Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 1 Mambo ya Nyakati 16
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 1 Mambo ya Nyakati

      • Sanduku linawekwa katika hema (1-6)

      • Wimbo wa shukrani wa Daudi (7-36)

        • “Yehova amekuwa Mufalme!” (31)

      • Utumishi mbele ya Sanduku (37-43)

1 Mambo ya Nyakati 16:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 8:1; 1Nya 15:1
  • +2 Sa. 6:17-19; 1 Fal. 8:5

1 Mambo ya Nyakati 16:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 1:3
  • +Law. 3:1

1 Mambo ya Nyakati 16:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wamukumbuke.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 18:2

1 Mambo ya Nyakati 16:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 6:31, 39
  • +1Nya 15:18
  • +1Nya 15:21
  • +1Nya 15:17, 19

1 Mambo ya Nyakati 16:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 6:31, 39

1 Mambo ya Nyakati 16:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 106:1
  • +Zab 67:2; 105:1-6; Isa 12:4

1 Mambo ya Nyakati 16:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mumupigie muziki.”

  • *

    Ao pengine, “Museme.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Sa. 23:1; Efe 5:19
  • +Zab 107:43

1 Mambo ya Nyakati 16:10

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 22:32; Isa 45:25; Yer 9:24
  • +1Nya 28:9; Flp 4:4

1 Mambo ya Nyakati 16:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kuwapo kwake.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amo 5:4; Sef 2:3
  • +Zab 24:5, 6

1 Mambo ya Nyakati 16:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 111:2-4

1 Mambo ya Nyakati 16:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wazao wa.” Tnn., “mbegu ya.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 41:8
  • +Zab 135:4

1 Mambo ya Nyakati 16:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 95:7
  • +Zab 105:7-11

1 Mambo ya Nyakati 16:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Neno lenye aliamuru.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 7:9

1 Mambo ya Nyakati 16:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 15:18; 17:1, 2
  • +Mwa 26:3-5

1 Mambo ya Nyakati 16:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 28:14

1 Mambo ya Nyakati 16:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 12:7; 17:8; 35:12
  • +Kum 32:8

1 Mambo ya Nyakati 16:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 34:30; Kum 26:5; Zab 105:12-15

1 Mambo ya Nyakati 16:20

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 20:1; 46:6

1 Mambo ya Nyakati 16:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 31:7, 42
  • +Mwa 12:17; 20:3

1 Mambo ya Nyakati 16:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 20:7

1 Mambo ya Nyakati 16:23

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 40:10; 96:1-6

1 Mambo ya Nyakati 16:25

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 15:11

1 Mambo ya Nyakati 16:26

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 45:20; 1 Kor. 8:4
  • +Isa 44:24

1 Mambo ya Nyakati 16:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “heshima.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 33:26; Zab 8:1
  • +1 Tim. 1:11

1 Mambo ya Nyakati 16:28

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 68:34; 96:7-13

1 Mambo ya Nyakati 16:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Mumuabudu.”

  • *

    Ao pengine, “kwa sababu ya utukufu wa utakatifu wake.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 28:58; Ne 9:5; Zab 148:13
  • +1Nya 29:3-5; Mt 5:23
  • +Kum 26:10

1 Mambo ya Nyakati 16:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Inchi yenye kuzaa.”

  • *

    Ao “kutikiswa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 104:5; Mhu. 1:4

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    1/10/2005, uku. 10-11

1 Mambo ya Nyakati 16:31

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 97:1
  • +Ufu 19:6

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/1/2014, uku. 11

1 Mambo ya Nyakati 16:33

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “amekuja.”

1 Mambo ya Nyakati 16:34

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 5:13; Lu 18:19
  • +Zab 103:17; Yer 31:3; Omb 3:22

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/1/2002, uku. 11

1 Mambo ya Nyakati 16:35

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “tushangilie katika sifa yako.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 68:20
  • +Zab 122:4
  • +Isa 43:21

1 Mambo ya Nyakati 16:36

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Tangu milele mupaka milele.”

