Mika
Munapaswa kujua yenye kuwa haki, haiko vile?
2 Lakini munachukia mambo ya muzuri+ na munapenda mambo ya mubaya;+
Munachuna watu wangu ngozi na kuondoa nyama kwenye mifupa yao.+
3 Pia munakula nyama ya watu wangu+
Na kuwachuna ngozi,
Munavunja mifupa yao, na kuiponda-ponda,+
Kama kitu chenye kupikwa ndani ya chungu,* kama nyama ndani ya chungu cha kupikia.
4 Wakati huo watamuita Yehova awasaidie,
Lakini hatawajibu.
5 Yehova anasema hivi juu ya manabii wenye kupotosha watu wake,+
Wenye kutangaza ‘Amani!’+ wakati wanatafuna kwa meno yao,+
Lakini wenye kutangaza* vita juu ya mutu yeyote mwenye hatie kitu katika vinywa vyao:
Jua litashuka juu ya manabii,
Na muchana utageuka kuwa giza kwao.+
Wote watafunika masharubu yao,*
Kwa maana hakuna jibu kutoka kwa Mungu.’”
8 Lakini mimi, ninajaa nguvu kupitia roho ya Yehova,
Na haki na uwezo,
Ili nimuambie Yakobo uasi wake na Israeli zambi yake.
9 Tafazali musikie jambo hili, ninyi vichwa vya nyumba ya Yakobo
Na ninyi makamanda wa nyumba ya Israeli,+
Wenye kuchukia haki na kupotosha mambo yote yenye kunyooka,+
10 Wenye kujenga Sayuni kwa kumwanga damu na Yerusalemu kwa ukosefu wa haki.+
11 Viongozi wake* wanapokea rushwa* ili kuhukumu,+
Makuhani wake wanafundisha ili wapate malipo,+
Na manabii wake wanafanya uaguzi ili wapate feza.+
Na hata hivyo wanamutegemea Yehova,* kwa kusema:
“Je, Yehova haiko pamoja na sisi?+
Hakuna musiba wenye utatupata.”+