Kutoka
36 “Bezaleli atafanya kazi pamoja na Oholiabu na kila mutu mwenye kuwa na ufundi* mwenye Yehova amepatia hekima na uelewaji ili kujua namna ya kufanya kazi yote ya utumishi mutakatifu kama vile Yehova ameamuru.”+
2 Kisha Musa akaita Bezaleli na Oholiabu na kila mutu mwenye ufundi mwenye Yehova alikuwa ameweka hekima katika moyo wake,+ kila mutu mwenye moyo wake ulimusukuma ili ajitolee kufanya kazi.+ 3 Kisha wakakamata kutoka kwa Musa michango yote+ yenye Waisraeli walikuwa wameleta kwa ajili ya kazi ya utumishi mutakatifu. Lakini, watu waliendelea kuleta matoleo ya kujipendea, asubui baada ya asubui.
4 Wakati walianza kufanya kazi takatifu, wafanyakazi wote wenye walikuwa na ufundi walikuja, mumoja kisha mwingine, 5 na walikuwa wanamuambia Musa: “Watu wanaleta vitu vingi kuliko vile vinaombwa kwa ajili ya kazi yenye Yehova ameamuru ifanywe.” 6 Kwa hiyo Musa akaamuru kwamba tangazo litolewe katika kambi yote, kwa kusema: “Wanaume na wanamuke, musilete vitu vingine tena kwa ajili ya muchango mutakatifu.” Basi watu wakazuiwa ili wasilete tena kitu kingine. 7 Vitu hivyo vilikuwa vyenye kuenea kwa ajili ya kazi yote yenye ilipaswa kufanywa, na vilikuwa vingi sana.
8 Kwa hiyo wafanyakazi wote wenye walikuwa na ufundi+ wakatengeneza tabenakulo+ ya vitambaa kumi (10) vya kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa, uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, na kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa; akashona* kwa uzi michoro ya makerubi juu ya vitambaa hivyo.+ 9 Kila kitambaa cha hema kilikuwa na urefu wa mikono* makumi mbili na munane (28) na upana wa mikono ine (4). Vitambaa vyote vilikuwa na kipimo kilekile. 10 Kisha akaunganisha pamoja vile vitambaa tano (5) vya hema, na vile vitambaa vingine tano akaviunganisha pamoja. 11 Kisha akatengeneza viviringo vya uzi ya rangi ya bluu kwenye upindo wa kitambaa kimoja cha hema mahali kingeunganishwa. Na akafanya vilevile kwenye upindo wa kitambaa cha inje kabisa cha hema mahali palepale kwenye kingeunganishwa. 12 Akatengeneza viviringo makumi tano (50) vya uzi kwenye kitambaa kimoja cha hema na viviringo makumi tano vya uzi kwenye upindo mwingine wa kitambaa mahali kingeunganishwa ili viviringo vya uzi viangaliane. 13 Mwishowe, akatengeneza vifungo makumi tano (50) vya zahabu na akaunganisha vitambaa vya hema pamoja kwa kutumia vifungo hivyo, kwa hiyo tabenakulo ikakuwa hema moja.
14 Kisha akatengeneza vitambaa vya hema vya manyoya ya mbuzi kwa ajili ya hema yenye kuwa juu ya tabenakulo. Akatengeneza vitambaa kumi na moja (11) vya hema.+ 15 Kila kitambaa cha hema kilikuwa na urefu wa mikono makumi tatu (30) na upana wa mikono ine (4). Vitambaa vyote kumi na moja (11) vya hema vilikuwa na kipimo kilekile. 16 Kisha akaunganisha pamoja vitambaa tano (5) vya hema, na akaunganisha pamoja vile vitambaa vingine sita (6) vya hema. 17 Halafu akatengeneza viviringo makumi tano (50) vya uzi kwenye upindo wa inje kabisa wa kitambaa cha hema mahali kinaunganishwa, na akatengeneza viviringo makumi tano vya uzi kwenye upindo wa kitambaa kingine cha hema chenye kuunganishwa nacho. 18 Na akatengeneza vifungo makumi tano (50) vya shaba vya kuunganisha hema pamoja kusudi ikuwe kitu kimoja.
