Isaya
29 “Ole wake Arieli,* Arieli, muji kwenye Daudi alipiga kambi!+
Endelea mwaka kwa mwaka;
Muzunguko wa sikukuu+ uendelee.
2 Lakini nitaleta taabu juu ya Arieli,+
Na kutakuwa kilio na maombolezo,+
Na atakuwa kwangu kama jiko la mazabahu ya Mungu.+
3 Nitapiga kambi pande zote juu yako,
Na nitakuzunguka kwa ajili ya vita kupitia lupango ya miti
Na kusimamisha juu yako vitu vya kutumia ili kuzunguka kwa ajili ya vita.+
4 Utashushwa;
Utazungumuza ukiwa katika udongo,
Na mavumbi yatafanya mambo yenye utasema yasisikike muzuri.
Sauti yako itatoka katika udongo+
Kama sauti ya mutu mwenye kupashana habari na pepo wachafu,
Na maneno yako yatatoka katika mavumbi kama sauti ya ndege.
5 Kikundi cha maadui* wako kitakuwa kama unga laini,+
Kikundi cha watu wenye kuonea kama vile maganda ya mbegu yenye kupeperuka.+
Na itatokea mara moja, bila kutazamia.+
6 Yehova wa majeshi atawakazia uangalifu
Kwa mungurumo na tetemeko la inchi na makelele makubwa,
Kwa upepo wa zoruba na zoruba kali na miali ya moto wenye kuteketeza.”+
7 Kisha kikundi cha watu wa mataifa yote yenye kupigana vita na Arieli,+
—Wale wote wenye kupigana vita naye,
Minara ya kumuzunguka kwa ajili ya vita
Na wale wenye kumuletea taabu—
Watakuwa kama ndoto, maono ya usiku.
8 Ndiyo, itakuwa kama vile wakati mutu mwenye njaa anaota ndoto kwamba anakula,
Lakini anaamuka akiwa na njaa,*
Na kama vile wakati mutu mwenye kiu anaota ndoto kwamba anakunywa,
Lakini anaamuka akiwa amechoka na akiwa na kiu.*
Ni vile itakuwa kwa kikundi cha watu wa mataifa yote
Yenye kupigana vita na Mulima Sayuni.+
Wamelewa, lakini haiko kwa sababu ya divai;
Wanayumba-yumba, lakini haiko kwa sababu ya pombe.
10 Kwa maana Yehova amemwanga juu yenu roho ya usingizi muzito;+
Na amefunga macho yenu, manabii,+
Na amefunika vichwa vyenu, waonaji.+
11 Maono yote yamekuwa kwenu kama maneno ya kitabu chenye kimefungwa kwa muhuri.+ Wakati wanakipatia mutu mwenye anajua kusoma, na kusema: “Tafazali, soma kitabu hiki kwa sauti,” atasema: “Siwezi, kwa maana kimefungwa kwa muhuri.” 12 Na wakati wanamupatia kile kitabu mutu mwenye hajue kusoma, na kusema: “Tafazali, soma kitabu hiki kwa sauti,” atasema: “Sijue kusoma hata kidogo.”
13 Yehova anasema: “Watu hawa wananikaribia kwa vinywa vyao,
Na wananiheshimia kwa midomo yao,+
Lakini moyo wao uko mbali sana na mimi,
Na wananiogopa kwa kutegemea amri za wanadamu zenye wamefundishwa.+
14 Kwa hiyo, mimi ndiye nitatendea tena watu hawa mambo ya ajabu,+
Kwa jambo la ajabu juu ya jambo la ajabu;
Na hekima ya watu wao wenye hekima itaangamia,
Na uelewaji wa watu wao wenye busara utafichwa.”+
15 Ole wao wale wenye wanafanya yao yote ili kumuficha Yehova mipango yao.*+
Matendo yao yanafanywa mahali kwenye giza,
Wakati huohuo wanasema: “Ni nani anatuona?
Ni nani anajua habari juu yetu?”+
Je, mufinyanzi* anapaswa kuonwa kuwa sawa na udongo?+
Je, kitu chenye kilitengenezwa kinapaswa kusema kuhusu ule mwenye alikitengeneza:
“Hakunitengeneza”?+
Na je, kitu chenye kilitengenezwa kitasema hivi kuhusu ule mwenye alikitengeneza:
“Hana uelewaji”?+
17 Kwa wakati mufupi tu Lebanoni itageuzwa kuwa shamba la matunda,+
Na shamba hilo la matunda litaonwa kuwa pori.+
18 Siku hiyo viziwi watasikia maneno ya kitabu,
Na kutoka katika weusi na giza macho ya vipofu yataona.+
19 Wapole watashangilia sana katika Yehova,
Na maskini kati ya watu watafurahi katika Mutakatifu wa Israeli.+
20 Kwa maana mutu mwenye kuonea hatakuwa tena,
Mwenye kujisifu atafikia mwisho wake,
Na wale wote wenye kukaa macho ili kuumiza wengine wataharibiwa,+
21 Wale wenye kwa neno la uongo wanafanya wengine wakuwe na hatia,
Wenye wanatega mutego kwa ajili ya ule muteteaji* kwenye mulango mukubwa wa muji,+
Na wale wenye wanaima haki mwenye haki kwa kutumia sababu zenye hazina musingi.+
22 Basi Yehova, mwenye alimukomboa Abrahamu,+ anaambia nyumba ya Yakobo hivi:
23 Kwa maana wakati ataona watoto wake,
Wenye ni kazi ya mikono yake, katikati yake,+
Watatakasa jina langu;
Ndiyo, watamutakasa Mutakatifu wa Yakobo,
Na watamuogopa sana Mungu wa Israeli.+
24 Wale wenye kupotoka katika roho watapata uelewaji,
Na wale wenye kunungunika watakubali mafundisho.”