18 Kila mutu mwenye anajitenga na wengine anafuatilia tamaa zake mwenyewe za uchoyo;
Anakataa hekima yote yenye kutumika.
2 Mutu mujinga hafurahie uelewaji;
Lakini anafurahia kufunua mambo yenye kuwa katika moyo wake.+
3 Wakati mutu muovu anakuja, zarau inakuja pia,
Na kukosa heshima kunakuja pamoja na haya.+
4 Maneno ya kinywa cha mutu ni maji yenye kuenda chini sana.+
Chemchemi ya hekima ni muto mudogo wenye kububujika.
5 Haiko muzuri kuonyesha muovu upendeleo+
Wala kuima muadilifu haki.+
6 Maneno ya mujinga yanatokeza mabishano,+
Na kinywa chake kinafanya apigwe.+
7 Kinywa cha mujinga ndicho kinamuharibu,+
Na midomo yake ni mutego kwa uzima wake.
8 Maneno ya muchongezi ni kama matonge matamu;+
Yanamezwa na kushuka mara moja katika tumbo.+
9 Kila mutu mwenye kuwa muvivu katika kazi yake
Ni ndugu ya mutu mwenye kuleta uharibifu.+
10 Jina la Yehova ni munara wenye nguvu.+
Mwenye haki anakimbilia ndani na kupata ulinzi.+
11 Mali ya tajiri ni muji wake wenye ngome;
Ni kama ukuta wa ulinzi katika mawazo yake.+
12 Mbele ya kuanguka kwa kishindo moyo wa mutu ni wenye kiburi,+
Na mbele ya utukufu kuko unyenyekevu.+
13 Wakati mutu anajibu mbele ya kusikia ukweli wa mambo,
Huo ni upumbavu na haya.+
14 Roho ya mutu inaweza kumutegemeza katika ugonjwa,+
Lakini ni nani anaweza kuvumilia roho yenye kupondwa?+
15 Moyo wa mutu mwenye uelewaji unapata ujuzi,+
Na sikio la mwenye hekima linatafuta kupata ujuzi.
16 Zawadi ya mwanadamu inamufungulia njia;+
Inamuwezesha kufika mbele ya wakubwa.
17 Mutu wa kwanza kueleza kesi yake ya hukumu anaonekana kuwa anasema kweli,+
Mupaka wakati mwingine anafika na kumuuliza maulizo.+
18 Kupiga kura kunakomesha mabishano+
Na kunakata maneno kati ya wapinzani wenye nguvu.
19 Ndugu mwenye wamekosea ni mugumu kuliko muji wenye ngome,+
Na kuko mabishano yenye kuwa kama mapingo ya ngome.+
20 Tumbo la mutu litajazwa kutokana na matunda ya maneno yake;+
Atashiba mazao ya midomo yake.
21 Kifo na uzima viko katika nguvu za ulimi;+
Wale wenye wanapenda kuutumia watakula matunda yake.+
22 Mwenye anapata bibi muzuri anapata kitu kizuri,+
Na anapata wema wa Yehova.+
23 Maskini anabembeleza wakati anaongea,
Lakini tajiri anajibu kwa ukali.
24 Kuko marafiki wenye kuwa tayari kuumizana,+
Lakini kuko rafiki mwenye anashikamana sana na mutu kuliko ndugu.+