  • *

    Ao “Ikuwe vile!”

1 Mambo ya Nyakati 16:37

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 15:16, 17
  • +1Nya 16:4-6
  • +Kut 29:38; 2Nya 13:11; Ezr 3:4

1 Mambo ya Nyakati 16:39

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 12:28
  • +1 Fal. 3:4

1 Mambo ya Nyakati 16:40

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 29:39; 2Nya 2:4

1 Mambo ya Nyakati 16:41

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 25:1
  • +1Nya 16:4
  • +2Nya 5:13; Ezr 3:11

1 Mambo ya Nyakati 16:42

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “vyombo vya wimbo wa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 6:31, 33; 15:16, 17
  • +1Nya 25:1, 3

Maandiko ingine

1 Nya. 16:11 Fal. 8:1; 1Nya 15:1
1 Nya. 16:12 Sa. 6:17-19; 1 Fal. 8:5
1 Nya. 16:2Law. 1:3
1 Nya. 16:2Law. 3:1
1 Nya. 16:4Hes 18:2
1 Nya. 16:51Nya 6:31, 39
1 Nya. 16:51Nya 15:18
1 Nya. 16:51Nya 15:21
1 Nya. 16:51Nya 15:17, 19
1 Nya. 16:71Nya 6:31, 39
1 Nya. 16:8Zab 106:1
1 Nya. 16:8Zab 67:2; 105:1-6; Isa 12:4
1 Nya. 16:92 Sa. 23:1; Efe 5:19
1 Nya. 16:9Zab 107:43
1 Nya. 16:10Law. 22:32; Isa 45:25; Yer 9:24
1 Nya. 16:101Nya 28:9; Flp 4:4
1 Nya. 16:11Amo 5:4; Sef 2:3
1 Nya. 16:11Zab 24:5, 6
1 Nya. 16:12Zab 111:2-4
1 Nya. 16:13Isa 41:8
1 Nya. 16:13Zab 135:4
1 Nya. 16:14Zab 95:7
1 Nya. 16:14Zab 105:7-11
1 Nya. 16:15Kum 7:9
1 Nya. 16:16Mwa 15:18; 17:1, 2
1 Nya. 16:16Mwa 26:3-5
1 Nya. 16:17Mwa 28:14
1 Nya. 16:18Mwa 12:7; 17:8; 35:12
1 Nya. 16:18Kum 32:8
1 Nya. 16:19Mwa 34:30; Kum 26:5; Zab 105:12-15
1 Nya. 16:20Mwa 20:1; 46:6
1 Nya. 16:21Mwa 31:7, 42
1 Nya. 16:21Mwa 12:17; 20:3
1 Nya. 16:22Mwa 20:7
1 Nya. 16:23Zab 40:10; 96:1-6
1 Nya. 16:25Kut 15:11
1 Nya. 16:26Isa 45:20; 1 Kor. 8:4
1 Nya. 16:26Isa 44:24
1 Nya. 16:27Kum 33:26; Zab 8:1
1 Nya. 16:271 Tim. 1:11
1 Nya. 16:28Zab 68:34; 96:7-13
1 Nya. 16:29Kum 28:58; Ne 9:5; Zab 148:13
1 Nya. 16:291Nya 29:3-5; Mt 5:23
1 Nya. 16:29Kum 26:10
1 Nya. 16:30Zab 104:5; Mhu. 1:4
1 Nya. 16:31Zab 97:1
1 Nya. 16:31Ufu 19:6
1 Nya. 16:342Nya 5:13; Lu 18:19
1 Nya. 16:34Zab 103:17; Yer 31:3; Omb 3:22
1 Nya. 16:35Zab 68:20
1 Nya. 16:35Zab 122:4
1 Nya. 16:35Isa 43:21
1 Nya. 16:371Nya 15:16, 17
1 Nya. 16:371Nya 16:4-6
1 Nya. 16:37Kut 29:38; 2Nya 13:11; Ezr 3:4
1 Nya. 16:391Nya 12:28
1 Nya. 16:391 Fal. 3:4
1 Nya. 16:40Kut 29:39; 2Nya 2:4
1 Nya. 16:411Nya 25:1
1 Nya. 16:411Nya 16:4
1 Nya. 16:412Nya 5:13; Ezr 3:11
1 Nya. 16:421Nya 6:31, 33; 15:16, 17
1 Nya. 16:421Nya 25:1, 3
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
  • 42
  • 43
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
1 Mambo ya Nyakati 16:1-43

Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati

16 Basi wakaingiza Sanduku la Mungu wa kweli na kuliweka ndani ya hema yenye Daudi alikuwa ameisimamishia;+ na wakatoa matoleo ya kuteketezwa na zabihu za ushirika mbele ya Mungu wa kweli.+ 2 Wakati Daudi alimaliza kutoa matoleo ya kuteketezwa+ na zabihu za ushirika,+ akabariki watu katika jina la Yehova. 3 Tena, aligawia Waisraeli wote, kila mwanaume na mwanamuke, mukate mumoja wa muviringo, keki ya tende, na keki ya zabibu zenye kukauka. 4 Kisha akaweka Walawi fulani wafanye utumishi mbele ya Sanduku la Yehova,+ wamuheshimie,* wamushukuru, na wamusifu Yehova Mungu wa Israeli. 5 Asafu+ alikuwa kichwa, na wa pili kisha yeye alikuwa Zekaria; na Yeieli, Shemiramoti, Yehieli, Matitia, Eliabu, Benaya, Obed-edomu, na Yeieli+ walipiga vyombo vya kamba na vinubi;+ na Asafu alipiga matoazi,+ 6 na Benaya na Yahazieli makuhani walipiga tarumbeta bila kuacha mbele ya sanduku la agano la Mungu wa kweli.

7 Hiyo ndiyo siku yenye Daudi kwa mara ya kwanza alitoa muchango wa wimbo wenye alitunga ili kumushukuru Yehova na akaupatia Asafu+ na ndugu zake:

8 “Mumushukuru Yehova,+ muitie jina lake,

Mujulishe matendo yake kati ya vikundi vya watu!+

9 Mumuimbie, mumuimbie sifa,*+

Mufikiri sana* juu ya kazi zake zote za ajabu.+

10 Mujisifu juu ya jina lake takatifu.+

Mioyo ya wale wenye kumutafuta Yehova ishangilie.+

11 Mumutafute Yehova+ na nguvu zake,

Mutafute uso wake* bila kuacha.+

12 Mukumbuke kazi za ajabu zenye amefanya,+

Miujiza yake na hukumu zenye ametangaza,

13 Ninyi uzao wa* Israeli mutumishi wake,+

Ninyi wana wa Yakobo, wachaguliwa wake.+

14 Yeye ni Yehova Mungu wetu.+

Hukumu zake ziko katika dunia yote.+

15 Mukumbuke agano lake milele,

Ahadi yenye alitoa,* mupaka vizazi elfu,+

16 Agano lenye alifanya pamoja na Abrahamu,+

Na kiapo chenye alimuapia Isaka,+

17 Chenye aliweka kuwa amri kwa Yakobo+

Na kuwa agano la kudumu kwa Israeli,

18 Akisema, ‘Nitakupatia inchi ya Kanaani+

Kuwa uriti wenu wenye muligawiwa.’+

19 Ilikuwa vile wakati mulikuwa watu kidogo,

Ndiyo, kidogo sana, na mulikuwa wageni katika inchi.+

20 Walitembea-tembea kutoka taifa moja mupaka taifa lingine,

Kutoka ufalme mumoja mupaka kikundi kingine cha watu.+

21 Hakumuruhusu mutu yeyote awakandamize,+

Lakini kwa sababu yao alikaripia wafalme,+

22 Akisema, ‘Musiguse watiwa-mafuta wangu,

Na musitendee manabii wangu jambo lolote la mubaya.’+

23 Mumuimbie Yehova, dunia yote!

Mutangaze wokovu wake siku kwa siku!+

24 Mutangaze utukufu wake kati ya mataifa,

Kazi zake za ajabu kati ya vikundi vyote vya watu.

