Isaya
35 Jangwa na inchi yenye kukauka vitafurahi,+
Jangwa tambarare litashangilia na kutoa maua kama zafarani.+
Wataona utukufu wa Yehova, uzuri wa Mungu wetu.
4 Muambie wale wenye kuhangaika katika moyo:
“Mukuwe na nguvu. Musiogope.
Muangalie! Mungu wenu atakuja na kisasi,
Mungu atakuja na malipo.+
Atakuja na kuwaokoa ninyi.”+
6 Wakati huo kilema wa miguu ataruka-ruka kama paa+
Na ulimi wa bubu utapiga vigelegele vya shangwe.+
Kwa maana maji yatabubujika katika jangwa,
Na mito midogo katika jangwa tambarare.
7 Inchi yenye kukaushwa na joto itakuwa kama kiziwa cha maji chenye matete,
Na inchi yenye kiu kama chemchemi za maji.+
Katika mashimo kwenye mbweha walikuwa wanapumuzikia,+
Kutakuwa majani ya mubichi na matete na mafunjo.*
Mwenye haiko safi hatapita kwenye njia hiyo.+
Imewekwa kwa ajili ya ule mwenye kutembea kwenye njia hiyo;
Hakuna mupumbavu mwenye atapotea na kuingia katika njia hiyo.
9 Hakuna simba mwenye atakuwa kule,
Na hakuna wanyama hatari wa pori wenye watakuja juu yake.
10 Wale wenye walikombolewa na Yehova watarudia+ na kuja Sayuni kwa vigelegele vya shangwe.+
Shangwe yenye haina mwisho itakuwa taji la vichwa vyao.+
Watafurahi na kushangilia,
Na huzuni na kilio cha maumivu vitaisha.+