Zaburi
Kwa kiongozi; juu ya Gititi.* Ya wana wa Kora.+ Muziki.
Moyo wangu na mwili wangu vinamupigia Mungu mwenye kuishi vigelegele vya shangwe.
3 Hata ndege anapata makao kule
Na mbaruwayu anajipatia chicha,*
Kwenye anatunza vitoto vyake
Karibu na mazabahu yako kubwa, Ee Yehova wa majeshi,
Mufalme wangu na Mungu wangu!
4 Wenye furaha ni wale wenye wanakaa katika nyumba yako!+
Wanaendelea kukusifu.+ (Sela)
5 Wenye furaha ni watu wenye wanapata nguvu kutoka kwako,+
Wenye mioyo yao imekazwa juu ya barabara kubwa.
6 Wakati wanapita katika Bonde la Mibaka,*
Wanalifanya kuwa mahali kwenye chemchemi;
Na mvua ya kwanza inalivalisha* baraka.
7 Wataendelea kutembea kutoka nguvu mupaka nguvu zaidi;+
Kila mumoja wao anaonekana mbele ya Mungu kule Sayuni.
8 Ee Yehova Mungu wa majeshi, sikia sala yangu;
Sikiliza, Ee Mungu wa Yakobo. (Sela)
10 Kwa maana siku moja katika viwanja vyako inapita siku elfu moja (1 000) mahali pengine popote!+
Ninachagua kusimama kwenye muingilio wa* nyumba ya Mungu wangu
Kuliko kukaa katika mahema ya uovu.
Yehova hatawaima jambo lolote la muzuri
Wale wenye kutembea kwa uaminifu-mushikamanifu.+
12 Ee Yehova wa majeshi,
Mwenye furaha ni mutu mwenye anakutegemea.+