Yeremia
24 Kisha Yehova akanionyesha vitunga mbili vya tini vyenye viliwekwa mbele ya hekalu la Yehova, kisha Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni kupeleka katika uhamisho Yekonia*+ mwana wa Yehoyakimu,+ mufalme wa Yuda, pamoja na wakubwa wa Yuda, mafundi, na mafundi wa vyuma;* aliwachukua kutoka Yerusalemu na kuwapeleka Babiloni.+ 2 Kitunga kimoja kilikuwa na tini za muzuri sana, kama tini za kwanza-kwanza, lakini kile kitunga kingine kilikuwa na tini za mubaya sana, na hivyo hazingeweza kukuliwa.
3 Kisha Yehova akaniuliza: “Unaona nini, Yeremia?” Basi nikasema: “Tini; tini za muzuri ni za muzuri sana, lakini tini za mubaya ni za mubaya sana, mubaya sana na hivyo haziwezi kukuliwa.”+
4 Kisha neno la Yehova likakuja kwangu, na kusema: 5 “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Kama hizi tini za muzuri, ni vile nitaona kwa njia ya muzuri wale wahamishwa wa Yuda, wenye nimetosha hapa na kupeleka katika inchi ya Wakaldayo. 6 Nitaweka jicho langu juu yao kwa faida yao, na nitawarudisha katika inchi hii.+ Nitawajenga, na sitabomoa; nitawapanda, na sitangoa.+ 7 Na nitawapatia moyo wa kunijua, kwamba mimi ni Yehova.+ Watakuwa watu wangu, na mimi nitakuwa Mungu wao,+ kwa maana watarudia kwangu kwa moyo wao wote.+
8 “‘Lakini kuhusu zile tini za mubaya zenye ni za mubaya sana na hivyo haziwezi kukuliwa,+ Yehova anasema hivi: “Ni vile nitamuona Mufalme Sedekia+ wa Yuda, wakubwa wake, mabaki ya Yerusalemu wenye waliachwa katika inchi hii, na wale wenye kukaa katika inchi ya Misri.+ 9 Nitawafanya kuwa kitu cha kuogopesha na musiba kwa falme zote za dunia,+ haya, neno la kimezali, kitu cha kuchekelewa, na laana+ kila mahali kwenye ninawatawanya.+ 10 Na nitatuma juu yao upanga,+ njaa, na ugonjwa wa kuambukiza,+ mupaka waangamie kutoka katika inchi yenye niliwapatia wao na mababu zao.”’”