Zaburi
KITABU CHA INE
(Zaburi 90-106)
Sala ya Musa, mutu wa
Mungu wa kweli.+
90 Ee Yehova, umekuwa makao yetu*+ katika vizazi vyote.
2 Mbele milima haijazaliwa
Ao mbele haujatokeza* dunia na inchi yenye kuzaa,+
Tangu milele mupaka milele, wewe ni Mungu.+
3 Unamufanya mwanadamu mwenye anaweza kufa arudie katika mavumbi;
Unasema: “Murudie, ninyi wana wa binadamu.”+
4 Kwa maana miaka elfu moja (1 000) mbele ya macho yako ni kama vile siku ya jana ikiisha kupita,+
Kama vile kesha moja la usiku.
9 Siku zetu zinafifia* kwa sababu ya kasirani yako kali;
Na miaka yetu inafikia mwisho kama sauti ya chini-chini.
10 Urefu wa maisha yetu ni miaka makumi saba (70),
Lakini imejaa taabu na huzuni;
Na inapita haraka, na tunaenda zetu.+
11 Ni nani anaweza kuelewa nguvu za hasira yako?
Kasirani yako kali ni kubwa kama woga wenye unastahili kuonyeshwa.+
13 Rudia, Ee Yehova!+ Hilo litaendelea mupaka wakati gani?+
Sikilia huruma watumishi wako.+
14 Utushibishe asubui kwa upendo wako mushikamanifu,+
Ili tupige vigelegele vya shangwe na kushangilia+ siku zetu zote.