Ezekieli
17 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, tega kitendawili na useme mezali kuhusu nyumba ya Israeli.+ 3 Unapaswa kusema, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Tai mukubwa,+ mwenye mabawa makubwa, na manyoya ya murefu, na mwenye kujaa manyoya yenye rangi mbalimbali, alikuja Lebanoni+ na kukamata sehemu ya juu ya mwerezi.+ 4 Alingoa chipukizi lake la juu sana na kulileta kwenye inchi ya wafanyabiashara* na kulitia katika muji wa wafanyabiashara.+ 5 Kisha akakamata mbegu fulani ya inchi hiyo+ na kuitia katika shamba lenye mbolea. Akaipanda kama muti wa muvinje pembeni ya maji mengi. 6 Kwa hiyo ikachipuka na kuwa muzabibu mufupi, wenye kutambaa,+ wenye majani yenye kuelekea ndani na mizizi yenye kukomaa chini yake. Kwa hiyo, ukakuwa muzabibu na ukatokeza machipukizi na matawi.+
7 “‘“Na tai mwingine mukubwa akakuja,+ mwenye mabawa makubwa na manyoya makubwa.+ Kisha muzabibu huo ukanyoosha mizizi yake kwa bidii kumuelekea, mbali na maeneo ya kidogo-kidogo ya bustani kwenye ulipandwa, na ukaelekeza majani yake kwake ili aumwangilie maji.+ 8 Ulikuwa tayari umepandwa katika shamba la muzuri karibu na maji mengi, ili utokeze matawi, uzae matunda, na ukuwe muzabibu mukubwa.”’+
9 “Sema, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Je, utasitawi? Je, mutu fulani hatangoa mizizi yake+ na kufanya matunda yake yaoze na machipukizi yake yakauke?+ Utakauka sana na hivyo hautahitaji mukono wenye nguvu wala watu wengi ili kuungoa kupitia mizizi yake. 10 Hata kama ulingolewa na kupandwa mahali pengine, je, utasitawi? Je, hautakauka kabisa wakati upepo wa mashariki utavuma juu yake? Utakauka katika eneo la kidogo la bustani kwenye ulichipuka.”’”
11 Na neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 12 “Tafazali ambia nyumba yenye kuasi, ‘Je, hamutambue maana ya mambo haya?’ Sema, ‘Angalia! Mufalme wa Babiloni alikuja Yerusalemu na kukamata mufalme wake na wakubwa wake na kurudia pamoja nao Babiloni.+ 13 Tena, alikamata mumoja wa uzao wa* kifalme+ na kufanya agano pamoja naye na kumutia chini ya kiapo.+ Kisha akakamata watu wa maana wa inchi,+ 14 ili ufalme huo ushushwe chini, usiweze kusimama, ili uendelee kuwa ikiwa tu unaendelea kushika agano lake.+ 15 Lakini mwishowe mufalme huyo alimuasi+ kwa kutuma wajumbe wake Misri ili apate farasi+ na jeshi kubwa kutoka kwao.+ Je, atafanikiwa? Je, ule mwenye kufanya mambo hayo ataponyoka azabu? Je anaweza kuvunja agano na bado aponyoke?’+
16 “‘“Kama vile hakika ninaishi,” ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema, “atakufa kule Babiloni, mahali kwenye mufalme* mwenye alimufanya yeye* kuwa mufalme anaishi, ule mwenye alizarau kiapo chake na mwenye alivunja agano lake.+ 17 Na lile jeshi kubwa na wanajeshi wengi wa Farao hawatamusaidia katika vita,+ wakati maboma ya kuzingira yatasimamishwa na wakati kuta za kuzunguka kwa ajili ya vita zitajengwa ili kuharibu uzima wa* watu wengi. 18 Amezarau kiapo na kuvunja agano. Hata kama alitoa ahadi,* amefanya mambo hayo yote, naye hataponyoka.”’
19 “‘Kwa hiyo, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Kama vile hakika ninaishi, nitaleta juu ya kichwa chake matokeo ya kuzarau kiapo changu+ na kuvunja agano langu. 20 Nitatupa wavu wangu* juu yake, naye atakamatwa katika wavu wangu wa kuwindia.+ Nitamuleta Babiloni na kuingia katika hukumu pamoja naye kule kwa sababu ya ukosefu wa uaminifu wenye alinitendea.+ 21 Wakimbizi wote katikati ya wanajeshi wake wataanguka kwa upanga, na wale wenye watabakia watasambazwa kila upande.*+ Halafu mutalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.”’+
22 “‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Nitakamata chipukizi kutoka sehemu ya juu ya mwerezi murefu sana+ na kulipanda, kutoka sehemu ya juu ya matawi yake nitakata chipukizi la teketeke,+ na mimi mwenyewe nitalipanda juu ya mulima murefu na wenye kuwa juu sana.+ 23 Nitalipanda juu ya mulima murefu wa Israeli; na matawi yake yatakomaa, na litazaa matunda na kuwa mwerezi mukubwa. Na ndege wa kila namna wataishi chini yake na kukaa katika kivuli cha majani yake. 24 Na miti yote ya shamba italazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimeshusha ule muti murefu na kuinua ule muti mufupi;+ nimekausha ule muti mubichi na kufanya ule muti wenye kukauka utoe maua.+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema na nimefanya vile.”’”