Ezekieli
21 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, elekeza uso wako Yerusalemu, na utoe tangazo juu ya mahali patakatifu, na kutoa unabii juu ya inchi ya Israeli. 3 Ambia inchi ya Israeli, ‘Yehova anasema hivi: “Angalia, nitapigana na wewe, na nitatosha upanga wangu katika mufuko wake wa upanga+ na kuondoa katikati yako mwenye haki na muovu. 4 Kwa sababu nitaondoa katikati yako mwenye haki na muovu, upanga wangu utachomolewa katika mufuko wake ili kushambulia miili yote,* kuanzia kusini mupaka kaskazini. 5 Watu wote watalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimechomoa upanga wangu kutoka katika mufuko wake. Hautarudia tena.”’+
6 “Na wewe, mwana wa binadamu, lia kwa maumivu ukitetemeka,* ndiyo, lia kwa uchungu mbele yao.+ 7 Na kama wanakuambia, ‘Sababu gani unalia kwa maumivu?’ utasema, ‘Kwa sababu ya habari fulani.’ Kwa maana hakika itakuja, na kila moyo utayeyuka kwa sababu ya woga na kila mukono utaninginia kwa uregevu na kila roho itahuzunika na kila goti litaangusha matone-matone ya maji.*+ ‘Angalia! Hakika itakuja—itatokea,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”
8 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 9 “Mwana wa binadamu, toa unabii na useme, ‘Yehova anasema hivi: “Sema, ‘Upanga! Upanga+ umenolewa, na umengarishwa. 10 Umenolewa kwa ajili ya uchinjaji mukubwa; umengarishwa ili ungae kama umeme wa radi.’”’”
“Je, hatupaswe kushangilia?”
“‘Je, utakataa* fimbo ya ufalme ya mwana wangu,+ kama vile kila muti unakataa?
11 “‘Umetolewa ili ungarishwe sana na kutumiwa kwa mukono. Upanga huo umenolewa na kungarishwa, ili utiwe katika mukono wa muuaji.+
12 “‘Mwana wa binadamu, lalamika na uomboleze,+ kwa maana upanga umekuja juu ya watu wangu; uko juu ya wakubwa wote wa Israeli.+ Hao wataharibiwa kwa upanga huo pamoja na watu wangu. Kwa hiyo piga paja lako kwa huzuni. 13 Kwa maana uchunguzi umefanywa,+ na nini itatokea ikiwa upanga unakataa fimbo ya ufalme? Haitaendelea* kuwa,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.
14 “Na wewe, mwana wa binadamu, toa unabii, na upige mikono na useme mara tatu (3) ‘Upanga!’ Ni upanga wa watu wenye kuuawa, upanga wa uchinjaji mukubwa, wenye kuwazunguka.+ 15 Mioyo yao itayeyuka kwa sababu ya woga+ na wengi wataanguka kwenye milango mikubwa ya muji wao; nitaleta mauaji kwa upanga. Ndiyo, unangaa kama umeme wa radi na umengarishwa ili kuchinja! 16 Kata sana upande wa kuume! Geukia upande wa kushoto! Uende mahali popote kwenye sehemu yako ya kukatia imeelekezwa! 17 Na mimi pia nitapiga mikono na kutosheleza kasirani yangu kali.+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.”
18 Na neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 19 “Sasa wewe, mwana wa binadamu, chora njia mbili ili upanga wa mufalme wa Babiloni ukuje. Zote mbili zitatoka katika inchi moja, na alama ya kuonyesha njia* inapaswa kusimamishwa mahali kwenye barabara inatengana ili kuingia katika ile miji mbili. 20 Unapaswa kuchora njia moja ili upanga ukuje juu ya Raba+ ya Waamoni, na njia ingine juu ya muji wa Yerusalemu wenye ngome+ katika Yuda. 21 Kwa maana mufalme wa Babiloni amesimama ili kufanya uaguzi kwenye njia-panda katika barabara, mahali kwenye zile barabara mbili zinatengana. Anatikisa mishale. Anauliza habari kutoka kwa sanamu* zake; anachunguza maini. 22 Uaguzi wenye kuwa katika mukono wake wa kuume umeelekezwa Yerusalemu, ili kusimamisha vyombo vya kubomolea, ili kutoa agizo la kuchinja, ili kufanya makelele ya vita, ili kutia mashine za kubomolea juu ya milango mikubwa, ili kujenga boma la kuzunguka kwa ajili ya vita, ili kujenga ukuta wa kuzunguka kwa ajili ya vita.+ 23 Lakini utaonekana kama uaguzi wa uongo mbele ya macho ya wale* wenye walikuwa wamewaapia viapo.+ Lakini anakumbuka hatia yao naye atawakamata.+
24 “Kwa hiyo, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Mumefanya hatia yenu ikumbukwe kwa kufunua makosa yenu na kufanya zambi zenu zionekane katika matendo yenu yote. Kwa kuwa sasa mumekumbukwa, mutakamatwa kwa nguvu.’*
25 “Lakini siku yako imefika, Ee mwenye umeumizwa mubaya, mukubwa muovu wa Israeli,+ wakati wa azabu yako ya mwisho. 26 Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Ondoa kilemba, na utoshe taji.+ Hili halitabakia namna liko.+ Inua mwenye kuwa chini,+ na ushushe mwenye kuwa juu.+ 27 Nitaliharibu, nitaliharibu, nitaliharibu. Na halitakuwa la mutu yeyote mupaka wakati ule mwenye kuwa na haki ya kisheria atakuja,+ na mimi nitamupatia hilo.’+
28 “Na wewe, mwana wa binadamu, toa unabii na useme, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi kuhusu Waamoni na kuhusu matusi yao.’ Sema, ‘Upanga! Upanga umechomolewa kwa ajili ya kuchinja; umengarishwa ili kuharibu na ili kungaa kama umeme wa radi. 29 Ijapokuwa maono ya uongo na uaguzi wa uongo kuwahusu ninyi, mutakusanywa juu ya watu wenye kuuawa,* watu waovu wenye siku yao imefika, wakati wa azabu yao ya mwisho. 30 Rudisha upanga katika mufuko wake. Nitakuhukumu mahali kwenye uliumbwa, katika inchi ya asili yako. 31 Nitamwanga gazabu yangu juu yako. Nitapuliza juu yako kwa moto wa kasirani yangu kali, na nitakutia katika mukono wa watu wenye hawana huruma, mafundi wa uharibifu.+ 32 Utakuwa kuni kwa ajili ya moto;+ damu yako mwenyewe itamwangwa katika inchi, na hautakumbukwa tena, kwa maana mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.’”