Mwanzo
16 Basi Sarai, bibi ya Abramu hakukuwa amemuzalia watoto,+ lakini alikuwa na mutumishi Mumisri mwenye jina lake lilikuwa Hagari.+ 2 Kwa hiyo Sarai akamuambia Abramu: “Tafazali unisikilize. Yehova amenizuia kuzaa watoto. Tafazali sasa, lala na mutumishi wangu. Pengine ninaweza kupata watoto kupitia yeye.”+ Kwa hiyo, Abramu akasikiliza mambo yenye Sarai alisema. 3 Kisha Abramu kuishi katika inchi ya Kanaani kwa miaka kumi (10), Sarai, bibi ya Abramu, akamuchukua Hagari, mutumishi wake Mumisri na kumupatia bwana yake Abramu akuwe bibi yake. 4 Kwa hiyo Abramu akalala na Hagari, na akapata mimba. Wakati alijua kwamba iko* na mimba, Hagari akaanza kumuzarau bimukubwa wake.
5 Kwa hiyo Sarai akamuambia Abramu: “Ubaya wenye ninatendewa ni kosa lako. Ni mimi nilimutia mutumishi wangu katika mikono yako,* lakini wakati alijua kwamba iko* na mimba, akaanza kunizarau. Yehova ahukumu kati yangu na wewe.” 6 Kwa hiyo Abramu akamuambia Sarai: “Angalia! Mutumishi wako iko* chini ya mamlaka yako. Umutendee jambo lolote lenye unaona kuwa la muzuri.” Basi Sarai akaanza kumuonea, na Hagari akakimbia mbali naye.
7 Kisha wakati fulani malaika wa Yehova akamukuta Hagari kwenye chemchemi ya maji katika jangwa, chemchemi yenye ilikuwa katika njia ya kuenda Shuri.+ 8 Naye akasema: “Hagari, mutumishi wa Sarai, unatoka wapi na unaenda wapi?” Naye akajibu: “Ninakimbia mbali na bimukubwa wangu Sarai.” 9 Kisha malaika wa Yehova akamuambia: “Rudia kwa bimukubwa wako na ujinyenyekeze chini ya mukono wake.” 10 Kisha malaika wa Yehova akamuambia: “Nitafanya uzao wako ukuwe mwingi* sana, na kwa hiyo haitawezekana kuhesabia uzao huo kwa sababu ya wingi wake.”+ 11 Malaika wa Yehova akaongeza kusema: “Sasa uko na mimba, na utazaa mwana, na utamupatia jina Ishmaeli,* kwa maana Yehova ameona mateso yako. 12 Atakuwa kama punda wa pori.* Mukono wake utapigana na kila mutu; na mukono wa kila mutu utapigana naye, na atakaa akiwa mwenye kuangaliana na ndugu* zake wote.”
13 Kisha akaitia jina la Yehova, mwenye alikuwa anazungumuza naye: “Wewe ni Mungu mwenye kuona,”+ kwa maana alisema: “Je, kweli nimemuona yeye mwenye kuniona?” 14 Ndiyo sababu kisima hicho kiliitwa Beer-lahai-roi.* (Kiko kati ya Kadeshi na Beredi.) 15 Basi Hagari akamuzalia Abramu mwana, na Abramu akamupatia mwana wake, mwenye Hagari alizaa, jina Ishmaeli.+ 16 Abramu alikuwa na miaka makumi munane na sita (86) wakati Hagari alimuzaa Ishmaeli.