeke, ndiyo, mujae sana katika upendo kwa mutu na mwenzake+ na kwa watu wote, kama vile sisi tunawatendea ninyi, 13 ili afanye mioyo yenu kuwa imara, yenye haina lawama katika utakatifu mbele ya Mungu+ na Baba yetu wakati wa kuwapo kwa Bwana wetu Yesu+ pamoja na watakatifu wake wote.