Mezali
4 Ambia hekima, “Wewe ni dada yangu,”
Na uite uelewaji “mutu wa jamaa yangu,”
6 Nikiwa kwenye dirisha la nyumba yangu,
Niliangalia chini kupitia kayungio ya dirisha langu,
7 Na wakati nilikuwa ninachunguza wajinga,*
Nilitambua kati ya vijana, kijana mumoja mwanaume mwenye kukosa akili ya muzuri.*+
8 Alipita katika barabara karibu na makutano ya barabara katika njia yenye kupeleka kwa mwanamuke huyo
Na alishika njia ya kuenda kwenye nyumba ya mwanamuke huyo
9 Mangaribi, wakati giza linaanza,+
Wakati usiku na giza vinaingia.
11 Ni mwenye makelele na iko* kichwa-nguvu.+
Habakiake* katika nyumba yake.
12 Wakati fulani iko* inje, wakati mwingine iko* katika viwanja vya watu wote,
Anajificha karibu na kila makutano ya barabara.+
13 Kisha anamukamata kwa nguvu kijana huyo na kumupatia busu;
Bila haya, mwanamuke huyo anamuambia:
14 “Nilipaswa kutoa zabihu za ushirika.+
Leo nilitimiza naziri zangu.
15 Ndiyo sababu nimekuja kukutana na wewe,
Kukutafuta, na nimekupata!
17 Nimenyunyiza* manemane, udi, na mudalasini juu ya kitanda changu.+
18 Kuja, tukunywe na kushiba upendo mupaka asubui;
Na tujifurahishe pamoja kwa mapendo,
19 Kwa maana bwana yangu haiko nyumbani;
Ameenda safari ya mbali.
20 Alibeba mufuko wa feza,
Na hatarudia mupaka siku ya mwezi wenye kuenea.”
21 Anamupotosha kwa ushawishi mukubwa.+
Anamutongoza kwa maneno laini.
22 Mara moja kijana huyo anamufuata, kama ngombe-dume mwenye anaenda kuchinjwa,
Kama mupumbavu mwenye anaenda kupewa azabu katika mikatale,*+
23 Mupaka wakati mushale unatoboa maini yake;
Kama ndege mwenye anakimbia kuingia katika mutego, hajue kwamba hilo litamufanya apoteze uzima wake.*+
24 Na sasa, wana wangu, munisikilize;
Musikilize kwa uangalifu maneno yenye ninasema.
25 Musiruhusu moyo wenu ugeuke na kufuata njia zake.
Musipotee njia na kufuata njia zake,+
26 Kwa maana amefanya wengi waanguke wakiwa wameuawa,+
Na wale wenye ameua ni wengi sana.+
27 Nyumba yake inaongoza katika Kaburi;*
Inashuka chini kwenye vyumba vya ndani vya kifo.