Maombolezo
א [Aleph]
2 Namna Yehova amefunika binti ya Sayuni katika wingu la kasirani yake!
Ametupa chini uzuri wa Israeli kutoka mbinguni mupaka duniani.+
Hakukumbuka kiti cha miguu yake+ katika siku ya kasirani yake.
ב [Beth]
2 Yehova amemeza bila huruma makao yote ya Yakobo.
Katika kasirani yake amebomoa ngome za binti ya Yuda.+
Ameangusha chini na kuchafua ufalme+ na wakubwa wake.+
ג [Gimel]
3 Katika joto kali la kasirani amekata nguvu zote* za Israeli.
Alirudisha mukono wake wa kuume wakati adui alikaribia,+
Na katika Yakobo aliendelea kuwaka kama moto wenye unateketeza kila kitu kuuzunguka.+
ד [Daleth]
4 Amekunja* upinde wake kama adui; na kama mupinzani, ametayarisha mukono wake wa kuume ili kushambulia;+
Aliendelea kuua wote wenye kupendeza macho.+
Na amemwanga kasirani yake kali kama moto+ katika hema ya binti ya Sayuni.+
ה [He]
5 Yehova amekuwa kama adui;+
Amemeza Israeli.
Amemeza minara yake yote;
Ameharibu mahali pake pote penye ngome.
Na katika binti ya Yuda anafanya kilio na maombolezo viongezeke.
ו [Waw]
6 Anatendea kibanda chake kwa jeuri,+ kama kibanda chenye kuwa katika bustani.
Yehova amefanya sikukuu na sabato zisahauliwe katika Sayuni,
Na katika kasirani yake kali haheshimie mufalme na kuhani.+
ז [Zayin]
7 Yehova amekataa mazabahu yake;
Amekataa patakatifu pake.+
Ametoa kuta za minara yake yenye ngome katika mukono wa adui.+
Wamepandisha sauti yao katika nyumba ya Yehova,+ kama katika siku ya sikukuu.
ח [Heth]
8 Yehova ameazimia kuharibu ukuta wa binti ya Sayuni.+
Amenyoosha kamba ya kupimia.+
Hakurudisha mukono wake nyuma ili asilete uharibifu.*
Na anafanya boma na ukuta viomboleze.
Vyote pamoja vimeregezwa.
ט [Teth]
9 Milango yake mikubwa imezama katika udongo.+
Ameharibu na kuvunja mapingo* yake.
Mufalme wake na wakubwa wake wako kati ya mataifa.+
Hakuna sheria;* hata manabii wake hawapate maono kutoka kwa Yehova.+
י [Yod]
10 Wazee wa binti ya Sayuni wamekaa chini kimya.+
Wanatupa mavumbi kwenye vichwa vyao na kuvaa nguo za magunia.+
Mabikira wa Yerusalemu wameinamisha vichwa vyao mupaka chini.
כ [Kaph]
11 Macho yangu yamechoka kwa sababu ya kutoa machozi.+
Sehemu zangu za ndani zinavurugika.*
Ini langu limemwangwa chini kwa sababu ya kuangamizwa kwa binti* ya watu wangu,+
Kwa sababu watoto na watoto wadogo wanazimia katika viwanja vya watu wote vya muji.+
ל [Lamed]
12 Wanaendelea kuuliza mama zao: “Nafaka na divai viko wapi?”+
Wakati wanazimia kama mutu mwenye aliumizwa katika viwanja vya watu wote vya muji,
Wakati uzima wao unapotea* katika mikono ya mama zao.
מ [Mem]
13 Ninaweza kutumia nini kama shahidi,
Ao ninaweza kukufananisha na nini, Ee binti ya Yerusalemu?
Ninaweza kukulinganisha na nini, ili kukufariji, Ee binti bikira wa Sayuni?
Kwa maana muvunjiko wako ni mukubwa kama bahari.+ Ni nani anaweza kukuponyesha?+
נ [Nun]
14 Maono yenye manabii wako waliona kwa ajili yako yalikuwa ya uongo na yenye hayana maana,+
Na hawakufunua kosa lako ili usipelekwe katika utekwa,+
Lakini waliendelea kuona kwa ajili yako maono ya matangazo ya uongo na yenye kupotosha.+
ס [Samekh]
15 Wale wote wenye kupita katika barabara wanapiga mikono ili kukuchekelea.+
Wanapiga muluzi kwa mushangao+ na kutikisa vichwa vyao juu ya binti ya Yerusalemu, na kusema:
“Je, huu ndio muji wenye walikuwa wanasema juu yake, ‘Unakamilika katika uzuri, furaha ya dunia yote’?”+
פ [Pe]
16 Maadui wako wote wamefungua kinywa chao juu yako.
Wanapiga muluzi na kusaga meno yao na kusema: “Tumemumeza.+
Hii ndiyo siku yenye tulikuwa tunangojea!+ Imefika, na tumeiona!”+
ע [Ayin]
Amebomoa bila huruma.+
Amefanya adui afurahi juu yako; ameinua nguvu* za wapinzani wako.
צ [Tsade]
18 Moyo wao unamulilia Yehova, Ee ukuta wa binti ya Sayuni.
Acha machozi yatiririke kama muto mudogo muchana na usiku.
Usijipatie pumuziko, usipatie jicho lako* pumuziko.
ק [Qoph]
19 Simama! Lia wakati wa usiku, kwenye mwanzo wa makesha.
Mwanga moyo wako kama maji mbele ya uso wa Yehova.
Inua mikono yako kwake kwa ajili ya uzima* wa watoto wako,
Wenye wanazimia kwenye kila pembe* ya barabara kwa sababu ya njaa.+
ר [Resh]
20 Ona, Ee Yehova, na uangalie ule mwenye ulitendea kwa ukali hivi.
Je, wanamuke waendelee kula uzao wao* wenyewe, watoto wao wenyewe wenye afya ya muzuri kabisa,+
Ao, je, makuhani na manabii wauawe katika patakatifu pa Yehova?+
ש [Shin]
21 Kijana mudogo na mwanaume muzee wamelala chini wakiwa wamekufa katika barabara.+
Mabikira wangu* na vijana wangu wanaume wameanguka kwa upanga.+
Umeua katika siku ya kasirani yako; umechinja bila huruma.+
ת [Taw]
22 Kama vile kwa ajili ya siku ya sikukuu,+ unaita woga kutoka kila mahali.