Yoshua
5 Wakati tu wafalme wote wa Waamori+ wenye walikuwa upande wa mangaribi* wa Yordani na wafalme wote wa Wakanaani+ wenye walikuwa karibu na bahari walisikia kwamba Yehova alikausha maji ya Yordani mbele ya Waisraeli mupaka wakati walimaliza kuvuka, wakavunjika moyo*+ na hawakukuwa na uhodari wowote kwa sababu ya Waisraeli.+
2 Wakati huo Yehova akamuambia Yoshua: “Tengeneza visu vya majiwe magumu na utahiri+ wanaume wa Israeli tena, mara ya pili.” 3 Basi Yoshua akatengeneza visu vya majiwe magumu na kutahiri wanaume wa Israeli kule Gibeat-haaraloti.*+ 4 Yoshua aliwatahiri kwa sababu hii: Wanaume wote wenye walitoka Misri, ni kusema, wanaume wote wa vita,* walikufa ndani ya jangwa katika safari yao kisha kutoka Misri.+ 5 Watu wote wenye walitoka Misri walikuwa wametahiriwa, lakini watu wote wenye walizaliwa katika jangwa katika safari yao kisha kutoka Misri hawakukuwa wametahiriwa. 6 Waisraeli walitembea miaka makumi ine (40)+ katika jangwa mupaka wakati taifa lote lilikufa, ni kusema, wanaume wa vita wenye walitoka Misri wenye hawakutii sauti ya Yehova.+ Yehova aliwaapia kwamba hatawaruhusu hata kidogo waone inchi+ yenye Yehova alikuwa ameapia mababu zao kwamba atatupatia,+ inchi yenye kutiririka maziwa na asali.+ 7 Basi akasimamisha wana wao pa nafasi yao.+ Yoshua akawatahiri; hawakukuwa wametahiriwa kwa sababu hawakuwatahiri wakati wa safari.
8 Wakati walimaliza kutahiri taifa lote, wakaendelea kukaa mahali kwenye walikuwa katika kambi mupaka wakati walipona.
9 Kisha Yehova akamuambia Yoshua: “Leo nimeondoa juu yenu haya ya Misri.” Basi mahali pale kunaitwa Gilgali*+ mupaka leo.
10 Waisraeli wakaendelea kupiga kambi Gilgali, na wakafanya sikukuu ya Pasaka siku ya kumi na ine (14) ya mwezi,+ wakati wa mangaribi, katika maeneo tambarare ya jangwa la Yeriko. 11 Na wakaanza kula mazao ya inchi siku yenye ilifuata Pasaka, ni kusema, mikate yenye haina chachu+ na nafaka zenye kukaangwa, siku ileile. 12 Na mana ikaacha kuanguka siku yenye ilifuata wakati walianza kula mazao fulani ya inchi; mana haikuanguka tena kwa ajili ya Waisraeli,+ lakini walianza kula mazao ya inchi ya Kanaani katika mwaka huo.+
13 Wakati Yoshua alikuwa karibu na Yeriko, aliinua macho na akaona mwanaume mumoja+ anasimama mbele yake na mwanaume huyo alikuwa na upanga katika mukono wake.+ Yoshua akaenda karibu naye na kumuuliza: “Uko upande wetu ao upande wa maadui wetu?” 14 Basi akamujibu: “Hapana, mimi ni mukubwa wa jeshi la Yehova, na nimefika sasa.”+ Basi Yoshua akaanguka uso chini na kuinama uso chini na kumuambia: “Bwana wangu anataka kumuambia mutumishi wake nini?” 15 Mukubwa wa jeshi la Yehova akamujibu Yoshua: “Vua viatu vyako kwenye miguu yako, kwa sababu mahali kwenye unasimama ni patakatifu.” Mara moja Yoshua akafanya vile.+