Ya Pili ya Yohana
1 Mwanaume muzee,* kwa bibi mwenye alichaguliwa, na kwa watoto wake, wenye kwa kweli ninawapenda, na haiko mimi tu, lakini pia wale wote wenye wamejua kweli, 2 kwa sababu ya kweli yenye inakaa ndani yetu na itakuwa pamoja na sisi milele. 3 Tutakuwa na fazili zenye hazistahiliwe, rehema, na amani kutoka kwa Mungu Baba na kutoka kwa Yesu Kristo, Mwana wa Baba, pamoja na kweli na upendo.
4 Ninafurahi sana kwa sababu nimekuta wamoja kati ya watoto wako wakitembea katika kweli,+ kama vile tulipokea amri kutoka kwa Baba. 5 Basi, sasa ninakuomba, Ee bibi, kwamba tupendane. (Sikuandikie amri mupya, lakini amri yenye tulikuwa nayo tangu mwanzo.)+ 6 Na upendo unamaanisha hivi, kwamba tuendelee kutembea kulingana na amri zake.+ Hii ndiyo amri, kama vile mulisikia tangu mwanzo, kwamba munapaswa kuendelea kutembea ndani yake. 7 Kwa maana wadanganyifu wengi wametokea katika ulimwengu,+ wale wenye hawakubali kama Yesu Kristo alikuja katika mwili.+ Hao ndio ule mudanganyifu na mupinga-Kristo.+
8 Mufanye angalisho, ili musipoteze mambo yenye tumefanya kazi ili kuyatokeza, lakini ili mupate zawabu kamili.+ 9 Kila mutu mwenye anavuka mipaka na hakae katika fundisho la Kristo hana Mungu.+ Mutu mwenye anakaa katika fundisho hili ndiye mwenye kuwa na Baba na Mwana pia.+ 10 Kama mutu anakuja kwenu na halete fundisho hili, musimupokee katika nyumba zenu+ wala kumusalimia. 11 Kwa maana mutu mwenye anamusalimia anashiriki katika matendo yake maovu.
12 Hata kama niko na mambo mengi ya kuwaandikia ninyi, sitaki kufanya vile kwa karatasi na wino, lakini ninatumaini kuja kwenu na kuzungumuza na ninyi uso kwa uso, ili furaha yenu ikuwe kamili.
13 Watoto wa dada yako, ule muchaguliwa, wanakutumia salamu zao.