Zaburi
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
64 Sikia sauti yangu, Ee Mungu, wakati ninakulilia.+
Linda uzima wangu kutokana na woga wa adui.
2 Unilinde kutokana na mipango mibaya yenye waovu wanafanya kwa uficho,+
Kutokana na kikundi cha wakosaji.
3 Wananoa ulimi wao kama vile upanga;
Wanalenga maneno yao makali kama mishale,
4 Ili wamupige mutu mwenye hana kosa wakiwa mahali pao pa kujificha;
Wanamupiga bila kutazamia, bila kuogopa.
5 Wanashikamana sana na kusudi lao la uovu;*
Wanazungumuzia namna ya kuficha mitego yao.
Wanasema: “Ni nani ataiona?”+
6 Wanatafuta njia za mupya za kutenda makosa;
Wanapanga kwa siri mipango yao ya ujanja;+
Mawazo yenye kuwa ndani ya moyo wa kila mumoja wao hayaeleweke kabisa.
7 Lakini Mungu atawapiga mishale;+
Bila kutazamia, wataumizwa na mushale.
8 Ulimi wao wenyewe utawafanya waanguke;+
Wale wote wenye kuangalia watatikisa kichwa.