Kwa Waebrania
8 Sasa jambo kubwa la mambo yenye tunasema ni hili: Tuko na kuhani mukubwa wa namna hii,+ na amekaa kwenye mukono wa kuume wa kiti cha ufalme cha Ukubwa mbinguni,+ 2 mutumishi* wa mahali patakatifu+ na wa hema ya kweli, yenye imesimamishwa na Yehova,* hapana na mwanadamu. 3 Kwa maana kila kuhani mukubwa anawekwa ili kutoa zawadi na pia zabihu; basi ilikuwa lazima huyu pia akuwe na kitu cha kutoa.+ 4 Kama angekuwa katika dunia, hangekuwa kuhani,+ kwa kuwa tayari kuko watu wenye wanatoa zawadi kulingana na Sheria. 5 Watu hao wanatoa utumishi mutakatifu katika mufano na kivuli+ cha vitu vya mbinguni;+ kama vile Musa, wakati alikuwa karibu kujenga hema, alipewa amri na Mungu: Kwa maana Mungu anasema: “Uhakikishe kwamba unatengeneza vitu vyote kulingana na mufano wavyo wenye ulionyeshwa kwenye mulima.”+ 6 Lakini sasa Yesu amepata utumishi* wa muzuri zaidi kwa sababu yeye vilevile ni mupatanishi+ wa agano la muzuri zaidi,+ lenye limewekwa kisheria juu ya ahadi ya muzuri zaidi.+
7 Kama lile agano la kwanza halingekuwa na kosa, hakungekuwa lazima ya agano la pili.+ 8 Kwa maana analaumu watu wakati anasema: “‘Angalia! Siku zinakuja,’ ni vile Yehova* anasema, ‘wakati nitafanya agano jipya pamoja na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda. 9 Halitakuwa kama lile agano lenye nilifanya pamoja na mababu zao ile siku yenye nilishika mukono wao ili kuwaongoza kutoka katika inchi ya Misri,+ kwa sababu hawakubakia katika agano langu, basi nikaacha kuwahangaikia,’ ni vile Yehova* anasema.
10 “‘Kwa maana hili ndilo agano lenye nitafanya pamoja na nyumba ya Israeli kisha siku hizo,’ ni vile Yehova* anasema. ‘Nitatia sheria zangu katika akili yao, na nitaziandika katika mioyo yao.+ Na nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.+
11 “‘Na hawatafundishana tena kila mutu na mwanainchi mwenzake na kila mutu na ndugu yake, wakisema: “Umujue Yehova!”* Kwa maana wote watanijua, kuanzia mudogo zaidi mupaka mukubwa zaidi kati yao. 12 Kwa maana nitakuwa mwenye rehema kuelekea matendo yao yenye hayako ya haki, na sitakumbuka tena zambi zao.’”+
13 Wakati anasema “agano jipya,” amefanya lile la zamani likuwe lenye halifae tena.+ Basi kile chenye hakifae tena na chenye kuzeeka kiko karibu kupotea.+