Waamuzi
10 Kisha Abimeleki, Tola mwana wa Pua, mwana wa Dodo, mwanaume wa Isakari, akatokea ili kuokoa Israeli.+ Aliishi Shamiri katika eneo lenye milima la Efraimu. 2 Alihukumu Israeli kwa miaka makumi mbili na tatu (23). Kisha akakufa na kuzikwa kule Shamiri.
3 Kisha yeye kukatokea Yairi Mugileadi, na akahukumu Israeli kwa miaka makumi mbili na mbili (22). 4 Yairi alikuwa na wana makumi tatu (30) wenye kupanda juu ya punda makumi tatu, na walikuwa na miji makumi tatu yenye mupaka leo inaitwa Hawot-yairi,+ iko katika inchi ya Gileadi. 5 Kisha Yairi akakufa na kuzikwa kule Kamoni.
6 Waisraeli wakafanya tena mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova,+ na wakaanza kutumikia Mabaali,+ sanamu za Ashtoreti, miungu ya Aramu,* miungu ya Sidoni, miungu ya Moabu,+ miungu ya Waamoni,+ na miungu ya Wafilisti.+ Wakamuacha Yehova na hawakumutumikia. 7 Basi kasirani ya Yehova ikawaka juu ya Israeli, na akawauzisha katika mikono ya Wafilisti na Waamoni.+ 8 Kwa hiyo wakavunja-vunja na kukandamiza sana Waisraeli katika mwaka huo—kwa miaka kumi na munane (18) walikandamiza Waisraeli wote wenye walikuwa ngambo ya Yordani yenye ilikuwa inchi ya Waamori katika Gileadi. 9 Waamoni pia walikuwa wanavuka Yordani ili kupigana na Yuda, Benyamini, na nyumba ya Efraimu; na Israeli walikuwa katika taabu kubwa sana. 10 Kisha Waisraeli wakamulilia Yehova awasaidie,+ wakisema: “Tumekutendea zambi, kwa maana tumeacha Mungu wetu na tumetumikia Mabaali.”+
11 Lakini Yehova akaambia Waisraeli: “Je, sikuwaokoa kutoka Misri+ na kutoka kwa Waamori,+ Waamoni, Wafilisti,+ 12 Wasidoni, Waamaleki, na Wamidiani wakati walikuwa wanawakandamiza? Wakati mulinililia, niliwaokoa katika mukono wao. 13 Lakini muliniacha na kutumikia miungu mingine.+ Ndiyo sababu sitawaokoa tena.+ 14 Muende kwa miungu yenye mulichagua na muililie iwasaidie.+ Iwaokoe wakati wa taabu.”+ 15 Lakini Waisraeli wakamuambia Yehova: “Tumetenda zambi. Ututendee kitu chochote chenye utaona kuwa kizuri mbele ya macho yako. Lakini tafazali, utuokoe leo hii.” 16 Basi wakaondoa katikati yao miungu ya kigeni na wakamutumikia Yehova,+ kwa hiyo hakuweza tena kuvumilia* kuona Israeli wakiteseka.+
17 Kisha wakati fulani Waamoni+ wakakusanywa pamoja, na wakapiga kambi katika Gileadi. Kwa hiyo Waisraeli wakakusanyika pamoja na wakapiga kambi katika Mispa. 18 Watu wa Gileadi na wakubwa wao wakaulizana: “Ni nani ataongoza ili kupigana na Waamoni?+ Akuwe mukubwa juu ya wakaaji wote wa Gileadi.”