Kutoka
31 Yehova akaendelea kusema na Musa, na kumuambia: 2 “Angalia, nimemuchagua* Bezaleli+ mwana wa Uri mwana wa Huru wa kabila la Yuda.+ 3 Nitamujaza roho ya Mungu, ili kumupatia hekima, uelewaji, na ujuzi wa kila namna ya ufundi, 4 ili atengeneze vyombo vya ufundi, ili afanye kazi ya zahabu, feza, na shaba, 5 ili achonge majiwe na kuyaweka katika vikalio vyake,+ na kutengeneza vitu vya mbao vya kila namna.+ 6 Pia, nimemuchagua Oholiabu+ mwana wa Ahisamaki wa kabila la Dani ili amusaidie, na ninatia hekima katika moyo wa wote wenye kuwa na ufundi,* ili watengeneze kila kitu chenye nilikuamuru:+ 7 hema ya mukutano,+ sanduku la Ushuhuda+ na kifuniko+ chenye kuwa juu yake, vifaa vyote vya hema, 8 meza+ na vyombo vyake, kinara cha taa cha zahabu safi na vyombo vyake vyote,+ mazabahu ya uvumba,+ 9 mazabahu ya toleo la kuteketezwa+ na vyombo vyake vyote, beseni na kitu cha kuweka beseni juu yake,+ 10 nguo zenye kusukwa muzuri, nguo takatifu za Haruni kuhani, nguo za wana wake ili watumikie wakiwa makuhani,+ 11 mafuta ya kutia mafuta, na uvumba wenye marashi kwa ajili ya patakatifu.+ Watafanya kila kitu chenye nimekuamuru.”
12 Yehova akaendelea kumuambia Musa: 13 “Sema na Waisraeli na kuwaambia, ‘Zaidi sana, mutashika sabato zangu,+ kwa maana ni alama kati yangu na ninyi katika vizazi vyenu ili mujue kwamba mimi, Yehova, ninawatakasa ninyi. 14 Munapaswa kushika Sabato, kwa maana ni kitu kitakatifu kwenu.+ Kila mutu mwenye ataichafua anapaswa kuuawa. Kama mutu yeyote anafanya kazi siku hiyo, basi mutu huyo anapaswa* kuondolewa* kati ya watu wake.+ 15 Kazi inaweza kufanywa kwa siku sita (6), lakini siku ya saba (7) ni sabato ya pumuziko kamili.+ Ni kitu kitakatifu kwa Yehova. Mutu yeyote mwenye atafanya kazi siku ya Sabato anapaswa kuuawa. 16 Waisraeli wanapaswa kushika Sabato; wanapaswa kushika Sabato katika vizazi vyao vyote. Ni agano la kudumu. 17 Ni alama ya kudumu kati yangu na watu wa Israeli,+ kwa sababu katika siku sita (6) Yehova alifanya mbingu na dunia na katika siku ya saba (7) alipumuzika na kustarehe.’”+
18 Sasa wakati tu alimaliza kuzungumuza naye kwenye Mulima Sinai, akamupatia Musa mabamba mbili ya Ushuhuda,+ mabamba ya majiwe yenye yaliandikwa na kidole cha Mungu.+