19 Akatengeneza kifuniko cha hema kwa kutumia ngozi za kondoo-dume zenye kutiwa rangi nyekundu na kifuniko cha ngozi za sili* cha kuweka juu ya hema.+
20 Kisha akatengeneza kwa ajili ya tabenakulo kadre za mbao za muti wa mugunga,*+ zenye zilisimama wima.+ 21 Kila kadre ya mbao ilikuwa na urefu wa mikono kumi (10) na upana wa mukono mumoja na nusu. 22 Kila kadre ya mbao ilikuwa na ndimi* mbili zenye kuunganishwa pamoja. Ni vile alitengeneza kadre zote za mbao za tabenakulo. 23 Kwa hiyo akatengeneza kadre za mbao kwa ajili ya upande wa kusini wa tabenakulo, kadre makumi mbili (20) za mbao, kuelekea kusini. 24 Kisha akatengeneza vikalio makumi ine (40) vya feza ili kuwekwa chini ya zile kadre makumi mbili (20) za mbao, vikalio mbili chini ya kadre moja ya mbao kwa ajili ya ndimi zake mbili na vikalio mbili chini ya kila kadre ya mbao yenye kufuata kwa ajili ya ndimi zake mbili.+ 25 Kwa ajili ya upande mwingine wa tabenakulo, upande wa kaskazini, akatengeneza kadre makumi mbili (20) za mbao 26 na vikalio vyake makumi ine (40) vya feza, vikalio mbili chini ya kadre moja ya mbao na vikalio mbili chini ya kila moja ya zile kadre zingine za mbao.
27 Kwa ajili ya sehemu ya nyuma ya tabenakulo kuelekea upande wa mangaribi, akatengeneza kadre sita (6) za mbao.+ 28 Akatengeneza kadre mbili za mbao ili zikuwe nguzo mbili za pembe za tabenakulo kwenye pembe za nyuma. 29 Nguzo hizo zilikuwa mbili-mbili kuanzia chini mupaka juu, mupaka kwenye pete ya kwanza. Ni vile alitengeneza zile nguzo mbili za pembe. 30 Kwa hiyo zilifikia hesabu ya kadre munane (8) za mbao pamoja na vikalio vyake kumi na sita (16) vya feza, vikalio mbili chini ya kila kadre ya mbao.
31 Kisha akatengeneza fito za muti wa mugunga,* fito tano (5) kwa ajili ya kadre za mbao za upande mumoja wa tabenakulo+ 32 na fito tano (5) kwa ajili ya kadre za mbao za upande mwingine wa tabenakulo na fito tano kwa ajili ya kadre za mbao za tabenakulo kwa ajili ya sehemu ya nyuma kuelekea upande wa mangaribi. 33 Akatengeneza ufito wa katikati ili upite katikati ya zile kadre za mbao kuanzia mwisho mumoja mupaka mwisho mwingine. 34 Akafunika zile kadre za mbao kwa zahabu, na akatengeneza pete za zahabu za kadre hizo za mbao ili zishikilie fito hizo, na akafunika fito hizo kwa zahabu.+
35 Kisha akatengeneza pazia+ la uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa. Akashona kwa uzi michoro ya makerubi+ kwenye pazia hilo.+ 36 Kisha akaitengenezea nguzo ine (4) za muti wa mugunga* na kuzifunika kwa zahabu, akatengeneza pia kulabu* za zahabu na vikalio ine vya feza kwa ajili ya nguzo hizo. 37 Tena akatengeneza kitambaa cha kuficha* kwa ajili ya muingilio wa hema kwa kutumia uzi ya rangi ya bluu, manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau, kitambaa cha rangi nyekundu yenye kungaa, na kitani kizuri chenye kusukwa-sukwa na kufumwa pamoja,+ 38 na pia nguzo zake tano (5) na kulabu* zake. Akafunika kwa zahabu sehemu za juu za nguzo hizo pamoja na vibanio* vyake, lakini vikalio vyake tano vilikuwa vya shaba.