Isaya
9 Lakini, gizagiza hilo halitakuwa kama wakati inchi ilikuwa na taabu, kama nyakati za zamani wakati inchi ya Zabuloni na inchi ya Naftali zilizarauliwa.+ Lakini kisha wakati fulani Yeye ataifanya iheshimiwe—njia ya pembeni ya bahari, katika eneo la Yordani, Galilaya ya mataifa.
2 Watu wenye walikuwa wanatembea katika giza
Wameona mwangaza mukubwa.
Na wale wenye kukaa katika inchi ya kivuli kizito,
Mwangaza umewaangazia.+
3 Umefanya taifa hilo likuwe na watu wengi;
Umefanya shangwe yake ikuwe kubwa.
Wanashangilia mbele yako
Kama watu wenye kushangilia wakati wa mavuno,
Kama wale wenye kugawanya kwa shangwe vitu vyenye vinachukuliwa katika vita.
4 Kwa maana umevunja-vunja nira ya muzigo wao,
Fimbo yenye kuwa kwenye mabega yao, fimbo ya musimamizi wa kazi,
Kama katika siku ya Midiani.+
5 Kila kiatu chenye kinatikisa dunia wakati kinatembea
Na kila nguo yenye kutiwa katika damu
Itakuwa kuni kwa ajili ya moto.
Jina lake litakuwa Mushauri wa Ajabu,+ Mungu Mwenye Nguvu,+ Baba wa Milele, Mukubwa wa Amani.
7 Kuongezeka kwa utawala wake*
Na amani, havitakuwa na mwisho,+
Kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ na juu ya ufalme wake
Ili kuufanya kuwa imara kabisa+ na kuutegemeza
Kuanzia sasa na milele.
Bidii ya Yehova wa majeshi itatenda mambo hayo.
9 Na watu wote watalijua,
—Efraimu na wakaaji wa Samaria—
Wenye wanasema katika kiburi chao na katika moyo wao wenye zarau:
Miti ya mikuyu imekatwa,
Lakini tutatia miti ya mierezi pa nafasi yake.”
11 Yehova atainua wapinzani wa Resini ili wapigane naye,
Na atachochea maadui wake watende,
12 Siria kutoka mashariki na Wafilisti kutoka mangaribi,*+
Watakula Israeli kwa vinywa vyenye kuwa wazi.+
Kwa sababu ya mambo hayo yote, kasirani yake haijarudia nyuma,
Lakini mukono wake ungali wenye kunyooshwa ili kupiga.+
15 Muzee na mutu mwenye kuheshimiwa sana ndiye kichwa,
Na nabii mwenye kutoa mafundisho ya uongo ndiye mukia.+
16 Wale wenye kuongoza watu hawa wanawafanya watange-tange;
Na wale wenye kuongozwa wamevurugika.
17 Ndiyo sababu Yehova hatashangilia juu ya vijana wao wanaume,
Na hatawaonyesha rehema watoto wao wenye hawana baba* na wajane wao;
Kwa sababu wote ni waasi-imani na watenda-maovu+
Na kila kinywa kinasema upumbavu.
Kwa sababu ya mambo hayo yote, kasirani yake haijarudia nyuma,
Lakini mukono wake ungali wenye kunyooshwa ili kupiga.+
18 Kwa maana uovu unawaka kama moto,
Unateketeza kwa moto miti midogo-midogo ya miiba na magugu.
Utawasha moto miti midogo-midogo ya pori,
Na itapanda juu katika mawingu ya moshi.
19 Katika kasirani kali ya Yehova wa majeshi
Inchi imewashwa moto,
Na watu watakuwa kuni kwa ajili ya moto.
Hakuna mwenye atakosa kuharibu hata ndugu yake.
20 Mutu atakata kwenye upande wa kuume
Lakini ataendelea kuwa na njaa;
Na mutu atakula kwenye upande wa kushoto
Lakini hatashiba.
Kila mutu atakula nyama ya mukono wake mwenyewe,
21 Manase atakula Efraimu,
Na Efraimu atakula Manase.
Wote pamoja watapigana na Yuda.+
Kwa sababu ya mambo hayo yote, kasirani yake haijarudia nyuma,
Lakini mukono wake ungali wenye kunyooshwa ili kupiga.+