Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 28
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Ezekieli

      • Unabii juu ya mufalme wa Tiro (1-10)

        • “Mimi ni mungu” (2, 9)

      • Wimbo wa huzuni kuhusu mufalme wa Tiro (11-19)

        • “Ulikuwa katika Edeni” (13)

        • “Kerubi mwenye kutiwa mafuta mwenye anafunika” (14)

        • ‘Ukosefu wa haki ulipatikana ndani yako’ (15)

      • Unabii juu ya Sidoni (20-24)

      • Israeli watarudishwa (25, 26)

Ezekieli 28:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 28:5
  • +Eze 27:4

Ezekieli 28:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Da. 2:48

Ezekieli 28:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zek 9:3

Ezekieli 28:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 23:1, 3; Eze 27:12

Ezekieli 28:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 30:10, 11
  • +Isa 23:9

Ezekieli 28:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kaburi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 27:26

Ezekieli 28:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wimbo wa maombolezo.”

  • *

    Tnn., “Ulifunga mufano kwa muhuri.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 28:3
  • +Eze 27:3

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/10/2005, uku. 23-24

Ezekieli 28:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 27:16

Ezekieli 28:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 14:13

Ezekieli 28:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yoe 3:4; Amo 1:9

Ezekieli 28:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 10:11; 2Nya 9:21; Eze 27:12
  • +Yoe 3:6
  • +Isa 23:9; Yer 25:17, 22; 47:4; Yoe 3:8

Ezekieli 28:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 27:3
  • +Isa 14:14
  • +Isa 14:15

Ezekieli 28:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amo 1:9, 10

Ezekieli 28:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 27:35
  • +Eze 27:36

Ezekieli 28:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 23:4; Yer 25:17, 22; Eze 32:30

Ezekieli 28:23

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 26:6

Ezekieli 28:24

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 33:55; Yosh. 23:12, 13

Ezekieli 28:25

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 30:3; Isa 11:12; Yer 30:18; Ho 1:11
  • +Isa 5:16
  • +Yer 23:8
  • +Mwa 28:13

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    “Kila Andiko,” uku. 137

Ezekieli 28:26

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 32:18; Yer 23:6; Ho 2:18
  • +Isa 65:21, 22; Yer 31:5; Amo 9:14
  • +Yer 30:16

Maandiko ingine

Eze. 28:2Eze 28:5
Eze. 28:2Eze 27:4
Eze. 28:3Da. 2:48
Eze. 28:4Zek 9:3
Eze. 28:5Isa 23:1, 3; Eze 27:12
Eze. 28:7Eze 30:10, 11
Eze. 28:7Isa 23:9
Eze. 28:8Eze 27:26
Eze. 28:12Eze 28:3
Eze. 28:12Eze 27:3
Eze. 28:13Eze 27:16
Eze. 28:14Isa 14:13
Eze. 28:15Yoe 3:4; Amo 1:9
Eze. 28:161 Fal. 10:11; 2Nya 9:21; Eze 27:12
Eze. 28:16Yoe 3:6
Eze. 28:16Isa 23:9; Yer 25:17, 22; 47:4; Yoe 3:8
Eze. 28:17Eze 27:3
Eze. 28:17Isa 14:14
Eze. 28:17Isa 14:15
Eze. 28:18Amo 1:9, 10
Eze. 28:19Eze 27:35
Eze. 28:19Eze 27:36
Eze. 28:21Isa 23:4; Yer 25:17, 22; Eze 32:30
Eze. 28:23Eze 26:6
Eze. 28:24Hes 33:55; Yosh. 23:12, 13
Eze. 28:25Kum 30:3; Isa 11:12; Yer 30:18; Ho 1:11
Eze. 28:25Isa 5:16
Eze. 28:25Yer 23:8
Eze. 28:25Mwa 28:13
Eze. 28:26Isa 32:18; Yer 23:6; Ho 2:18
Eze. 28:26Isa 65:21, 22; Yer 31:5; Amo 9:14
Eze. 28:26Yer 30:16
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Ezekieli 28:1-26

Ezekieli

28 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, ambia kiongozi wa Tiro, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:

“Kwa sababu moyo wako umekuwa na majivuno,+ unaendelea kusema, ‘Mimi ni mungu.

Ninakaa kwenye kiti cha ufalme cha mungu katika moyo wa bahari.’+

Lakini wewe ni mwanadamu tu, hauko mungu,

Hata kama katika moyo wako unajiona kuwa mungu.

 3 Angalia! Uko na hekima kuliko Danieli.+

Haujafichwa siri yoyote.

