Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Matendo 27
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Matendo

      • Paulo anasafiri katika bahari kuenda Roma (1-12)

      • Zoruba inapiga mashua (13-38)

      • Mashua inavunjika (39-44)

Matendo 27:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 25:12

Matendo 27:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

  • *

    Bandari ni mahali mashua zinaegesha.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 19:29; 20:4; Kol 4:10

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 203-204

Matendo 27:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “fazili za kibinadamu.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 204

Matendo 27:4

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 204, 208

Matendo 27:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Bandari ni mahali mashua zinaegesha.

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 204-205, 208

Matendo 27:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 205, 208

Matendo 27:7

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 205

Matendo 27:8

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 205

Matendo 27:9

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 16:29, 30; 23:27

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Watu Wote),

    Na. 5 2017 uku. 9

    Munara wa Mulinzi,

    1/2/2010, uku. 23

    Kutoa Ushahidi, uku. 205-207

Matendo 27:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

  • *

    Ao “nafsi zetu.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Watu Wote),

    Na. 5 2017 uku. 9

Matendo 27:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 205-207

Matendo 27:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Bandari ni mahali mashua zinaegesha.

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 205-207

Matendo 27:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Nanga ni jiwe ao chuma chenye kufungwa kwa kamba ao kwa munyororo na kuingizwa ndani ya maji ili mashua isibebwe na maji.

Matendo 27:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Ni kusema, upepo wa kaskazini-mashariki.

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 207

Matendo 27:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Matendo 27:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Mashua ya kidogo yenye ingetumiwa ili kuokoa uzima.

  • *

    Tezi ni sehemu ya nyuma ya mashua.

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 207

Matendo 27:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

  • *

    Angalia Maana ya Maneno.

  • *

    Tanga ni kitambaa kikubwa chenye kinafungwa kwenye mashua na kinasukumwa na upepo ili mashua iende mbele.

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 207

Matendo 27:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Matendo 27:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 207

Matendo 27:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “yenye haikukuwa ya kidogo.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 207

Matendo 27:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 27:9, 10

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 207-208

Matendo 27:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “nafsi moja yenye itapotea.”

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 207-208

Matendo 27:23

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 5:18, 19; Ebr 1:7, 14

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 208

Matendo 27:24

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 23:11; 25:11, 12

Matendo 27:26

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 28:1

Matendo 27:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 208-209

Matendo 27:28

Maelezo ya Chini

  • *

    Bildi ni chombo chenye kinatumiwa kupima urefu wa maji kuenda chini.

  • *

    Karibu metre 36 (futi 120). Angalia Nyongeza B14.

  • *

    Karibu metre 27 (futi 90). Angalia Nyongeza B14.

Matendo 27:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Tezi ni sehemu ya nyuma ya mashua.

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 208-209

Matendo 27:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

  • *

    Omo ni sehemu ya mbele ya mashua.

Matendo 27:31

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 27:22

Matendo 27:32

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Matendo 27:35

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 206, 208-209

Matendo 27:37

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “nafsi.”

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Matendo 27:38

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yon 1:5

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 209

Matendo 27:39

Maelezo ya Chini

  • *

    Guba ni sehemu ya bahari yenye inaingia katika inchi kavu.

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 28:1

Matendo 27:40

Maelezo ya Chini

  • *

    Kasia ni chombo chenye kufanana na mwiko chenye kinatumiwa kuendesha mashua.

  • *

    Tanga ni kitambaa kikubwa chenye kinafungwa kwenye mashua na kinasukumwa na upepo ili mashua iende mbele.

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 209

    “Kila Andiko,” uku. 200

Matendo 27:41

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

  • *

    Omo ni sehemu ya mbele ya mashua.

  • *

    Tezi ni sehemu ya nyuma ya mashua.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 27:22; 2 Kor. 11:25

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Kutoa Ushahidi, uku. 209

Matendo 27:44

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua ya maji; bateau.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mdo 27:23, 24

Maandiko ingine

Mdo. 27:1Mdo 25:12
Mdo. 27:2Mdo 19:29; 20:4; Kol 4:10
Mdo. 27:9Law. 16:29, 30; 23:27
Mdo. 27:21Mdo 27:9, 10
Mdo. 27:23Mdo 5:18, 19; Ebr 1:7, 14
Mdo. 27:24Mdo 23:11; 25:11, 12
Mdo. 27:26Mdo 28:1
Mdo. 27:31Mdo 27:22
Mdo. 27:38Yon 1:5
Mdo. 27:39Mdo 28:1
Mdo. 27:41Mdo 27:22; 2 Kor. 11:25
Mdo. 27:44Mdo 27:23, 24
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
  • 33
  • 34
  • 35
  • 36
  • 37
  • 38
  • 39
  • 40
  • 41
  • 42
  • 43
  • 44
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Matendo 27:1-44

