Isaya
59 Angalia! Mukono wa Yehova hauko mufupi sana usiweze kuokoa,+
Wala sikio lake haliko nzito sana lisiweze kusikia.+
2 Hapana, makosa yenu wenyewe ndiyo yamewatenganisha na Mungu wenu.+
Zambi zenu zilimufanya awafiche uso wake,
Na anakataa kuwasikia.+
Midomo yenu inasema uongo,+ na ulimi wenu unasema ukosefu wa haki kwa sauti ya chini.
Wanategemea jambo la kuwazia-wazia tu*+ na kusema mambo yenye hayana mafaa yoyote.
Wanatunga mimba ya taabu na kuzaa jambo lenye kuumiza.+
Kila mwenye anakula mayai yao atakufa,
Na yai lenye kuvunjwa linatotoa nyoka-kipiri.
Kazi zao ni zenye kuumiza,
Na matendo ya jeuri yako katika mikono yao.+
Mawazo yao ni mawazo yenye kuumiza;
Uharibifu na taabu viko katika njia zao.+
Wanapotosha barabara zao;
Hakuna mwenye anatembea mule mwenye atapata amani.+
Tunaendelea kutumainia mwangaza, lakini, angalia! kuko giza;
Tunaendelea kutumainia uangavu, lakini tunaendelea kutembea katika weusi.+
Tunajikwaa katikati ya muchana kama katika giza la mangaribi;
Kati ya wenye nguvu tuko kama vile wafu.
11 Sisi wote tunaendelea kunguruma kama dubu
Na kulia kwa huzuni kama njiwa.
Tunatumainia kupata haki, lakini hakuna;
Tunatumainia kupata wokovu, lakini uko mbali sana na sisi.
Kwa maana maasi yetu yako pamoja na sisi;
Tunajua muzuri makosa yetu.+
13 Tumemukosea na kumukana Yehova;
Tumemugeuzia Mungu wetu migongo yetu.
Tumesema kuhusu ukandamizaji na uasi;+
Tumetunga uongo na kusema kwa sauti ya chini maneno ya uongo kutoka katika moyo.+
Na uadilifu* unasimama mbali;+
Kwa maana kweli imejikwaa* katika kiwanja cha watu wote,
Na jambo lenye kunyooka haliwezi kuingia.
16 Aliona kama hapakukuwa mutu,
Na alishangaa kama hakuna mwenye aliingilia kati,
Basi mukono wake ukaleta wokovu,*
Na haki yake mwenyewe ikamutegemeza.
18 Atawapatia zawabu kulingana na matendo yao:+
Kasirani kali kwa wapinzani wake, malipo kwa maadui wake.+
Na atalipa visiwa kile chenye vinastahili.
19 Wataogopa jina la Yehova kuanzia mahali jua linashukia
Na utukufu wake kuanzia mahali jua linatokea,
Kwa maana ataingia kama muto wenye kuenda haraka,
Wenye kuendeshwa na roho ya Yehova.
21 “Lakini mimi, hili ndilo agano langu pamoja nao,”+ ni vile Yehova anasema. “Roho yangu yenye kuwa juu yako na maneno yangu yenye nimetia katika kinywa chako—hayataondolewa katika kinywa chako, katika kinywa cha watoto wako,* ao katika kinywa cha wajukuu wako,”* ni vile Yehova anasema, “kuanzia sasa na milele.”