 4 Umejifanya kuwa tajiri kwa hekima yako na utambuzi wako,

Na unaendelea kukusanya zahabu na feza katika hazina zako.+

 5 Ufundi wako katika biashara ulikuletea utajiri mwingi,+

Na moyo wako ukakuwa na majivuno kwa sababu ya utajiri wako.”’

6 “‘Kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:

“Kwa sababu katika moyo wako unajiona kuwa mungu,

 7 Ninaleta wageni juu yako, wenye hawana huruma kabisa kati ya mataifa,+

Nao watachomoa panga zao ili kushambulia uzuri wa hekima yako

Nao watachafua utukufu wako mukubwa.+

 8 Watakushusha katika shimo,*

Na utakufa kifo cha jeuri katika moyo wa bahari kubwa.+

 9 Je, bado utamuambia ule mwenye kukuua, ‘Mimi ni mungu?’

Utakuwa mwanadamu bure, hapana mungu, katika mukono wa wale wenye kukuchafua.”’

10 ‘Kwa mukono wa wageni, utakufa kifo cha watu wenye hawatahiriwe,

Kwa maana mimi mwenyewe nimesema,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”

11 Na neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 12 “Mwana wa binadamu, imba wimbo wa huzuni* kuhusu mufalme wa Tiro, na umuambie, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:

“Ulikuwa mufano wa ukamilifu,*

Ulijaa hekima+ na ulikuwa na uzuri mukamilifu.+

13 Ulikuwa katika Edeni, bustani ya Mungu.

Ulipambwa kwa kila jiwe lenye samani

⁠—​Zabarijadi, topazi, na yaspi;

krisolito, shohamu, na yashefi; yakuti, feruzi,+ na zumaridi;

Na vikalio na vishikio vya majiwe hayo vilikuwa vya zahabu.

Vilitayarishwa siku yenye uliumbwa.

14 Nilikuweka kuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta mwenye anafunika.

Ulikuwa kwenye mulima mutakatifu wa Mungu,+ na ulitembea kati ya majiwe yenye moto.

15 Haukukuwa na kosa katika njia zako tangu siku uliumbwa

Mupaka wakati ukosefu wa haki ulipatikana ndani yako.+

16 Kwa sababu ya biashara yako nyingi,+

Ulijaa jeuri, na ulianza kutenda zambi.+

Kwa hiyo nitakufukuza kama kitu kichafu kutoka kwenye mulima wa Mungu na kukuharibu,+

Ee kerubi mwenye kufunika, mbali na majiwe ya moto.

17 Moyo wako ukakuwa na majivuno kwa sababu ya uzuri wako.+

Ulipotosha hekima yako kwa sababu ya utukufu wako mukubwa.+

Nitakutupa chini kwenye dunia.+

Nitakufanya kuwa kitu cha kutazamwa na wafalme.

18 Kwa sababu ya hatia yako kubwa na ukosefu wako wa haki katika biashara, umechafua mahali pako patakatifu.

Nitatokeza moto katikati yako, nao utakuteketeza.+

Nitakufanya kuwa majivu juu ya dunia mbele ya wote wenye kukuangalia.

19 Wale wote wenye walikujua kati ya vikundi vya watu watakuangalia kwa mushangao.+

Mwisho wako utafika kwa kushitukia na utakuwa mubaya,

Na wewe hautakuwa tena kwa wakati wote.”’”+

20 Na neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 21 “Mwana wa binadamu, elekeza uso wako Sidoni,+ na utoe unabii juu yake. 22 Utasema, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:

“Angalia, nitapigana na wewe, Ee Sidoni, na nitatukuzwa katikati yako;

Na watu watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova wakati nitaleta hukumu juu yake na kutakaswa ndani yake.

23 Nitatuma ugonjwa wa kuambukiza ndani yake na damu itateremuka katika barabara zake.

Wenye kuuawa wataanguka katikati yake wakati upanga utakuja juu yake kutoka pande zote;

Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+

24 “‘“Halafu nyumba ya Israeli haitazungukwa tena na michongoma yenye kuumiza na miiba yenye kuleta maumivu,+ wale wenye kuwatendea kwa zarau; na watu watalazimika kujua kwamba mimi ni Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova.”’

25 “‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Wakati nitakusanya tena nyumba ya Israeli kutoka katika vikundi vya watu kwenye walisambazwa,+ nitatakaswa kati yao mbele ya macho ya mataifa.+ Nao watakaa katika inchi yao+ yenye nilimupatia mutumishi wangu Yakobo.+ 26 Wataishi katika inchi hiyo kwa usalama+ na watajenga nyumba na kupanda mashamba ya mizabibu,+ na watakaa kwa usalama wakati nitaleta hukumu juu ya wale wote wenye kuwazunguka wenye wanawatendea kwa zarau;+ na watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova Mungu wao.”’”

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine