Mezali
14 Mwanamuke mwenye hekima kabisa anajenga nyumba yake,+
Lakini mwanamuke mupumbavu anaibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2 Mutu mwenye kutembea katika unyoofu wake anamuogopa Yehova,
Lakini ule mwenye njia zake ni za udanganyifu* anamuzarau Yeye.
3 Fimbo ya kiburi iko katika kinywa cha mupumbavu,
Lakini midomo ya wenye hekima itawalinda.
4 Kwenye hakuna ngombe, chombo cha kukulishia wanyama kiko safi,
Lakini nguvu za ngombe-dume zinaleta mavuno mengi.
6 Mutu mwenye kuchekelea wengine anatafuta hekima lakini haipate hata kidogo,
Lakini ujuzi unakuja kwa urahisi kwa mutu mwenye uelewaji.+
8 Kwa hekima, mutu mwerevu anaelewa njia yenye anafuata,
10 Moyo unajua uchungu wake mwenyewe,*
Na hakuna mutu wa inje mwenye anaweza kushiriki katika furaha yake.
12 Kuko njia yenye inaonekana kuwa sawa mbele ya macho ya mutu,+
Lakini mwishowe inaongoza kwenye kifo.+
13 Hata katika kicheko moyo unaweza kusikia maumivu,
Na shangwe inaweza kuishia katika huzuni.
14 Mutu mwenye kupotoka katika moyo atavuna matokeo ya njia zake,+
Lakini mutu muzuri anavuna zawabu ya matendo yake.+
17 Mutu mwenye kukasirika haraka anatenda kwa ujinga,+
Lakini mutu mwenye kufikiri sana juu ya mambo* anachukiwa.
19 Watu wabaya watalazimika kuinama mbele ya watu wema,
Na waovu watainama kwenye milango mikubwa ya wenye haki.
21 Mwenye anazarau jirani yake anatenda zambi,
Lakini mutu yeyote mwenye anaonyesha huruma watu wa hali ya chini ni mwenye furaha.+
22 Je, wale wenye kufanya mipango mibaya hawatapotea njia?
Lakini wale wenye nia ya kutenda mema watapata upendo mushikamanifu na uaminifu.+
27 Kumuogopa Yehova ni chemchemi ya uzima,
Ili kuepusha mutu na mitego ya kifo.
29 Mutu mwenye hakasirike haraka iko* na utambuzi mwingi,+
Lakini mwenye hana uvumilivu anaonyesha upumbavu wake.+
31 Mwenye anapunja mutu wa hali ya chini anatukana Mutengenezaji wake,+
Lakini mutu yeyote mwenye anasikilia maskini huruma anamutukuza Mungu.+
32 Uovu wa muovu utamushusha chini,
Lakini mwenye haki atapata kimbilio katika uaminifu-mushikamanifu wake.+