Danieli
10 Katika mwaka wa tatu (3) wa utawala wa Koreshi+ mufalme wa Uajemi, ufunuo ulitolewa kwa Danieli, mwenye aliitwa kwa jina Belteshaza;+ na ujumbe ulikuwa wa kweli, na ulihusu ugomvi mukubwa. Na akaelewa ujumbe huo na akapewa uelewaji juu ya mambo yenye alikuwa ameona.
2 Katika siku hizo, mimi Danieli, nilikuwa nimeomboleza+ kwa majuma tatu (3) kamili. 3 Sikukula chakula kizuri, na hakuna nyama wala divai yenye iliingia katika kinywa changu, na sikujipakaa mafuta kwa majuma tatu (3) kamili. 4 Katika siku ya makumi mbili na ine (24) ya mwezi wa kwanza, wakati nilikuwa pembeni ya ule muto mukubwa, Tigri,*+ 5 niliinua macho na nikaona mwanaume mwenye kuvaa nguo ya kitani,+ na kuzunguka kiuno chake kulikuwa mukaba* wa zahabu ya Ufazi. 6 Mwili wake ulikuwa kama krisolito,+ uso wake ulikuwa kama umeme wa radi, macho yake yalikuwa kama mienge yenye kuwaka moto, mikono yake na miguu yake ilionekana kama shaba yenye kungarishwa,+ na sauti ya maneno yake ilikuwa kama sauti ya watu wengi. 7 Mimi tu, Danieli, ndiye niliona maono hayo; watu wenye walikuwa pamoja na mimi hawakuona maono hayo.+ Lakini walishikwa na mutetemeko mukubwa, na wakakimbia na kujificha.
8 Kisha niliachwa peke yangu, na wakati niliona maono hayo makubwa, hakuna nguvu zenye zilibakia ndani yangu na sura yangu yenye kuheshimika ikaniacha na nguvu zote zikanitoka.+ 9 Kisha nikasikia sauti yake akisema; lakini wakati nilimusikia akisema, nilipatwa na usingizi muzito nikiwa nimelala uso chini.+ 10 Lakini kisha pale mukono ukanigusa,+ na ukanitikisa ili niinuke kwa mikono na magoti yangu. 11 Kisha akaniambia:
“Ee Danieli, wewe mutu mwenye samani sana,*+ kaza uangalifu juu ya maneno yenye ninataka kukuambia. Sasa, simama mahali pako, kwa maana nimetumwa kwako.”
Wakati aliniambia vile, nikasimama, nilikuwa ninatetemeka.
12 Kisha akaniambia: “Usiogope,+ Ee Danieli. Maneno yako yalisikiwa tangu siku ya kwanza yenye ulielekeza moyo wako kwenye uelewaji na kujinyenyekeza mbele ya Mungu wako, na nimekuja kwa sababu ya maneno yako.+ 13 Lakini mukubwa+ wa ufalme wa Uajemi alisimama ili kunipinga kwa siku makumi mbili na moja (21). Lakini kisha pale Mikaeli,*+ mumoja kati ya wakubwa wa mbele,* alikuja kunisaidia; na nilibakia pale karibu na wafalme wa Uajemi. 14 Nimekuja ili kukufanya uelewe mambo yenye yatapata watu wako katika kipindi cha mwisho cha zile siku,+ kwa sababu hayo bado ni maono kwa ajili ya siku zenye zitakuja.”+
15 Sasa wakati aliniambia maneno hayo, niliinamisha uso wangu chini na nikakuwa bubu. 16 Kisha mumoja mwenye kuonekana kama mwanadamu akagusa midomo yangu,+ na nikafungua kinywa changu na kumuambia ule mwenye alikuwa amesimama mbele yangu: “Bwana wangu, ninatetemeka kwa woga kwa sababu ya maono hayo, na sina nguvu.+ 17 Basi namna gani mutumishi wa bwana wangu anaweza kusema na bwana wangu?+ Kwa maana sasa sina nguvu, na hakuna pumuzi yenye kubakia ndani yangu.”+
18 Ule mwenye kuonekana kama mwanadamu akanigusa tena na kunitia nguvu.+ 19 Kisha akasema: “Usiogope,+ Ee mutu mwenye samani sana.*+ Ukuwe na amani.+ Ukuwe na nguvu, ndiyo, ukuwe na nguvu.” Wakati alisema na mimi nilitiwa nguvu na nikasema: “Bwana wangu aseme, kwa maana umenitia nguvu.”
20 Kisha akasema: “Je, unajua sababu gani nimekuja kwako? Sasa nitarudia kupigana na mukubwa wa Uajemi.+ Wakati nitaondoka, mukubwa wa Ugiriki atakuja. 21 Hata hivyo, nitakuambia mambo yenye yameandikwa katika maandishi ya kweli. Hakuna mwenye iko* ananitegemeza kwa nguvu katika mambo haya isipokuwa Mikaeli,+ mukubwa wako.+