Matendo ya Mitume

27 Basi kwa kuwa iliamuliwa tusafiri katika mashua* kuenda Italia,+ wakamutia Paulo na wafungwa wengine katika mukono wa ofisa wa jeshi mwenye kuitwa Yulio, wa kikundi cha maaskari cha Augusto. 2 Tukapanda katika mashua* ya kutoka Adramitiamu yenye ilikuwa karibu kusafiri kuenda kwenye bandari* zenye kuwa pembeni ya bahari katika jimbo la Asia, tukasafiri kwa mashua; Aristarko,+ Mumakedonia wa Tesalonike, alikuwa pamoja na sisi. 3 Siku yenye ilifuata tukafika Sidoni, na Yulio akamutendea Paulo kwa fazili* na kumuruhusu aende kwa marafiki wake ili wamuhangaikie.

4 Wakati tulitoka pale, tukasafiri katika bahari chini ya kisiwa cha Kipro ili kujilinda na upepo wenye ulikuwa unatutokea upande wa mbele. 5 Kisha tukapita katika bahari kubwa pembeni-pembeni ya Kilikia na Pamfilia na tukasimama kwenye bandari* ya Mira kule Likia. 6 Pale ofisa wa jeshi akapata mashua* yenye kutoka Aleksandria yenye ilikuwa inaenda Italia, na akatuagiza tupande katika mashua hiyo. 7 Sasa, kisha kusafiri polepole kwa siku nyingi, tukafika kwa shida kule Kinido. Kwa kuwa upepo ulituzuia kusonga mbele, tukasafiri chini ya Krete kule Salmone. 8 Tukasafiri kwa shida karibu-karibu na inchi kavu, tukafika mahali kwenye kunaitwa Bandari ya Muzuri, karibu na muji wa Lasea.

9 Wakati mwingi ulikuwa umepita na kufikia sasa ilikuwa hatari kusafiri katika bahari, kwa sababu hata kipindi cha kufunga cha Siku ya Kufunika Zambi+ kilikuwa kimepita, basi Paulo akatoa pendekezo, 10 akawaambia: “Wanaume, ninaona kwamba safari hii italeta uharibifu na upotevu mukubwa, haiko tu mizigo na mashua,* lakini pia uzima wetu.”* 11 Hata hivyo, ofisa wa jeshi akamusikiliza muendesha-mashua na mwenye mashua* kuliko kusikiliza mambo yenye Paulo alikuwa anasema. 12 Kwa kuwa bandari* hiyo haikufaa watu kukaa katika kipindi cha baridi, wengi wakasema tuendelee na safari ili kuona kama wangeweza kukaa katika kipindi cha baridi kule Feniki, yenye ni bandari ya Krete yenye kufunguka kuelekea kaskazini-mashariki na kusini-mashariki.

13 Wakati upepo wa kusini ulivuma kwa utulivu, waliwaza wametimiza kusudi lao, wakangoa nanga* na wakaanza kusafiri pembeni-pembeni ya Krete karibu na inchi kavu. 14 Lakini, kisha wakati kidogo, upepo mukali wenye kuitwa Euroakilo* ukavuma kwa nguvu juu yake. 15 Kwa kuwa mashua* ilipigwa sana na upepo na haikuweza kuuvumilia, tukaiachilia, na upepo ukaanza kutusukuma. 16 Kisha tukapita haraka chini ya kisiwa kidogo chenye kuitwa Kauda, na bado ilikuwa vigumu kuokoa mashua ya kidogo* yenye ilikuwa kwenye tezi* ya mashua.* 17 Lakini kisha kuipandisha ndani ya mashua* kubwa, wakafunga mashua hiyo kwa kamba, na kwa kuwa waliogopa kukwama kwenye muchanga wa Sirti,* wakafungua kamba zenye kufunga tanga* na hivyo wakaanza kusukumwa na upepo. 18 Kwa sababu tulikuwa tunarushwa-rushwa kwa nguvu na zoruba, siku yenye ilifuata wakaanza kupunguza uzito wa mashua.* 19 Na siku ya tatu (3), wakatupa kamba fulani za mashua* hiyo kwa mikono yao wenyewe.

