Hosea
3 Kisha Yehova akaniambia: “Uende tena, umupende ule mwanamuke mwenye anapendwa na mwanaume mwingine na mwenye anafanya uzinifu,+ kama vile Yehova anapenda watu wa Israeli+ wakati wanageuka kuelekea miungu mingine+ na wanapenda keki za zabibu zenye kukauka.”*
2 Basi nikajinunulia mwanamuke huyo kwa vipande kumi na tano (15) vya feza na kipimo kimoja cha homeri* na nusu ya shayiri. 3 Kisha nikamuambia: “Utaendelea kuwa wangu kwa siku nyingi. Haupaswe kufanya ukahaba,* na haupaswe kulala na mwanaume mwingine, na mimi nitakutendea kwa njia ileile.”*
4 Hiyo ni kwa sababu kwa wakati murefu* watu wa Israeli watakaa bila mufalme,+ bila mukubwa, bila zabihu, bila nguzo, na bila efodi+ na sanamu za terafimu.*+ 5 Kisha watu wa Israeli watarudia na kumutafuta Yehova Mungu wao+ na Daudi mufalme wao,+ na watakuja wakitetemeka kwa Yehova na kwa wema wake katika kipindi cha mwisho cha zile siku.+