Amosi
2 “Yehova anasema hivi:
‘“Kwa sababu Moabu ameasi* mara tatu (3),+ na kwa sababu ameasi mara ine (4), sitabadilisha hilo,
Kwa sababu aliteketeza kwa moto mifupa ya mufalme wa Edomu ili kupata chokaa.
2 Kwa hiyo nitatuma moto katika Moabu, na utateketeza minara yenye ngome ya Kerioti;+
Moabu atakufa katika makelele,
Kutakuwa makelele ya vita na sauti ya baragumu.+
3 Nitaondoa mutawala* katikati yake
Na nitaua wakubwa wake wote pamoja naye,”+ ni vile Yehova anasema.’
4 Yehova anasema hivi:
‘Kwa sababu Yuda ameasi mara tatu (3),+ na kwa sababu ameasi mara ine (4), sitabadilisha hilo,
Kwa sababu walikataa sheria ya* Yehova,
Na kwa sababu hawakufuata masharti yangu;+
Lakini wamepotoshwa na uongo wenye mababu zao walifuata.+
6 Yehova anasema hivi:
‘Kwa sababu Israeli ameasi mara tatu (3),+ na kwa sababu ameasi mara ine (4), sitabadilisha hilo,
Kwa sababu wanauzisha wenye haki ili wapate feza,
Na wanauzisha maskini kwa bei ya viatu mbili.+
7 Wanakanyanga vichwa vya watu wa hali ya chini katika mavumbi ya dunia,+
Na wanafunga njia ya wapole.+
Mwanaume na baba yake wanalala na mutoto mwanamuke uleule,
Na hivyo wanachafua jina langu takatifu.
8 Wanajinyoosha karibu na kila mazabahu+ juu ya nguo zenye walinyanganya ili zikuwe kitu chenye kinawekeshwa kwa ajili ya mukopo;+
Na divai yenye wanakunywa katika nyumba ya* miungu yao waliipata kwa watu wenye walilipisha amande.’*
9 ‘Lakini mimi ndiye niliharibu Mwamori mbele ya watu wangu,+
Mwenye alikuwa murefu kama mierezi na mwenye nguvu kama mialoni;
Niliharibu matunda yake yenye kuwa juu na mizizi yake yenye kuwa chini.+
10 Niliwapandisha kutoka katika inchi ya Misri,+
Na niliwatembeza katika jangwa kwa miaka makumi ine (40),+
Ili mukamate inchi ya Mwamori.
11 Niliinua wamoja kati ya wana wenu ili wakuwe manabii+
Na wamoja kati ya vijana wenu wanaume ili wakuwe Wanaziri.+
Je, haiko vile, Enyi watu wa Israeli?’ ni vile Yehova anasema.
12 ‘Lakini muliendelea kupatia Wanaziri divai ili wakunywe,+
Na muliwaamuru manabii: “Hamupaswe kutoa unabii.”+
13 Kwa hiyo nitawaponda-ponda katika mahali penu,
Kama vile gari lenye kujaa nafaka yenye kukatwa linaponda-ponda kitu chenye kuwa chini yake.
14 Mwenye kuenda mbio hatakuwa na mahali pa kukimbilia,+
Mwenye nguvu hataendelea kuwa na nguvu zake,
Na hakuna mupiganaji-vita mwenye ataokoa uzima wake.*
15 Mwenye upinde hatasimama,
Mutu mwenye miguu yenye kuenda mbio hataponyoka,
Na mupanda-farasi hataokoa uzima wake.*