Zaburi
91 Mutu yeyote mwenye kukaa mahali pa siri pa Mwenye Kuwa Juu Zaidi+
Ataishi katika kivuli cha Mweza-Yote.+
3 Kwa maana atakuokoa katika mutego wa muwindaji wa ndege,
Katika ugonjwa wa kuambukiza wenye kuharibu.
Uaminifu wake+ utakuwa ngao kubwa+ na ukuta wa ulinzi.*
5 Hautaogopa mambo yenye kuogopesha sana ya usiku,+
Wala mushale wenye kuruka muchana,+
6 Wala ugonjwa wa kuambukiza wenye kuwinda kimya-kimya katika giza,
Wala uharibifu wenye kuharibu katikati ya muchana.
7 Elfu moja (1 000) wataanguka pembeni yako
Na elfu kumi (10 000) kwenye mukono wako wa kuume,
Lakini haitakukaribia wewe.+
9 Kwa sababu ulisema: “Yehova ni kimbilio langu,”
Umemufanya Mwenye Kuwa Juu Zaidi kuwa makao yako;*+
10 Hakuna musiba wenye utakufikia,+
Na hakuna pigo lenye litakaribia hema yako.
13 Utakanyanga mwana-simba na nyoka-kobra;
Utamukanyangia chini simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo na nyoka mukubwa.+
14 Mungu alisema: “Kwa sababu ananipenda,* nitamuokoa.+
Nitamulinda kwa sababu anajua* jina langu.+
Nitakuwa pamoja naye katika taabu.+
Nitamuokoa na kumutukuza.