Isaya
60 “Simama, Ee mwanamuke,+ toa mwangaza, kwa maana mwangaza wako umekuja.
Utukufu wa Yehova unakuangazia.+
2 Kwa maana, angalia! giza litafunika dunia
Na weusi muzito utafunika mataifa;
Lakini Yehova atakuangazia,
Na utukufu wake utaonekana juu yako.
4 Inua macho yako na uangalie pande zote kukuzunguka!
Wote wamekusanywa; wanakuja kwako.
Watoto wako wanaume wanaendelea kuja kutoka mbali sana,+
Na watoto wako wanamuke wakiwa wametegemezwa kwenye kiuno.+
5 Wakati huo utaona na kungaa,+
Na moyo wako utapiga na kujaa sana,
Kwa sababu utajiri wa bahari utaelekezwa kwako;
Mali za mataifa zitakuja kwako.+
Wale wote wenye kutoka Sheba—watakuja;
Watabeba zahabu na ubani.
Watatangaza sifa za Yehova.+
7 Makundi yote ya Kedari+ yatakusanywa kwako.
Kondoo-dume wa Nebayoti+ watakutumikia.
9 Kwa maana visiwa vitanitumainia;+
Mashua* za Tarshishi zinaongoza,*
Kuleta watoto wako wanaume kutoka mbali,+
Wakiwa na feza yao na zahabu yao,
Kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wako na kwa Mutakatifu wa Israeli,
10 Wageni watajenga kuta zako,
Na wafalme wao watakutumikia,+
Kwa maana nilikupiga katika kasirani yangu kali,
11 Milango yako mikubwa itakuwa wazi kila wakati;+
Haitafungwa muchana wala usiku,
Ili kukuletea mali za mataifa,
Na wafalme wao wataongoza.+
12 Kwa maana taifa lolote na ufalme wowote wenye hautakutumikia utaangamia,
Na mataifa yataharibiwa kabisa.+
13 Utukufu wa Lebanoni utakuja kwako,+
Muti wa muberoshi, muti wa mutizari, na muti wa muvinje pamoja,+
Ili kupamba patakatifu pangu;
Nitatukuza mahali pa miguu yangu.+
14 Wana wa wale wenye walikukandamiza watakuja na kuinama mbele yako;
Wale wote wenye kukutendea bila heshima watainama kwenye miguu yako,
Na watakuita muji wa Yehova,
Sayuni ya Mutakatifu wa Israeli.+
15 Kuliko kuwa mwenye aliachwa na kuchukiwa, bila mutu mwenye kupita ndani yako,+
Nitakufanya kuwa kiburi cha milele,
Chanzo cha shangwe katika vizazi vyote.+
16 Na kwa kweli utakunywa maziwa ya mataifa,+
Utanyonya maziwa ya wafalme;+
Na hakika utajua kwamba mimi, Yehova, ni Mwokozi wako,
Na Mwenye Nguvu wa Yakobo ni Mukombozi wako.+
17 Pa nafasi ya shaba nitaleta zahabu,
Na pa nafasi ya chuma nitaleta feza,
Pa nafasi ya mbao, shaba,
Na pa nafasi ya majiwe, chuma;
Na nitaweka amani kuwa waangalizi wako
Na haki kuwa watu wako wa kugawa kazi.+
Na utaita kuta zako Wokovu+ na milango yako mikubwa Sifa.
19 Kwa maana jua halitakuwa tena mwangaza wako wakati wa muchana,
Wala mwangaza wa mwezi hautakuangazia,
Kwa maana Yehova atakuwa mwangaza wako wa milele,+
Na Mungu wako atakuwa uzuri wako.+
20 Jua lako halitashuka tena,
Wala mwezi wako hautafifia,
Kwa maana Yehova atakuwa mwangaza wako wa milele,+
Na siku zako za kuomboleza zitakuwa zimeisha.+
22 Mudogo atakuwa elfu (1 000)
Na mutu wa hali ya chini atakuwa taifa lenye nguvu.
Mimi mwenyewe, Yehova, nitaharakisha jambo hilo kwa wakati wake.”