Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati
16 Basi wakaingiza Sanduku la Mungu wa kweli na kuliweka ndani ya hema yenye Daudi alikuwa ameisimamishia;+ na wakatoa matoleo ya kuteketezwa na zabihu za ushirika mbele ya Mungu wa kweli.+ 2 Wakati Daudi alimaliza kutoa matoleo ya kuteketezwa+ na zabihu za ushirika,+ akabariki watu katika jina la Yehova. 3 Tena, aligawia Waisraeli wote, kila mwanaume na mwanamuke, mukate mumoja wa muviringo, keki ya tende, na keki ya zabibu zenye kukauka. 4 Kisha akaweka Walawi fulani wafanye utumishi mbele ya Sanduku la Yehova,+ wamuheshimie,* wamushukuru, na wamusifu Yehova Mungu wa Israeli. 5 Asafu+ alikuwa kichwa, na wa pili kisha yeye alikuwa Zekaria; na Yeieli, Shemiramoti, Yehieli, Matitia, Eliabu, Benaya, Obed-edomu, na Yeieli+ walipiga vyombo vya kamba na vinubi;+ na Asafu alipiga matoazi,+ 6 na Benaya na Yahazieli makuhani walipiga tarumbeta bila kuacha mbele ya sanduku la agano la Mungu wa kweli.
7 Hiyo ndiyo siku yenye Daudi kwa mara ya kwanza alitoa muchango wa wimbo wenye alitunga ili kumushukuru Yehova na akaupatia Asafu+ na ndugu zake:
10 Mujisifu juu ya jina lake takatifu.+
Mioyo ya wale wenye kumutafuta Yehova ishangilie.+
12 Mukumbuke kazi za ajabu zenye amefanya,+
Miujiza yake na hukumu zenye ametangaza,
13 Ninyi uzao wa* Israeli mutumishi wake,+
Ninyi wana wa Yakobo, wachaguliwa wake.+
14 Yeye ni Yehova Mungu wetu.+
Hukumu zake ziko katika dunia yote.+
15 Mukumbuke agano lake milele,
Ahadi yenye alitoa,* mupaka vizazi elfu,+
16 Agano lenye alifanya pamoja na Abrahamu,+
Na kiapo chenye alimuapia Isaka,+
17 Chenye aliweka kuwa amri kwa Yakobo+
Na kuwa agano la kudumu kwa Israeli,
18 Akisema, ‘Nitakupatia inchi ya Kanaani+
Kuwa uriti wenu wenye muligawiwa.’+
19 Ilikuwa vile wakati mulikuwa watu kidogo,
Ndiyo, kidogo sana, na mulikuwa wageni katika inchi.+
20 Walitembea-tembea kutoka taifa moja mupaka taifa lingine,
Kutoka ufalme mumoja mupaka kikundi kingine cha watu.+
21 Hakumuruhusu mutu yeyote awakandamize,+
Lakini kwa sababu yao alikaripia wafalme,+
22 Akisema, ‘Musiguse watiwa-mafuta wangu,
Na musitendee manabii wangu jambo lolote la mubaya.’+
23 Mumuimbie Yehova, dunia yote!
Mutangaze wokovu wake siku kwa siku!+
24 Mutangaze utukufu wake kati ya mataifa,
Kazi zake za ajabu kati ya vikundi vyote vya watu.
25 Kwa maana Yehova ni mukubwa na anastahili kusifiwa sana.
Ni mwenye kuogopesha sana kuliko miungu mingine yote.+
26 Miungu yote ya vikundi vya watu ni miungu yenye haina mafaa yoyote,+
Lakini Yehova ndiye alifanya mbingu.+
28 Mumupatie Yehova kile chenye anastahili, ninyi familia za vikundi vya watu,
Mumupatie Yehova kile chenye anastahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+
Mumuinamie* Yehova katika mapambo matakatifu.*+
30 Mutetemeke mbele yake, dunia yote!
Dunia* imewekwa imara kabisa; haiwezi kuhamishwa.*+
32 Bahari ingurume na vyote vyenye kuijaza;
Maeneo ya mashamba na vyote vyenye kuwa ndani yake vishangilie.
33 Wakati uleule miti ya pori ipige vigelegele vya shangwe mbele ya Yehova,
Kwa maana anakuja* kuhukumu dunia.
35 Na museme, ‘Utuokoe, Ee Mungu wa wokovu wetu,+
Utukusanye na kutuokoa kutoka kwa mataifa,
Ili tushukuru jina lako takatifu+
36 Yehova Mungu wa Israeli, asifiwe
Kwa umilele wote.’”*
Na watu wote wakasema, “Amina!”* na wakamusifu Yehova.
37 Kisha Daudi akaacha Asafu+ na ndugu zake pale mbele ya sanduku la agano la Yehova ili wafanye utumishi bila kuacha mbele ya Sanduku hilo,+ kulingana na kawaida ya kila siku.+ 38 Obed-edomu na ndugu zake, watu makumi sita na munane (68), na Obed-edomu mwana wa Yedutuni, na Hosa walikuwa walinzi wa milango mikubwa; 39 na Sadoki+ kuhani na makuhani wenzake walikuwa mbele ya tabenakulo ya Yehova mahali pa juu kule Gibeoni+ 40 ili kumutolea Yehova kwa ukawaida matoleo ya kuteketezwa kwenye mazabahu ya toleo la kuteketezwa, asubui na mangaribi, na kufanya mambo yote yenye yameandikwa katika Sheria ya Yehova yenye aliamuru Israeli.+ 41 Pamoja nao kulikuwa Hemani na Yedutuni+ na wanaume wengine wenye walichaguliwa wenye walitajwa kwa majina yao ili wamushukuru Yehova,+ kwa sababu “upendo wake mushikamanifu unadumu milele”;+ 42 na pamoja nao kulikuwa Hemani+ na Yedutuni ili wapige tarumbeta, matoazi, na vyombo vyenye vilitumiwa ili kumusifu* Mungu wa kweli; na wana wa Yedutuni+ walikuwa kwenye mulango mukubwa. 43 Kisha watu wote wakaenda kwao, na Daudi akaenda kubariki nyumba yake mwenyewe.