Cha Kwanza cha Samweli
4 Na neno la Samweli likafikia Israeli wote.
Kisha Israeli wakaenda kupigana na Wafilisti; wakapiga kambi pembeni ya Ebenezeri, na Wafilisti walikuwa wamepiga kambi Afeki. 2 Wafilisti wakajipanga kwa ajili ya vita ili kukutana na Israeli, lakini pigano likaendeka mubaya na Israeli wakashindwa na Wafilisti, wenye walipiga na kuua wanaume karibu elfu ine (4 000) kwenye kiwanja cha pigano katika eneo la mashamba. 3 Wakati watu walirudia katika kambi, wazee wa Israeli wakasema: “Sababu gani Yehova ameruhusu tushindwe leo na Wafilisti?*+ Tulete sanduku la agano la Yehova kutoka Shilo,+ ili likuwe pamoja na sisi na lituokoe katika mukono wa maadui wetu.” 4 Kwa hiyo watu wakatuma wanaume kuenda Shilo, na wakabeba kutoka kule sanduku la agano la Yehova wa majeshi, mwenye anakaa akiwa mufalme juu ya* makerubi.+ Wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi,+ walikuwa pia kule pamoja na sanduku la agano la Mungu wa kweli.
5 Wakati tu sanduku la agano la Yehova liliingia katika kambi, Waisraeli wote wakaanza kufanya makelele kwa sauti kubwa, na hivyo dunia ikatikisika. 6 Wakati Wafilisti walisikia sauti ya makelele hayo, wakasema: “Sababu gani kuko makelele mingi sana katika kambi ya Waebrania?” Mwishowe wakapata habari kwamba Sanduku la Yehova lilikuwa limeingia katika kambi. 7 Wafilisti wakaogopa, kwa sababu walisema: “Mungu ameingia katika kambi!”+ Kwa hiyo wakasema: “Ole wetu, kwa maana jambo kama hili halijatokeaka mbele! 8 Ole wetu! Ni nani atatuokoa katika mukono wa Mungu huyu mwenye utukufu? Huyu ndiye Mungu mwenye alipiga Misri kwa kila namna ya mauaji katika jangwa.+ 9 Mukuwe hodari na mutende kama wanaume, ninyi Wafilisti, ili musiwatumikie Waebrania kama vile waliwatumikia ninyi.+ Mutende kama wanaume na mupigane!” 10 Kwa hiyo Wafilisti wakapigana, na Israeli wakashindwa,+ na kila mumoja akakimbilia katika hema yake. Mauaji yalikuwa makubwa sana; kwa upande wa Israeli, maaskari elfu makumi tatu (30 000) wenye kutembea kwa miguu waliuawa. 11 Tena, Sanduku la Mungu likakamatwa, na wana wawili wa Eli, Hofni na Finehasi, wakakufa.+
12 Mutu fulani wa Benyamini akakimbia kutoka katika uwanja wa vita na akafika Shilo siku hiyo akiwa amevaa nguo zenye kupasuka na akiwa na mavumbi kwenye kichwa chake.+ 13 Wakati mutu huyo alifika, Eli alikuwa amekaa kwenye kiti pembeni ya barabara na alikuwa anaangalia, kwa kuwa moyo wake ulikuwa unatetemeka kwa sababu ya Sanduku la Mungu wa kweli.+ Mutu huyo akaingia katika muji ili kujulisha habari hiyo, na muji wote ukaanza kulia kwa sauti kubwa. 14 Wakati Eli alisikia sauti ya vilio hivyo, akauliza: “Sauti ya muvurugo huu ni ya nini?” Mutu uleule akaingia haraka na kumujulisha Eli habari hiyo. 15 (Wakati huo Eli alikuwa na miaka makumi kenda na munane [98], na macho yake yalikuwa yanaangalia mbele tu, na hakuweza kuona.)+ 16 Kisha mutu huyo akamuambia Eli: “Ni mimi nilitoka kwenye uwanja wa pigano! Leo hii nimekimbia kutoka kwenye uwanja wa pigano.” Basi Eli akauliza: “Ni nini ilitokea, mwana wangu?” 17 Kwa hiyo mutu huyo mwenye alileta habari akaeleza: “Israeli wamekimbia Wafilisti, na watu wameshindwa mubaya sana;+ pia, wana wako wawili, Hofni na Finehasi, wamekufa,+ na Sanduku la Mungu wa kweli limekamatwa.”+
18 Wakati alitaja Sanduku la Mungu wa kweli, Eli akaangukia nyuma kutoka kwenye kiti chake pembeni ya mulango mukubwa, na shingo yake ikavunjika na akakufa, kwa sababu alikuwa amezeeka na alikuwa muzito. Alikuwa amehukumu Israeli kwa miaka makumi ine (40). 19 Binti-mukwe wake, bibi ya Finehasi, alikuwa na mimba na alikuwa karibu kuzaa. Wakati alisikia habari kwamba Sanduku la Mungu wa kweli limekamatwa na kwamba baba-mukwe wake na bwana yake wamekufa, akajikunja na kwa kushitukia akapata uchungu wa kuzaa na akazaa. 20 Wakati alikuwa anakufa, wanamuke wenye walikuwa wamesimama pembeni yake wakasema: “Usiogope, kwa maana umemuzaa mwana.” Hakujibu na hakukazia uangalifu jambo hilo.* 21 Lakini alimuita mwana huyo Ikabodi,*+ na kusema: “Utukufu umetoka Israeli na kuenda katika uhamisho,”+ alikuwa anazungumuzia Sanduku la Mungu wa kweli lenye lilikamatwa na mambo yenye yalimupata baba-mukwe wake na bwana yake.+ 22 Akasema: “Utukufu umetoka Israeli na kuenda katika uhamisho, kwa sababu Sanduku la Mungu wa kweli limekamatwa.”+