20 Wakati jua na nyota havikuonekana kwa siku nyingi na tulikuwa tunapigwa na zoruba kali,* mwishowe tumaini lote la kuokoka likaanza kupotea. 21 Kisha watu kukaa wakati murefu bila kula, Paulo alisimama katikati yao na kusema: “Wanaume, kwa kweli mulipaswa kufuata shauri langu na hamungesafiri katika bahari kutoka Krete na hivyo hamungepata uharibifu huu na hamungepoteza vitu.+ 22 Lakini, sasa ninawatia moyo musiogope, kwa maana hakuna hata mumoja wenu mwenye atapotea,* mashua* tu ndiyo itapotea. 23 Usiku huu malaika+ wa Mungu mwenye mimi ni mali yake na mwenye ninatolea utumishi mutakatifu alisimama karibu yangu 24 na akasema: ‘Usiogope, Paulo. Unapaswa kusimama mbele ya Kaisari,+ na angalia! Mungu amekupatia wale wote wenye wanasafiri pamoja na wewe.’ 25 Kwa hiyo, wanaume, musiogope, kwa maana ninamuamini Mungu kwamba itakuwa kabisa kama vile niliambiwa. 26 Hata hivyo, lazima tutupwe kwenye inchi kavu kwenye kisiwa fulani.”+

27 Sasa wakati usiku wa kumi na ine (14) ulifika na tukiwa tunarushwa-rushwa katika Bahari ya Adria, katikati ya usiku watumishi wa mashua* wakaanza kuona kama vile walikuwa wanakaribia inchi kavu. 28 Wakapima urefu kuenda chini kwa bildi* na kupata pima makumi mbili (20),* basi wakasonga mbele kidogo wakaishusha tena na kupata pima kumi na tano (15).* 29 Na kwa sababu waliogopa kwamba tutakwama kwenye miamba, wakatupa nanga ine (4) kutoka kwenye tezi* na wakaanza kutamani ikuwe asubui. 30 Lakini wakati watumishi wa mashua* walianza kujaribu kutoroka kutoka kwenye mashua na kushusha mashua ya kidogo ndani ya bahari wakisingizia kwamba walikusudia kushusha nanga kutoka kwenye omo,* 31 Paulo akamuambia ofisa wa jeshi na maaskari: “Kama watu hawa hawabakie katika mashua,* hamuwezi kuokoka.”+ 32 Basi maaskari wakakata kamba za ile mashua* ya kidogo na wakaiacha ianguke.

33 Sasa wakati ilikaribia kuwa asubui, Paulo akawatia wote moyo wakule chakula, kwa kusema: “Leo ni siku ya kumi na ine (14) tangu mumekuwa munangojea kwa wasiwasi, bila kula chakula chochote. 34 Basi ninawatia moyo mukule chakula; hiyo ni kwa ajili ya usalama wenu, kwa maana hakuna hata unywele mumoja wa kichwa cha mutu yeyote kati yenu wenye utapotea.” 35 Kisha kusema vile, akakamata mukate, akatoa shukrani kwa Mungu mbele yao wote, akauvunja, na akaanza kula. 36 Basi wote wakajipa moyo na wakaanza kula. 37 Sisi wote tulikuwa watu* mia mbili makumi saba na sita (276) katika mashua.* 38 Wakati walikuwa wamekula chakula mupaka wakashiba, wakapunguza uzito wa mashua* kwa kutupa ngano katika bahari.+

39 Wakati ilikuwa asubui, hawakutambua inchi hiyo,+ lakini waliona guba* yenye inchi kavu, na walitaka kabisa kupeleka mashua* kwenye inchi kavu kama wangeweza. 40 Basi wakakata nanga na kuziacha zianguke katika bahari, wakati uleule wakafungua kamba za makasia* yenye kuongoza; na kisha kupandisha tanga* la mbele kwenye upepo, wakaelekea kwenye inchi kavu. 41 Wakati waligonga rundo kubwa la muchanga lenye lilikuwa linapigwa na bahari pande zote mbili, wakakwamisha mashua* na omo* ikajigonga na kukaa bila kutikisika, lakini mawimbi yakaanza kuvunja tezi* kwa nguvu vipande-vipande.+ 42 Halafu maaskari wakaamua kuua wafungwa ili mutu yeyote asiogelee na kutoroka. 43 Lakini ofisa wa jeshi alikuwa anapenda kabisa kumufikisha Paulo salama na akawazuia kutimiza mupango wao. Akaamuru wale wenye wanaweza kuogelea wajitupe katika bahari na watangulie kuogelea mupaka kwenye inchi kavu, 44 na wenye walibakia wangefuata, wamoja juu ya mbao na wengine juu ya vipande vya mashua.* Basi wote wakafika salama kwenye inchi kavu.+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine