Yobu
19 Yobu akajibu:
4 Na kama kwa kweli nimefanya kosa,
Ni kosa langu mimi mwenyewe.
5 Kama munaendelea kujiinua juu yangu,
Na kuonyesha kwamba ninastahili kulaumiwa,
6 Basi, mujue kama Mungu ndiye amenidanganya,
Na kunikamata katika wavu wake wa* kuwinda.
7 Angalia! Ninaendelea kuita kwa sauti kubwa, ‘Jeuri!’ lakini sipate jibu;+
Ninaendelea kuomba musaada, lakini hakuna haki.+
8 Amefunga njia yangu kwa ukuta wa majiwe, na siwezi kupita;
Amefunika njia zangu kwa giza.+
9 Ameondoa utukufu wangu
Na kuvua taji juu ya kichwa changu.
10 Amenibomoa kila upande mupaka niangamie;
Anangoa tumaini langu kama muti.
11 Kasirani yake inawaka juu yangu,
Na ananiona kuwa adui yake.+
12 Majeshi yake yanakuja pamoja na kunizunguka kwa ajili ya vita,
Na yanapiga kambi kuzunguka hema yangu.
13 Amefukuza ndugu zangu mbali na mimi,
Na wale wenye kunijua wamegeuka na kuniacha.+
15 Wageni katika nyumba yangu+ na watumishi wangu wanamuke wananiona kama mugeni;
Nimekuwa mugeni mbele ya macho yao.
16 Ninamuita mutumishi wangu, lakini hajibu;
Ninamulilia kwa kinywa changu ili anisikilie huruma.
18 Hata watoto wadogo wananizarau;
Wakati ninasimama, wanaanza kunicheka.
20 Mifupa yangu inakamatana na ngozi na nyama ya mwili wangu,+
Na nimeponyoka na ngozi ya meno yangu.
21 Munionyeshe rehema, marafiki wangu, munionyeshe rehema,
Kwa maana mukono wa Mungu mwenyewe umenigusa.+
23 Ingekuwa muzuri kama maneno yangu yangeandikwa,
Kama yangeandikwa katika kitabu!
24 Kama tu yangeandikwa milele katika mwamba,
Kwa kalamu ya chuma na risasi!
25 Kwa maana ninajua muzuri kwamba mukombozi wangu+ anaishi;
Kisha wakati fulani atakuja na kusimama juu ya dunia.*
26 Kisha ngozi yangu kuharibiwa hivi,
Wakati ningali katika mwili wangu, nitamuona Mungu,
27 Mimi mwenyewe nitamuona,
Macho yangu mwenyewe yatamuona, hapana macho ya mutu mwingine.+
Lakini ndani yangu kabisa ninajisikia mwenye kulemewa!*
28 Kwa maana munasema, ‘Tunamutesa namna gani?’+
Kwa kuwa mimi ndiye chanzo cha lile tatizo.