Zaburi
Wimbo wa Safari za Kupanda.
130 Ninakuita nikiwa katika sehemu za chini kabisa, Ee Yehova.+
2 Ee Yehova, sikia sauti yangu.
Masikio yako yasikilize vilio vyangu vya kuomba musaada.
5 Ninamutumainia Yehova, nafsi yangu yote inamutumainia;
Ninangojea neno lake.
6 Ninamungojea* Yehova kwa hamu,+
Kuliko namna walinzi wanangojea asubui,+
Ndiyo, kuliko namna walinzi wanangojea asubui.
7 Israeli aendelee kumungojea Yehova,
Kwa maana Yehova ni mushikamanifu katika upendo wake,+
Na iko* na nguvu nyingi za kukomboa.
8 Atakomboa Israeli katika makosa yao yote.