Yoshua
6 Basi Yeriko ilikuwa imefungwa kabisa kwa sababu ya Waisraeli; hakuna mutu alikuwa anatoka wala kuingia.+
2 Kisha Yehova akamuambia Yoshua: “Angalia, nimetia katika mikono yako Yeriko, mufalme wake, na wapiganaji-vita wake wenye nguvu.+ 3 Ninyi wote wanaume wa vita munapaswa kutembea kuzunguka muji, mutazunguka muji mara moja. Munapaswa kufanya vile kwa siku sita (6). 4 Uambie makuhani saba (7) watembee mbele ya Sanduku wakiwa wenye kubeba baragumu saba zenye zilitengenezwa kwa pembe za kondoo-dume. Lakini siku ya saba, mutazunguka muji mara saba na makuhani wapige zile baragumu.+ 5 Wakati pembe ya kondoo-dume itatoa sauti, ni kusema, wakati tu mutasikia sauti ya baragumu,* watu wote watafanya makelele makubwa ya vita. Kisha ukuta wa muji utaanguka chini,+ na watu watapanda, kila mutu ataenda mbele moja kwa moja.”
6 Basi Yoshua mwana wa Nuni akaita makuhani na kuwaambia: “Mubebe sanduku la agano, na makuhani saba (7) watembee mbele ya Sanduku la Yehova wakiwa wenye kubeba baragumu saba zenye zilitengenezwa kwa pembe za kondoo-dume.”+ 7 Kisha akaambia watu: “Muende na muzunguke muji, na wanajeshi wenye kubeba silaha+ wapite mbele ya Sanduku la Yehova.” 8 Na watu wakafanya kama vile Yoshua alikuwa amewaambia, makuhani saba (7) wenye kubeba mbele ya Yehova baragumu saba zenye zilitengenezwa kwa pembe za kondoo-dume wakapita mbele na kupiga zile baragumu, na sanduku la agano la Yehova lilikuwa linawafuata. 9 Na wanajeshi wenye kubeba silaha wakapita mbele ya makuhani wenye walikuwa wanapiga zile baragumu, na kikundi cha nyuma cha walinzi kilikuwa kinafuata Sanduku wakati baragumu ziliendelea kupigwa.
10 Na Yoshua alikuwa ameamuru watu: “Musifanye makelele wala musiache sauti zenu zisisikike. Musiseme neno lolote mupaka siku nitawaambia, ‘Mufanye makelele!’ Basi mutafanya makelele.” 11 Na akafanya Sanduku la Yehova lizunguke muji, likazunguka mara moja, kisha wakarudia katika kambi na wakalala usiku wote kule.
12 Yoshua akaamuka asubui sana siku yenye ilifuata, na makuhani wakabeba Sanduku+ la Yehova, 13 na makuhani saba (7) wenye kubeba baragumu saba zenye zilitengenezwa kwa pembe za kondoo-dume walitembea mbele ya Sanduku la Yehova wakiendelea kupiga zile baragumu. Na wanajeshi wenye kubeba silaha walitembea mbele yao na kikundi cha nyuma cha walinzi kilikuwa kinafuata Sanduku la Yehova wakati zile baragumu ziliendelea kupigwa. 14 Siku ya pili walizunguka muji mara moja, kisha wakarudia katika kambi. Walifanya vile kwa siku sita (6).+
15 Siku ya saba (7) waliamuka asubui sana, wakati tu kulipambazuka,* na wakazunguka muji kama kawaida lakini mara saba. Ni siku hiyo tu ndiyo walizunguka muji mara saba.+ 16 Na mara ya saba (7), makuhani walipiga zile baragumu, na Yoshua akaambia watu: “Mufanye makelele,+ kwa maana Yehova amewapatia muji huu! 17 Muji huu na vitu vyote vyenye kuwa ndani vinapaswa kuharibiwa;+ vyote ni vya Yehova. Rahabu tu+ ule kahaba ndiye anapaswa kuendelea kuishi, yeye na wale wote wenye kuwa katika nyumba yake, kwa sababu alificha wajumbe wenye tulituma.+ 18 Lakini mujiepushe na kitu chenye kinapaswa kuharibiwa,+ ili musitamani kitu chenye kinapaswa kuharibiwa na kukikamata,+ musifanye kambi ya Israeli kuwa kitu chenye kinapaswa kuharibiwa kwa kuleta musiba* juu yake.+ 19 Lakini feza yote na zahabu na vyombo vya shaba na chuma ni vitu vitakatifu kwa Yehova.+ Vinapaswa kuwekwa katika hazina ya Yehova.”+
20 Basi wakati baragumu zilipigwa, watu wakafanya makelele.+ Na wakati tu watu walisikia sauti ya baragumu na kufanya makelele makubwa ya vita, ukuta ukaanguka chini.+ Kisha watu wakapanda na kuingia katika muji, kila mutu akaingia moja kwa moja, na wakakamata muji. 21 Wakaharibu kwa upanga vyote vyenye vilikuwa katika muji, wanaume na wanamuke, vijana na wazee, ngombe-dume, kondoo, na punda.+
22 Yoshua akaambia wale wanaume wawili wenye walipeleleza inchi: “Muende katika nyumba ya ule mwanamuke kahaba, mumupeleke inje pamoja na watu wake wote, kama vile mulimuapia.”+ 23 Basi wale vijana wapelelezi wakaenda na wakamutosha Rahabu inje, pamoja na baba yake, mama yake, ndugu zake, na watu wake wote; ndiyo, wakatosha inje familia yake yote,+ na wakawapeleka kwa usalama mahali fulani inje ya kambi ya Israeli.
24 Kisha wakateketeza muji kwa moto na kila kitu chenye kilikuwa ndani. Lakini feza, zahabu, vyombo vya shaba na chuma, wakaviweka katika hazina ya nyumba ya Yehova.+ 25 Rahabu tu ule kahaba, na nyumba ya baba yake na watu wake wote ndio Yoshua hakuharibu;+ na Rahabu anaishi katika Israeli mupaka leo,+ kwa sababu alificha wajumbe wenye Yoshua alituma kupeleleza Yeriko.+
26 Wakati huo Yoshua akatangaza kiapo* hiki: “Alaaniwe mbele ya Yehova mutu mwenye atajaribu kujenga tena muji huu wa Yeriko. Kwa kufiwa na muzaliwa wake wa kwanza atajenga musingi wake, na kwa kufiwa na mwana wake mudogo zaidi ataweka milango yake.”+
27 Basi Yehova alikuwa pamoja na Yoshua,+ na sifa za Yoshua zikaenea katika dunia yote.+