25 Kwa maana Yehova ni mukubwa na anastahili kusifiwa sana.

Ni mwenye kuogopesha sana kuliko miungu mingine yote.+

26 Miungu yote ya vikundi vya watu ni miungu yenye haina mafaa yoyote,+

Lakini Yehova ndiye alifanya mbingu.+

27 Mbele yake kuko ukubwa* na utukufu;+

Nguvu na furaha viko katika makao yake.+

28 Mumupatie Yehova kile chenye anastahili, ninyi familia za vikundi vya watu,

Mumupatie Yehova kile chenye anastahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+

29 Mumupatie Yehova utukufu wenye jina lake linastahili;+

Mulete zawadi na muingie mbele yake.+

Mumuinamie* Yehova katika mapambo matakatifu.*+

30 Mutetemeke mbele yake, dunia yote!

Dunia* imewekwa imara kabisa; haiwezi kuhamishwa.*+

31 Mbingu zishangilie, na dunia ifurahi;+

Mutangaze kati ya mataifa: ‘Yehova amekuwa Mufalme!’+

32 Bahari ingurume na vyote vyenye kuijaza;

Maeneo ya mashamba na vyote vyenye kuwa ndani yake vishangilie.

33 Wakati uleule miti ya pori ipige vigelegele vya shangwe mbele ya Yehova,

Kwa maana anakuja* kuhukumu dunia.

34 Mumushukuru Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+

Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.+

35 Na museme, ‘Utuokoe, Ee Mungu wa wokovu wetu,+

Utukusanye na kutuokoa kutoka kwa mataifa,

Ili tushukuru jina lako takatifu+

Na tukusifu kwa shangwe.*+

36 Yehova Mungu wa Israeli, asifiwe

Kwa umilele wote.’”*

Na watu wote wakasema, “Amina!”* na wakamusifu Yehova.

37 Kisha Daudi akaacha Asafu+ na ndugu zake pale mbele ya sanduku la agano la Yehova ili wafanye utumishi bila kuacha mbele ya Sanduku hilo,+ kulingana na kawaida ya kila siku.+ 38 Obed-edomu na ndugu zake, watu makumi sita na munane (68), na Obed-edomu mwana wa Yedutuni, na Hosa walikuwa walinzi wa milango mikubwa; 39 na Sadoki+ kuhani na makuhani wenzake walikuwa mbele ya tabenakulo ya Yehova mahali pa juu kule Gibeoni+ 40 ili kumutolea Yehova kwa ukawaida matoleo ya kuteketezwa kwenye mazabahu ya toleo la kuteketezwa, asubui na mangaribi, na kufanya mambo yote yenye yameandikwa katika Sheria ya Yehova yenye aliamuru Israeli.+ 41 Pamoja nao kulikuwa Hemani na Yedutuni+ na wanaume wengine wenye walichaguliwa wenye walitajwa kwa majina yao ili wamushukuru Yehova,+ kwa sababu “upendo wake mushikamanifu unadumu milele”;+ 42 na pamoja nao kulikuwa Hemani+ na Yedutuni ili wapige tarumbeta, matoazi, na vyombo vyenye vilitumiwa ili kumusifu* Mungu wa kweli; na wana wa Yedutuni+ walikuwa kwenye mulango mukubwa. 43 Kisha watu wote wakaenda kwao, na Daudi akaenda kubariki nyumba yake mwenyewe.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine